Na John Gagarini, Kibaha
Akizungumza na waandishi wa habari Sauda
Said alisema kuwa mvua inaponyesha maji yanajaa na kuwa kero kwa wateja
wanaofika kununua bidhaa.
Said alisema kuwa mbali ya kutokuwa
na mitaro pia soko hilo lina uchafu mwingi kutokana na kutotolewa kwa kipindi
kirefu na kusababisha uchafu huo kutoa harufu kali.
“Changamoto nyingine ni ukosefu wa
vifaa vya kufanyia usafi kwani mbali ya kutoa kiasi cha shilingi 200 kila siku
kama ushuru usafi haufanyiki ipasavyo hivyo kufanya mazingira ya soko kuwa
machafu,” alisema Said.
Alisema kuwa soko hili kwa sasa
linazalisha uchafu mwingi sana lakini tatizo ni halmashauri kushindwa kuondoa
uchafu kwa wakati na kufanya mlundikano wa uchafu kuwa mkubwa hali ambayo ina
hatarisha afya za watumiaji.
Naye mwenyekiti wa soko hilo Thobias
Michael alisema kuwa soko hilo ni kubwa kuliko masoko yote mkoani Pwani na
linahudumia wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya za Bagamoyo, Kibaha na
Kisarawe lakini mazingira yake si rafiki kwa watumiaji kutokana na uchafu
kukithiri.
Michael alisema kuwa waliahidiwa kuwa
watajengewa soko la kisasa ili kuondokana na changamoto wa soko hilo kwa sasa
kuwa dogo kutokana na kuwa na wafanyabiashara wengi.
“Kwa sasa idadi ya wafanyabiashara ni
450 ni kubwa sana na uzalishaji wa uchafu ni mkubwa sana lakini uzoaji taka
unakwenda taratibu sana na vifaa vya kufanyia usafi hakuna kwani hata gari la
kuzolea taka hakuna inawabidi Halmashauri kukodisha,” alisema Michael.
Kwa upande wake mganga mkuu wa
halmashauri ya wilaya ya Kibaha Dk Mariamu Maliwa alisema kuwa changamoto kubwa
iliyopo ni ukosefu wa gari la Halmashauri kwa ajili ya kuzolea uchafu lakini
wanakodisha gari kwa ajili ya kuzoa uchafu huo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment