Ndugu Omary Abdul Punzi Afisa Mahusino wa Mradi wa Mazingira wa RAMATA (Rafiki wa Mazingira Tanzania) kutoka GBCF nchini Tanzania Tarehe 1.6.2024 awafunda wakina mama wa UWT tawi la Ndumbwi Mbezi Juu Kata ya Mbezi juu Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Monday, June 3, 2024
WANAWAKE WA NDUMBWI WAASWA KUWAENZI WANAWAKE VINARA WAZALENDO
Ndugu Omary Abdul Punzi Afisa Mahusino wa Mradi wa Mazingira wa RAMATA (Rafiki wa Mazingira Tanzania) kutoka GBCF nchini Tanzania Tarehe 1.6.2024 awafunda wakina mama wa UWT tawi la Ndumbwi Mbezi Juu Kata ya Mbezi juu Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Sunday, June 2, 2024
CHAURU YACHAGUA VIONGOZI WAKE
CHAMA Cha Ushirika wa Umwagiliaji Mpunga Ruvu (CHAURU) cha Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimefanikiwa kumchagua Mchujuko Mchujuko kuwa mwenyekiti atakayeongoza kwa kipindi cha miaka mitano.
Kwenye uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Ofisa Ushirika Halmashauri ya Chalinze alimtangaza Mchujuko aliyepata jumla ya kura 214 sawa na asilimia 91.8 kati ya kura 1,165 halali zikiwa 1,162 na kura zilizoharibika ni tatu ambapo mshindi alipaswa kupata angalau asilimia 50 ya kura.
Akitangaza washindi wa uchaguzi huo msimamizi huyo Raphael Kajale amemtangaza makamu wa mwenyekiti ni Otnel Mbura aliyepata kura 186 sawa na asilimia 79.8.
Kajale amewataja wagombea wengine kuwa ni Sade Mwakitalu alipata kura 173 sawa na asilimia 74, Renatha Mwaipopo alipata kura 171 sawa na asilimia 73.3 na Shea Bilali aliyepata kura 154 sawa na asilimia 67 hawa wote wataunda bodi ya ushirika huo.
Amewataja wajumbe wa kamati ya maadili waliochaguliwa ni Moses Polepole, Rajab Mfyome, Theresia Shayo, James Ole Njolay na Zuhura Matimbwa.
Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo mkuu wa uchaguzi uliompa ushindi mwenyekiti mpya Mchujuko amesema kuwa kikubwa atakachokifanya ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji kutoka tani tano za sasa hadi saba mpaka 10 na kukarabati miundombinu.
Awali mwenyekiti aliyemaliza muda wake Chacha Sadala akishukuru amesema pia wamefanikiwa kununua trekta na jembe lake ukarabati wa pampu nne kukarabati mashine mbili za kukoboa mpunga na tayari hekari 800 zimepandwa kati ya hekari 1,800 na hadi itakapofika Juni 30 wakulima wote watakuwa wamepanda mashamba yao.
Sunday, May 26, 2024
TAASISI ZINAZAZOUNGA MKONO CCM ZIKITUMIKIE CHAMA SIYO KUSUBIRI UTEUZI
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wametakiwa wasizitumie taasisi mbalimbali zinazomuunga Mkono Rais na chama kama sehemu ya kupata teuzi za kuwa viongozi.
Aidha zimetakiwa zisitembee mifukoni na baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi bali wawaache waliopo madarakani wamalize muda wao wa uongozi.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Pwani David Mramba wakati wa mkutano na taasisi hizo.
Mramba amesema kuwa baadhi wanajiunga na taasisi hizo ili waonekane wachaguliwe kwenye nafasi mbalimbali za uongozi kwenye chama na serikali.
Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Ruvuma John Haule alizitaka taasisi hizo kuitumia vizuri mitandao ya kijamii kwa kuelezea mambo mazuri yanayofanywa na awamu ya sita.
Naye Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Morogoro Zangina Zangina amesema kuwa taasisi hizo zihamasishe wale wenye sifa wajiandae kugombea wakati utakapofika.
Thursday, May 23, 2024
CHONGELA AAPISHWA KUWA DIWANI
Wednesday, May 22, 2024
KILONGA CUP MBIONI KUTIMUA VUMBI
Tuesday, May 21, 2024
Saturday, May 18, 2024
JKT RUVU YAZINDUA BUSTANI YA WANYAMAPORI
MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amezindua bustani ya Wanyamapori ya Kikosi cha Jeshi cha Ruvu JKT (Wildlife).
John akizindua bustani hiyo iliyopo kwenye eneo la Kikosi cha 832 KJ Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani amewataka wananchi kujitokeza kwenda kuangalia wanyama ambao sasa wanapatikana karibu.
Amesema uwepo wa Mbuga hiyo mbali ya kuwapunguzia gharama wananchi wanaotaka kuangalia wanyama pia itaongeza mapato ya Kikosi hicho na serikali.
Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi hicho Kanali Peter Mnyani amesema kuwa wameanza na wanyama wachache lakini watawaongeza ili wawe wengi ambapo watakuwa na fursa ya kupiga picha na wanyama hao.
Mnyani amesema kuwa mwezi Juni wataongeza wanyama wakiwemo Simba ili kuongeza idadi ya wanyama na eneo hilo lina ukubwa wa hekari 70.
Amesema mbali ya kufuga wanyama hao pia wanatunza mazingira kutokana na eneo hilo kuwa na mazingira mazuri na ya asili.