Na John Gagarini, Bagamoyo
Kutokana na shule hiyo kuwa kwenye mazingira magumu walimu
wengi wamekuwa hawako tayari kufundisha shule hiyo yenye wanafunzi 51 wa
kuanzia darasa la kwanza hadi la saba ambayo ni idadi ndogo kutokana na
mazingira hayo.
Akizungumza mbele ya Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dk Shukuru
Kawambwa, moja ya wakazi wa Kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina la Adam Rashid
alisema kuwa moja ya changamoto zinazowakabili ni pamoja na kutokuwa na usafiri
wa uhakika kutokana na ubovu wa miundombinu.
“Usafiri wa kutokana Kijijini hapa hadi makao makuu ya wilaya
ni kilometa 54 kwa njia ya barabara na usafiri wake ni pikipiki na gharama yake
ni kiasi cha shilingi 50,000 huku ule wa kutumia njia ya bahari mitumbwi
gharama yake ni kiasi cha shilingi 60,000 kwenda na kurudi,” alisema Rashid.
Alisema gharama hizo ni kubwa sana ajambo ambalo linawafanya
walimu washindwe kwenda kufundisha kutokana na mazingira hayo ambapo walimu hao
wawili wamekuwa wakipokezana kufundisha madarasa hayo.
“Wanafunzi wanafundishwa siku chache kutokana na walimu hao
wakati mwingine kutofika kabisa shuleni hali ambayo inawakatisha tamaa wanafunzi
na kusababisha kuwa na idadi ndogo ya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo,”
alisema Rashid.
Aidha aliiomba serikali kusaidia kupatikana kwa walimu ili
kukabiliana na hali ya wanafunzi hao kukosa masomo na kusababisha elimu kuwa
duni hali ambayo itatoa matokeo mabaya kwa wanafunzi wanaosoma kwenye shule
hiyo.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Makurunge Kabile Paulo alisema
kuwa walimu wengi wanashindwa kwenda kufundisha shuleni hapo kutokana na
mazingira magumu kwani hakuna huduma muhimu za jamii hivyo kushindwa kukaa
huko.
Paulo alisema kuwa baadhi ya huduma ambazo hazipo ni pamoja
na huduma ya afya kwani hakuna zahanati na huduma nyingine muhimu ambazo
huwabidi kuzifuata Bagamoyo au maeneo mengine jambo ambalo limekuwa
likiwagharimu.
Naye mbunge wa Jimbo hilo la Bagamoyo Dk Shukuru Kawambwa alisema
kuwa kweli hiyo ni changamoto ambayo inawakabili wakazi na walimu hao lakini
kwa kushirikiana na diwani wa kata hiyo watahakikisha wanaitatua.
Dk Kawambwa alisema kuwa Halmashauri itafanya mgao wa walimu
na ataiomba itoe kipaumbele kwa shule hiyo kwa kuwapatia walimu ili waweze
kwenda huko na kuongeza nguvu ya ufundishaji kwenye shule hiyo ambayo iko
pembezoni na kuwataka vijana waliosoma vyuo vya ualimu na ni wenyeji wa kata
hiyo kujitolea kwenda kufundisha kama njia mbadala ya upungufu huo wa walimu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment