Na John Gagarini, Kibaha
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake mjini
Kibaha mwenyekiti wa mtaa huo Hamis Mwarizo alisema kuwa vijana hao watapewa
mafunzo hayo kutoka ofisi ya kata ili vijana waweze kujua namna ya kufuga
samaki.
Mwarizo alisema kuwa mafunzo hayo yatatolewa kwa vijana ambao
watakuwa wameunda vikundi ambavyo vitaendesha mradi huo ambao utatoa ajira kwa
vijana hao na watakuwa wakipeana zamu ya kusimamia.
“Lengo la mradi huo ni kuongeza ajira kwa vijana ambapo
asilimia 70 ya mapato yatakwenda kwenye kikundi na asilimia 30 yatakwenda
kwenye mtaa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii ya mtaa wetu,”
alisema Mwarizo.
Alisema kuwa kwa sasa tayari vijana 16 wameshapatikana kwa
ajili ya kuanzisha kikundi cha mwanzo na wengine wanaendelea kujiandikisha na
baadaye kikundi hicho kitasajiliwa ili kitambulike kisheria baada ya mradi huo
kupitishwa ana wananchi kwenye mkutano mkuu wa mtaa.
“Kundi la kwanza litaendesha kwa kipindi cha miaka 10 na
baadaye litapewa kundi lingine kwa ajili ya kuendeleza mradi huo ambao mbali ya
kuwapatia vijana ajira pia utaipatia jamii ya eneo hilo na maeneo jirani lishe
kwa ajili ya kuboresha afya,” alisema Mwarizo.
Katika hatua nyingine alisema kuwa kwa sasa wanaendelea na
taratibu za kulipima eneo la bwawa hilo ili kujua mipaka yake halisi ambapo
maji yake baada ya kupimwa yalibainika kuwa hayafai kwa kunywa kwani yana viluilui
ambavyo vinaweza kusababisha maradhi ya ugonjwa wa tumbo hivyo yatatumika kwa
ajili ya kulimia bustani pamoja na kufulia.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment