Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Ushirika wa Mikopo cha
Shirika la Elimu Kibaha (KEC SACCOS LTD) kimeweza kutoa mikopo yenye thamani ya
shilingi bilioni 1.3 kwa wanachama wake kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisini kwake mwenyekiti wa Ushirika huo Kachingwe Kaselenge alisema kuwa mtaji
wao kwa sasa umefikia zaidi ya Bilioni 2.
Kaselenge alisema kuwa kwa sasa akiba
ndani ya chama imefikia bilioni 1.7 hisa zikiwa ni shilingi milioni 213.9 na
mkopo ni bilioni 2.2 ambapo kwa kila mwezi wanatoa mikopo yenye thamani ya
shilingi milioni 190.
“Tunamshukuru Mungu kwa sasa chama
kinaendelea vizuri kwani marejesho ni asilimia 98 hadi 99 ni wanachama wachache
tu ambao wanarejesha kwa matatizo nah ii inatokana na kuwa na mikopo sehemu
nyingine kwani sheria inasema mtumishi anapokopa lazima ibaki asilimia 1/3 ya mshahara
wake,” alisema Kaselenge.
Alisema kuwa wanachama wao ni
watumishi wa Shirika hilo lakini kutokana na kuwa na uwezo mkubwa wameongeza
wanachama ambao ni wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha (KDC) na wale
wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha (KTC) pamoja na wafanyakazi waofisi ya mkuu wa
mkoa.
“Chama chetu ni moja ya vyama
vikongwe hapa nchini kwani kwa mwaka huu kinatimiza miaka 50 tangu kunzishwa
kwake na tunajivunia mafanikio makubwa tuliyoyapata tangu kuanzishwa kwake
kwani wanachama wameweza kunufaika na mikopo inayotolewa kwani zaidi ya watu 5,040
wananufaika kwa siku na mikopo hii kwani wanachama wana miradi mbalimbali kama
ya mabasi, shule, ufugaji bodaboda na shughuli nyingine za kimaendeleo,”
alisema Kaselenge.
Aidha alisema kuwa mtaji walio nao ni
wa ndani kwani hawakopi kwenye mabenki kama baadhi ya vyama vinavyofanya hivyo
hawana deni lolote wale mkopo kwenye taasisi za kifedha ambapo hubidi kuweka
riba kubwa ili kufidia mikopo kwani kutokana na kuwa na mtaji wa ndani riba yao
ni asilimia 1.6.
“Kuna mikopo ya aina mbalimbali ikiwa
ni pamoja na ile ya Dharura kama vile misiba na majanga mbalimbali, Maendeleo
ikiwa ni pamoja na ujuenzi wa nyumba usafiri na ufugaji, Elimu kusoma na kusomesha
na mwanachama anapofariki familia inalipwa 300,000 na kama ni mwenza wake
analipwa 200,000 kwani asilimia moja ni bima ya mkopo na endapo anafariki deni
linakufa na fedha zake watalipwa ndugu bila ya kukatwa chochote kwani bima
itakuwa inalinda mkopo huo,” alisema Kaselenge.
Alibainisha kuwa wanakabiliwa na
changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwa na ushindani mkubwa toka kwenye
taasisi za kifedha ambazo zinawashawishi wanachama wao kujiunga nao kwa
kuwalipia madeni wanayodaiwa kwenye chama, sheria kutaka vyama hivyo kutolipa
kodi lakini wanaaambiwa walipe kodi na mwanachama anauwezo wa kukopa mara tatu
ya akiba yake aliyojiwekea kati ya shilingi milioni moja hadi milioni zaidi ya 20.
Ushirika huo ulianzishwa mwaka 1966
ukiwa na wanachama ukiwa na wanachama 66 lakini kwa sasa una wanachama 840 na kilianzishwa
kwa ajili ya kusaidiana na kusaidia
jamii inayowazunguka kwa kujitolea misaada sehemu mbalimbali kama hospitali na
maeneo yenye uhitaji.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment