Na John Gagarini,
Kibaha
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Mjumbe wa Halmashauri Kuu
Taifa CCM (MNEC) Rugemalila Rutatina wakati akifungua mkutano wa Baraza la (UVCCM)
Kibaha Mjini na kusema kuwa kilimo endapo kitatumia vizuri kinaweza kuboresha
uchumi wao badala ya kumtegemea mtu kuwasaidia.
Rutatina alisema kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakiwafanya
vijana kama ngazi ya kupandia kwa kuwafanikishia mambo yao kisha kuwaacha bila
ya kuwajengea mazingira endelevu.
“Uzuri ni kwamba Chama pamoja na umoja wenu una mashamba
ambayo ni kama mtaji wa kuanzia kwa ajili ya kilimo cha kisasa ambacho kitakuwa
na tija kwa kutumia mipango mbalimbaili ya kuendeleza kilimo ikiwa ni pamoja na
Kilimo Kwanza,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa ili vijana wajikomboe wanapaswa kuanzisha miradi
ya kudumu kupitia rasilimali za chama ambazo endapo zingetumika ipasavyo
zingewaondoa vijana ndani ya chama na nje kuwa tegemezi katika kuendesha umoja
wao.
“Kilimo ni moja ya njia za kuwakomboa na kuacha kumtegemea
mtu lakini endapo mtaanzisha miradi ya kilimo itawaondoa huko mliko na
kuwafanya mjitegemee na kuendesha mambo yenu bila kuwa tegemezi,” alisema
Rutatina.
Aidha alisema kuwa kwa sasa fursa ni nyingi kwa vijana ikiwa
ni pamoja na mikopo kwa ajili kujikwamua kiuchumi na zana za kilimo kama
matrekta wanaweza kuazima kwenye chama.
Kwa upande wake katibu wa (UVCCM) Kibaha Mjini David Malecela
alisema kuwa wana maeneo mengi ambayo hata hivyo hayajaendelezwa hali ambayo
imesababisha watu kuyavamia.
Malecela alisema kuwa kwa sasa wako kwenye mipango ya
kuhakikisha wanayamiliki kisheria ili kukabiliana na watu wanaoyavamia maeneo
yao ambayo yakiendelezwa yatakuwa ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya umoja.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment