Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umebaini uwepo wa
watumishi hewa 25 wakiwemo walio kufa na wameipa serikali hasara kiasi cha
shilingi milioni 641,361,239 kutokana na kupokea mishahara pasipo kufanya kazi
ambalo ni kosa kisheria.
Akizungumza na gazeti hili ofisini
kwake mjini Kibaha mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evaristi Ndikilo alisema kuwa hasara
hiyo imebainika baada ya kufanya uhakiki kwa mara ya pili na kuona kuwa fedha
za mishahara ziliendelea kutolewa kwa watumishi hewa licha ya kutokuwepo
kazini.
Ndikilo alisema kuwa kati ya watumishi
19 ni wale waliokufa, waliostaafu na kuacha kazi lakini mishahara yao ilikuwa
ikiendelea kutoka na kusababisha hasara hiyo baada ya kuwafanyia uhakiki
watumishi 150 ili kuwatafuta watumishi hewa kutokana na agizo la Rais Dk John
Magufuli.
“Kundi hili la kwanza limeipa hasara
serikali kiasi cha shilingi milioni 69.1 huku wale ambao hawapo kabisa kazini
wameipa hasara serikali kiasi cha shilingi milioni 12.4 na watumishi watoro na
wale walio na mashauri ya kinidhamu wameipa hasara serikali kiasi cha shilingi
milioni 448.2,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa kati ya watumishi 150
waliohakikiwa 31 walibainika kuwa ni watoro na hawakujitokeza siku ya uhakiki
lakini walionekana kuwa ni watumishi halali kwa kuonyesha nyaraka muhimu huku
18 wakibainika kuwa ni watoro na wanamashauri ya kinidhamu lakini waliendelea
kulipwa mishahara.
“Watumishi 76 ambao ni watoro na wanamashauri
ya kinidhamu mishahara yao imesimamishwa ili wasiendee kuitia hasara serikali
wakati mashauri yao yanafanyiwa kazi,” alisema Ndikilo
Aidha alisema kuwa wakurugenzi wa
Halmashauri saba za wilaya walisema kuwa kiasi cha shilingi milioni 249,452,390
zilirudishwa Hazina na kuwataka wapeleke
viambatanisho kama ushahidi vinavyoonyesha kuwa walipeleka hazina na si maneno
matupu.
“Kama ni kweli kiasi hicho cha fedha
kilipelekwa hazina fedha ziltakazokuwa zimepotea ni kiasi cha zaidi ya shilingi
milioni 391.8 ambazo wanapaswa kuonyesha vielelezo vya kuzipeleka hazina kwani
maelezo hayo bado hayajaturidhisha wanatakiwa watupe uthibitisho ili tuliamini
hilo,” alisema Ndikilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment