Na John Gagarini, Kibaha
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisni kwake mjini Kibaha Dk Mariamu Maliwa alisema kuwa walifanikiwa
kuudhibiti kwa kufungia biashara za vyakula ambazo hazikutimiza masharti ya
afya.
Dk Maliwa alisema kuwa mgonjwa wa
mwisho aliyekuwa amelazwa kwenye kituo cha afya Mlandizi aliruhusiwa Aprili 21na
kufanya kutokuwa na mgonjwa Kipindupindu hata mmoja kutoka wagonjwa 115
waliogundulika kuwa na ugonjwa huo kuanzia mwezi Machi mwaka huu.
“Kwa zaidi ya kipindi cha wiki moja
tulizuia biashara zote za vyakula pamoja na matunda kwani tuliona kuwa sehemu
hizo zilikuwa chanzo cha ugonjwa huo na tulipozifungia wagonjwa walipungua
lakini kabla ya kuzifungia kulikuwa kunapatikana wagonjwa hadi nane kwa siku
moja hali amabayo ilikuwa ni mbaya sana,” alisema Dk Maliwa.
Alisema kuwa mbali ya kuzuia biashara
zote za vyakula pia walikuwa wakitoa elimu juu ya kujikinga na ugonjwa kuhamasisha
usafi kwenye maeneo ya biashara, majumbani na sehemu zinazozalisha uchafu kwa
wingi, uzoaji taka na kuhamasisha matumizi ya vyoo na kwa wale wasio na vyoo
wachimbe vyoo.
“Walikaidi kujenga vyoo tumewapeleka
mahakamani kwani wanaonekana kukaidi maagizo hayo kwani kujisaidia holela nako
kuna changngia kuenea kwa ugonjwa huu,” alisema Dk Maliwa.
Aidha alisema kuwa wagonjwa hao
walitoka kwenye maeneo mbalimbali ya Kibaha na nje ya Kibaha ambapo Ruvu
walikuja wagonjwa 63, Mlandizi 27, Visiga na Kongowe 13, Dutumi wanane,
Vingunguti na Mbezi wawili, Mzenga mmoja na wale waliokufa mmoja alifia
hospitali huku wawili wakifia majumbani.
Alisema kuwa wataruhusu wauzaji wa
vyakula mara watakapoona kuna mabadiliko ya ufuataji wa kanuni za afya mara
baada ya maofisa wa afya kupita na kujiridhisha kuwa vyanzo vyote vya ugonjwa
huo vimedhibitiwa na kuzingatiwa kwa kanuni za usafi na kuwataka wananchi
kuweka mazingira yao kwenye hali ya usafi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment