Monday, June 3, 2024

WANAWAKE WA NDUMBWI WAASWA KUWAENZI WANAWAKE VINARA WAZALENDO







Ndugu Omary Abdul Punzi Afisa Mahusino wa Mradi wa Mazingira wa RAMATA (Rafiki wa Mazingira Tanzania) kutoka GBCF nchini Tanzania Tarehe 1.6.2024 awafunda wakina mama wa UWT tawi la Ndumbwi Mbezi Juu Kata ya Mbezi juu Wilaya ya Ubungo Jijini  Dar es Salaam.

Ndugu Omary Punzi aliwaelekeza kuwa Taifa hili limejengwa katika Misingi ya Kizalendo na walioitengeneza hii nchi ni wakina mama mfano Mwenyekiti wa kwanza Taifa wa Uwt  Sofia Kawawa na  Mwanasiasa Mashuhuri Bibi Titi Mohammed aliyejitoa kuchangia Mchango wake katika nchi hii.

Aliwaomba wanawake wamuunge mkono Mhe Dr Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta ya kutunza Mazingira na sekta nyingine za Kiuchumi.

Kwa kuzifuata hizi Falsa za TA TE TI TO TU
TA = Tangaza nchi yako bila uoga
TE= Tetea nchi yako bila uoga tusikubali idhalilike
TI= Timiza wajibu wako kwa kila hali
TO= Toa Ushauri kwa hali na Mali
TU= Tubu pale unapokosea

Pia aliwakumbisha sifa kuu ya kiongozi ni Kulalamikiwa na kuwa na Kiherehere chenye Manufaa kwa nchi yake

Naye Wakili msomi Godfrey Kizito Chambi alitoa mada ya Umuhimu wa wanawake katika kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mtaa wa mwaka 2024 na wasisite kwenda kujiandikisha katika Daftari la kudumu la kupiga kula  zoezi hilo  la kupata kitambulisho kwa ajili ya uchaguzi litakalo anza tarehe 1.7.2024 alisisitiza kuwa wasijitokeze kupokea au kutoa rushwa katika mchakato wa Uchaguzi utarudisha nyuma na kuwapata wagombea siyo sahihi na aliendelea kuwakumbusha wanawake hao juu ya Umuhimu wa kutunza Mazingira kwa kutumia rasilimali rafiki ili mazingira yetu yawe rafiki alisema shughuli za binadamu zinaongoza kuchochea kuharibu Mazingira.

Kwa upande Rehema Muya Mwenyekiti wa UWT Kata ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano huo alimwaga sifa kwa Mwenyekiti  na katibu wa tawi la ndumbwi kwa kufanya jambo kubwa la kuandaa mada hizo na kuwakusanya Wanawake wa UWT hii inaonesha kuwa sasa CCM inakwenda kupata Ushindi wa Kishindo kwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika uchaguzi wa 2024 na 2025

Naye Mhe Anna lukindo Diwani wa kata ya Mbezi Juu alisema kuwa Serikali Mhe Dk  Samia Suluhu Hassani imewasaidia wananchi wa Mbezi Juu kujenga Daraja Mito Miwili lengo kutatua kero ya muda mrefu ya kupita hapo Daraja  hilo likikamilika litakuwa chachu ya Maendeleo kutokana na Kasi inayofanywa na Mhe Josephat Gwajima na Timu nzima ya Viongozi wa Kinondoni sambamba na hilo alivutiwa na Mada za mkutano huo.

Katibu wa Tawi la Ndumbwi ndugu Witnes Ngowi alisema kuwa UWT katika Tawi hilo wamejipanga na kuhakikisha kuwa watashinda kwa kishindo katika Uchaguzi wa 2024 na  2025.

Kwa upande wa Catherine Mpangala Mwenyekiti wa Tawi la Ndumbwi alisema wameanda Mkutano huo   kwa lengo la kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi na kuwakumbusha watanzania kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa serikali ya Mitaa hivyo wasisite kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha katia Daftari la Kupiga kula litakalo anza Julai Mosi.

Aliwashukuru Bank ya NMB kuja kutoa Elimu ya Mikopo kwa wakina mama na na watoa mada ya Ujasiliamali kutoka kwa Estar Muhanga ,Mada Itifaki na Uzalendo iliyotolewa na ndugu Omary Punzi  na ile mada ya Utunzaji wa Mazingira na Umuhimu wa kushiriki Uchaguzi wa serikali za mita iliyotolewa na wakili Msomi Geoffrey Kizito 

Ndugu Catherine aliwawapongeza wanachama wa UWT kufika kwa wingi Sambamba na viongozi wa Chama kutoka Wilaya na kata kuja kushiriki Mkutano huo.

Sunday, June 2, 2024

CHAURU YACHAGUA VIONGOZI WAKE








CHAMA Cha Ushirika wa Umwagiliaji Mpunga Ruvu (CHAURU) cha Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimefanikiwa kumchagua Mchujuko Mchujuko kuwa mwenyekiti atakayeongoza kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwenye uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Ofisa Ushirika Halmashauri ya Chalinze alimtangaza Mchujuko aliyepata jumla ya kura 214 sawa na asilimia 91.8 kati ya kura 1,165 halali zikiwa 1,162 na kura zilizoharibika ni tatu ambapo mshindi alipaswa kupata angalau asilimia 50 ya kura.

Akitangaza washindi wa uchaguzi huo msimamizi huyo Raphael Kajale amemtangaza makamu wa mwenyekiti ni Otnel Mbura aliyepata kura 186 sawa na asilimia 79.8.

Kajale amewataja wagombea wengine kuwa ni Sade Mwakitalu alipata kura 173 sawa na asilimia 74, Renatha Mwaipopo alipata kura 171 sawa na asilimia 73.3 na Shea Bilali aliyepata kura 154 sawa na asilimia 67 hawa wote wataunda bodi ya ushirika huo.

Amewataja wajumbe wa kamati ya maadili waliochaguliwa ni Moses Polepole, Rajab Mfyome, Theresia Shayo, James Ole Njolay na Zuhura Matimbwa.

Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo mkuu wa uchaguzi uliompa ushindi mwenyekiti mpya Mchujuko amesema kuwa kikubwa atakachokifanya ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji kutoka tani tano za sasa hadi saba mpaka 10 na kukarabati miundombinu.

Awali mwenyekiti aliyemaliza muda wake Chacha Sadala akishukuru amesema pia wamefanikiwa kununua trekta na jembe lake ukarabati wa pampu nne kukarabati mashine mbili za kukoboa mpunga na tayari hekari 800 zimepandwa kati ya hekari 1,800 na hadi itakapofika Juni 30 wakulima wote watakuwa wamepanda mashamba yao.

Sunday, May 26, 2024

TAASISI ZINAZAZOUNGA MKONO CCM ZIKITUMIKIE CHAMA SIYO KUSUBIRI UTEUZI


WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wametakiwa wasizitumie taasisi mbalimbali zinazomuunga Mkono Rais na chama kama sehemu ya kupata teuzi za kuwa viongozi.

Aidha zimetakiwa zisitembee mifukoni na baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi bali wawaache waliopo madarakani wamalize muda wao wa uongozi.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Pwani David Mramba wakati wa mkutano na taasisi hizo.

Mramba amesema kuwa baadhi wanajiunga na taasisi hizo ili waonekane wachaguliwe kwenye nafasi mbalimbali za uongozi kwenye chama na serikali.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Ruvuma John Haule alizitaka taasisi hizo kuitumia vizuri mitandao ya kijamii kwa kuelezea mambo mazuri yanayofanywa na awamu ya sita.

Naye Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Morogoro Zangina Zangina amesema kuwa taasisi hizo zihamasishe wale wenye sifa wajiandae kugombea wakati utakapofika.

Thursday, May 23, 2024

CHONGELA AAPISHWA KUWA DIWANI

DIWANI wa Kata ya Msangani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Gunze Chongela ameapishwa baada ya kushinda uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Leonard Mlowe .

Chongela alikula kiapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Hamis Ally wakati wa kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha.

Gunze ameahidi kuwatumikia wananchi wa kata hiyo kwa kusimamia miradi ya maendeleo kupitia ilani ya CCM.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amemtaka diwani huyo kuebdeleza mazuri yaliyoachwa na mtangulizi wake ili kuleta maendeleo kwenye kata hiyo.

Wednesday, May 22, 2024

KILONGA CUP MBIONI KUTIMUA VUMBI

MAANDALIZI ya michuano ya soka ya Kilonga Cup msimu wa tano yameanza ambapo timu zimealikwa kushiriki michuano hiyo ambayo inayotarajia kutimua vumbi huko Bagamoyo Mkoani Pwani.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mjini Kibaha katibu wa mashindano hayo Idd Mpingo amesema kuwa michuano hiyo inatarajia kuanza mwezi Juni kwenye uwanja wa Mwanakalenge.

Mpingo amesema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri ambapo kwa sasa ni usajili wa timu zitakazoshiriki michuano hiyo ambapo timu ya Kiduli imethibitisha kushiriki michuano hiyo.

Amesema kuwa zawadi kwa mshindi mwaka huu zitakuwa nzuri ikilinganishwa na mwaka jana ambapo mwaka jana mshindi alijinyakulia milioni 3 na mshindi wa pili alijinyakulia milioni 1.5.

Kiingilio cha ushiriki kwa timu ni shilingi 150,000 ambapo pia zawadi zitatolewa kwa mchezaji bora, mfungaji bora na kipa bora lengo likiwa ni kuongeza hamasa kwa wachezaji.

Ametoa wito kwa vilabu ndani na nje ya Mkoa wa Pwani kujitokeza kushiriki michuano hiyo na wanawakaribisha wadhamini kujitokeza kudhamini michuano hiyo.

Ameishukuru serikali na vyama vya soka na waamuzi kwa ushirikiano wanaoutoa kwao katika kufanikisha michuano ambayo imeibua vipaji vingi vinavyotamba kwenye ligi mbalimbali nchini.

Tuesday, May 21, 2024



MWAJUMA Makuka ni jina maarufu kwenye Mtaa wa Msangani ambalo limetokana na uongozi wake thabiti akiwa ni mwanamke wa shoka kutokana na jinsi anavyopambana kuwaletea maendeleo wananchi anaowaongoza.

Ubora wake unatokana na umahiri wake wa kutekeleza majukumu yake kikamilifu bila ya kujali jinsi yake na kufanya baadhi ya mambo ambayo watangulizi wake ambao ni wanaume walishindwa katika uongozi wao.

Makuka ni mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Msangani Mtaa ulio jirani na kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Msangani kata ya Msangani Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani.

"Moja ya vitu vilivyokuwa vikiniumiza kama kiongozi ni kutokuwa na huduma ya uzalishaji mama wajawazito kwenye zahanati yetu ya Kata ya Msangani ambayo iko kwenye mtaa wa Msangani lakini changamoto hiyo iko mbioni kwisha kwani tayari vitanda viwili kwa ajili ya kuzalishia akinamama wajawazito kimepatikana",amesema Makuka.

Amesema kuwa mama wajawazito walikuwa wakipata huduma mbali na hivi sasa tayari vifaa vimeshaletwa ikiwa ni pamoja na vitanda vya kuzalishia na vifaa vingine ambapo huduma hizo zitaanza kutolewa hivi karibuni.

“Kwa kuanzia nyumba ya Mganga iko tayari ambapo kwa sasa imepauliwa baada ya serikali kutoa kiasi cha shilingi milioni 22 kinachosubiriwa ni kumalizia na mganga akiwepo huduma zitatolewa kwa saa 24 kwani kwa sasa huduma hutolewa muda wa kazi lakini baada ya hapo hufungwa hivyo endapo ikitokea changamoto ya mgonjwa huwabidi kumpeleka Tumbi au kituo cha afya Mkoani,”amesema Makuka.

Alisema kwa sasa huduma zote za vipimo zinatolewa lakini huduma za uzalishaji hazifanyiki hapo kutokana na kutokuwa na vifaa vya uzalishaji lakini kwa sasa huduma hizo zitatolewa hapo hali ambayo itawakomboa wanawake wakati wa kujifungua kwani huduma zitakuwa karibu na kupunguza changamoto za uzazi.

Alisema kuwa kutokana na huduma za afya kuwa karibu wanawake amabao wengi wanajishughulisha na shughuli za kiuchumi watakuwa na muda mwingi wa kufanya shughuli zao kwani wanwake wao ndiyo wanaotumia zaidi huduma za afya ambapo wao wakiumwa au watoto wao wakiumwa wao ndiyo huwapeleka watoto hospiatali tofauti na wanaume.

Mbali ya mafanikio ya ujenzi wa zahanati ambayo aliikuta kwenye hatua za awali vitu vingine ambavyo amefanikiwa na anajivunia ni pamoja na ujenzi wa madarasa mawali ya shule ya Msingi Msanagani, ofisi ya serikali ya mtaa ambayo ni ya kisasa ambayo ina vyumba vitatu na wanatafuta fedha kuongeza ili kupata ukumbi.

"Huduma ya maji nayo yalikuwa hayajasambaa kipindi naingia madarakani lakini kwa sasa sehemu kubwa ya mtaa ina huduma ya maji safi ambapo maeneo mawili tu ya Kiembeni na Mwanyundo ndiyo hayana maji pia aliwahi kuwapatia viti mwendo vinne watu wenye ulemavu katika mtaa wake,"amesema Makuka. 

Akizungumzia kuhusu masuala ya uongozi amesema kuwa Wazee wa Mtaa huo ndiyo walimwambia watampigania hivyo hakukutana na masuala ya ubaguzi kwani wazee hao walihakikisha hakuna anayeweza kutumia mila au desturi kumkwamisha katika harakati zake za kuwa kiongozi wanamheshimu sana hakuna mtu ambaye anaongelea masuala ya mapenzi.

“Nashukuru sana kwani kabla ya kuwa mwenyekiti wa mtaa nilikuwa katibu wa Kijiji na katibu wa ccm Msangani wakati huo hivyo sikukumbana na changamoto ya kubaguliwa au kunyanyaswa kijinsia kwani wazee wa kiume ndiyo waliopendekeza niwanie nafasi hiyo,’alisema Makuka.

Alisema kuwa aliingia kwenye uchaguzi wa ndani ya chama akiwa na washindani wenzake wanne wanaume na yeye mwanamke pekee lakini aliwashinda na kuwaacha mbali na yeye kuwa mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwashinda wanaume ambapo hata hivyo hakukuwa na uchaguzi wa vyama vingine baada ya vyama vya upinzani kujitoa kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa mwaka 2021.

Je mume wake alimsaidia vipi anasema alikuwa msaada mkubwa kwake kwani alikuwa akimsaidia na hakuwa na wivu naye na wakati akifanya shughuli za kisiasa alikuwa msaada kwake na alimuwezesha masuala mengi ili kuhakikisha shughuli zake zinakwenda vizuri bila ya kukwama na alikuwa msaada na anamkumbuka sana ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ni mwelewa na hakuwa na wivu kwani alikuwa akitambua kazi za viongozi.

"Nilikuwa nashirikiana naye vizuri kwenye baadhi ya majukumu ya kifamilia ili mimi niweze kutekeleza majukumu yangu ya kisiasa ambapo nikiwa sipo nyumbani mume wangu alikuwa akinisaidia kuhudumia familia kwani tuna watoto ambao walikuwa wakitakiwa kupata huduma mbalimbali,"amesema Makuka.

Pia hutenga muda kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya kifamilia na uongozi kwani huwa anatenga muda wake kwa ajili ya kuhudumia familia pale anapomaliza anahudumia wananchi wa mtaa wake na siasa haimfanyi ashindwe kuhudumia familia yake.

Anaelezea kuhusu changamoto ambayo wakati mwingine ni kikwazo kwa wanawake kwenye kuwania nafasi za uongozi ni rushwa ya ngono hakukumbana nayo kwa sababu wazee maarufu ndiyo walimshauri awanie nafasi hiyo hivyo hakukumbana na kikwzo cha kuombwa rushwa ya ngono kwa hilo anamshukuru Mungu kwani hakuna aliyeweza kumtamkia kuhusu masuala ya ngono japokuwa mambo hayo yapo na upande wa mila na desturi ambazo zilikuwa zikiwakandamiza wanawake kadri muda unavyokwenda zinapungua.

Alisema anawashukuru wananchi wakiwemo wanaume ambapo hawa mbezi kwa kusema kauli au misemo mbalimbali kwani anawaongoza anashirikiana nao vizuri kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na shughuli za kujitolea na wanawake ndiyo wanaojitokeza kwa wingi kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo. 

Aliongeza kuwa ushauri wake kwa viongozi wanwake na wale wanaotarajia kugombea jambo kubwa wanalotakiwa kulifanya ni kuwa na ujasiri na kutokuwa na woga japo yeye alipoambiwa agombee uenyekiti alikuwa na woga lakini alijipa moyo na kukabili changamoto za uongozi.

Moja ya wakazi wa mtaa huo Ahmed Majengo alisema mwenyekiti wao ni shupavu licha ya kuwa ni mwanamke kwani anapambana sana katika kuhakikisha analeta maendeleo kwenye mtaa wake na pia anakabili changamoto ikiwa ni pamoja na dawa za kulevya na biashara ya wanawake kujiuza ambayo inaongezeka.

Majengo alisema kuwa kitu kinachomsaidia ni mtiifu na anayependa ukweli ambapo hupenda kukemea bilaya kuogopa ambapo matukio hata ya wizi yanapungua na uhalifu kwa ujumla siyo wa kutisha kutokana na hatua anazochukua kwani akijua kuna kijana analeta shida na akijiridhisha anamkamata na kumchukulia hatua.

Naye Amina Matima alisema kuwa mwenyekiti wao anafanyakazi haijalishi kuwa ni usiku au muda gani yeye anafanyakazi bila ya woga na hata ikifika hatua ya kuchangia mfano ujenzi wowote anachangia bila ya shida yoyote.

Salum Abdala anasema kuwa anajua changamoto nyingi na anazikabili licha ya kuwa yeye ni mwanamke haimfanyi kushindwa kuongoza na anasimamia miradi mingi ya maendeleo imefanikiwa kutokana na misimamo yake kwani hakubali kuyumbishwa na mtu yoyote.

Abdala anasema kuwa hawajutuii kumchagua kwani hata kubeba tofali anabeba kufukia mashimo barabarani anafanya kazi zote kama mwanaume kwake hakuna mfumo dume kwani anapambana bila ya hofu yoyote.

Makuka alianza siasa miaka ya 90 ambapo kabla ya kushika nafasi hiyo ya uenyekiti, katibu mwenezi wa kata hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu kuwa makamu mwenyekiti wa chama cha ushirika cha msingi cha Msangani, pia aliwahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya shule ya Msingi Msangani na ana watoto watatu ambao wote hakuna anayefuata nyayo zake.








Saturday, May 18, 2024

JKT RUVU YAZINDUA BUSTANI YA WANYAMAPORI

MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amezindua bustani ya Wanyamapori ya Kikosi cha  Jeshi cha Ruvu JKT (Wildlife).

John akizindua bustani hiyo iliyopo kwenye eneo la Kikosi  cha 832 KJ Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani amewataka wananchi kujitokeza kwenda kuangalia wanyama ambao sasa wanapatikana karibu. 

Amesema uwepo wa Mbuga hiyo mbali ya kuwapunguzia gharama wananchi wanaotaka kuangalia wanyama pia itaongeza mapato ya Kikosi hicho na serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi hicho Kanali Peter Mnyani amesema kuwa wameanza na wanyama wachache lakini watawaongeza ili wawe wengi ambapo watakuwa na fursa ya kupiga picha na wanyama hao.

Mnyani amesema kuwa mwezi Juni wataongeza wanyama wakiwemo Simba ili kuongeza idadi ya wanyama na eneo hilo lina ukubwa wa hekari 70.

Amesema mbali ya kufuga wanyama hao pia wanatunza mazingira kutokana na eneo hilo kuwa na mazingira mazuri na ya asili.