Na John Gagarini, Kibaha
Pambano hilo ambalo lilipigwa kwenye ukumbi wa Container wilayani
Kibaha mkoani Pwani lilikuwa la vuta ni kuvute kutokana na umahiri wa mabondia
hao ambao hata hivyo walikuwa wakicheza kwa kuogopana kwa hofu ya kupoteza
ushindi.
Hata hivyo Tall alikuwa mjanja na kumzidi mbinu mpinzani wake
ambaye muda mwingi alikuwa akijihami kwa kuficha uso ili kukwepa ngumi kali
zilizokuwa zikirushwa na mpinzani wake.
Kwenye mapambano mengine Yasini Said alimpiga Julius Jackson,
Emanuel Endrew alimpiga Ramadhan Keshi, Ramadhan Kamage alimtwanga Kassim
Chuma, Salehe Muntari alimtwanga Aziz Pendeza, Hassan Mgosi alimtwanga Hemed
Hemed, Said Chino alimtwanga Idd Mgwinyo kwa TKO, huku Alfred Masinda na Nurdin
Mijibwa na Abdala Luwanje na Rajabu Mbena walitoka sare.
Akikabidhi mkanda huo kutoka TPBO mgeni rasmi katika pambano
hilo Selina Wilson Diwani wa Viti Maalumu aliwapongeza waandaaji wa pambano
hilo Butamanya Promotion kwa kuleta shindano hilo Kibaha.
Wilson alisema kuwa kuleta mchezo huo Kibaha ni kuibua vipaji
vilivyopo mikoani na kuwapa uzoefu mabondia wa hapa kuweza kujifunza mbinu za
ngumi.
“Mimi ni kijana na nimeona jinsi gani watu wanavyopenda
mchezo huu hapa Kibaha na mkoa wa Pwani nitahakikisha naunga mkono mchezo huu
na kupeleka halamashauri changamoto zinazowakabili ili ziweze kufanyiwa kazi
kwa lengo la kuboresha mchezo huu,” alisema Wilson.
Kwa upande wake bondia wa zamani Habibu Kinyogoli alisema
kuwa mabondia wa mkoa wa Pwani wameonyesha uwezo lakini walichokosa ni mbinu za
mapigano hivyo atajitolea kuwafundisha mabondia wa mkoa wa Pwani.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment