Saturday, April 9, 2016

HOSPITALI YA BAGAMOYO YADAIWA M 220 NA MSD

Na John Gagarini, Kibaha
HOSPITALI ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani inakabiliwa na upungufu mkubwa wa dawa baada ya kukosa dawa kuanzia Januari mwaka huu kutoka Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kutokana na kudaiwa deni la shilingi milioni 220.
Hayo yamesemwa na mganga mkuu mfawidhi wa Hospitali hiyo Tumaini Byron wakati Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo kutembelea wagonjwa na kuwapa misaada mablimbali katiaka kusherehekea miaka 61 ya kuanzishwa Jumuiya hiyo.
Dk Byron amesema kuwa kutokana na deni hilo Hospitali hiyo kwa sasa imeonekana haikopesheki kutokana na deni hilo hivyo kunywimwa dawa hadi pale watakapolipa deni hilo la madawa.
Amesema wanakosa dawa kutokana na deni hilo kwani hata wakiomba hawapati hivyo kuwapa wakati mgumu wao pamoja na wagonjwa ambao hutakiwa kwenda kununua kwenye maduka ya madawa.
Aidha amesema kuwa wanashindwa kupewa au kukopeshwa vifaa tiba pamoja na vipimo mbalimbali ikiwa ni pamoja na vipimo vya wingi wa damu mkojo na malaria.
Amebainisha kuwa changamoto nyingine ni upungufu wa watumishi kwani kwa sasa wana watumishi 147 huku mahitaji yakiwa ni watumishi 250, vitanda vilivyopo ni 24 tu ambapo walau vingepatika japo 100 pamoja na uchakavu wa miundombinu ya umeme..
Kwa upande wake Mfamasia wa wilaya ya Bagamoyo Mohamed Makarai amesema kuwa mbali ya deni hilo la dawa pia MSD kutokuwa na dawa hivyo kuwa ni tatizo la nchi nzima kuanzia Oktoba na Novemba mwaka jana.
Makarai amesema kuwa serikali ilibadilisha mfumo wa kutoa tenda kwa wazabuni kwa ajili ya kuwapelekea dawa ambapo kwa sasa utaratibu umebadilika kwani hakutakuwa na kutoa tenda tena.
Amesema kuwa walikuwa wakichukua dawa kwa mali kauli na kutoa fedha baadaye hata hivyo walitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 100 ambapo moja ya changamoto ya kukosa fedha ni pamoja na kuwa na misamaa ikiwemo ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano, wazee, wajawazito na wale wenye magonjwa sugu hivyo serikali inapaswa kufidia pengo la makundi hayo ambayo yanapewa dawa bure.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment