MAKAMU wa Rais wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Philip Mpango ameitaka mikoa nchini kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo mabaraza ya biashara ya mikoa na kutowatumia wakati wa kuomba michango ya shughuli za maendeleo.
Tuesday, August 22, 2023
MAKAM WA RAIS DK MPANGO ATAKA WAKUU WA MIKOA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI
Sunday, August 20, 2023
NYERERE SUPER CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI TAREHE 23.9.2023
Katika kundeleza FIKRA za mwasisi wetu wa Taifa Mwalimu Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiongozwa na Katibu wa Taasisi hiyo Ndugu Omary Punzi Tarehe 20.8.2023 imefanya Hitimisho la kikao Cha maandalizi ya Mashindano ya NYERERE SUPER CUP yatakaotimua vumbi Tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023.Mashindano hayo yatashirikisha Wilaya Mbili wilaya ya KIBITI na RUFIJI Kwa Timu 12 Timu sita kutoka kundi A (KIBITI)Timu shiriki Bungu,Jaribu,Mtawanya, Kibiti,Mchukwi,Dimani,na upande wa kundi B Rufiji timu zinazoshiriki Ngorongo,Utete,.Mgomba, Muhoro,Umwe na Mkongo vikao hivyo vyote viwili Cha Tarehe 19.8.2023 na 20.8.2023 vilikuwa na agenda ya Kuandaa kanuni na ratiba ya kuanza Usajili wa wachezaji,wajumbe wote walikubaliana Dirisha la Usajili lifunguliwe tarehe 23.8.2023 na kuisha 13.8.2023 inatoa shukrani Kwa NSSF na Chuo Cha Afya St David college Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na wilaya ya Kibiti na Rufiji,Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji,Chama Cha Mpira KIBITI na RUFIJI
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATOA SHUKRANI KWA WADAU MAANDALIZI NYERERE SUPER CUP
Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani inatoa shukrani Kwa Viongozi wote mliofanikisha safari yetu ya maandalizi ya NYERERE SUPER CUP Taasisi inashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti na Rufiji 3.Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji 4.Chama Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 5.Chama cha Mpira wilaya Kibiti na Rufiji 6.Mdhamini Nssf na St David college Chuo Cha Afya kimara temboni,Madiwani wa Kibiti na Rufiji kuruhusu Viongozi wao kuhudhuria kikao na washiriki waliohudhuria UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA
*LYIDENGE ATAKA WAFANYAKAZI WA MIRADI KUWA NA NIDHAMU*
Amebainisha hayo leo Agosti 20 alipotembela mradi huo wakati akizungumza na wafanyakazi hao kuona kama wana changamoto zozote za kiusalama.
SSP Lyidenge aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa wameaminiwa na serikali kufanya kazi hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu na wasijihusishe na vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa vitendea kazi na kuwataka wawe walinzi wa kwanza wa vifaa hivyo.
Sambamba na hayo SSP Lyidenge aliwasihi viongozi wa mradi huo kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi ikiwemo lugha nzuri yenye staha ili kuongeza hamasa ya utendaji na kufikia malengo ya mradi kwa wakati uliokusudiwa.
"Niwaombe viongozi kuwatia moyo na kuwa na lugha shawishi kwa mnao wasimamia ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, lugha zisizo na staha huwavunja moyo watendaji na kujikuta ikiwapunguzia morali ya kujituma".
Sote tunatambua umuhimu wa mradi huu utakavyochochea maendeleo ya kiuchumi kwa kwa wakazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla” alisema Lyidenge
CCM WAASWA KUFUATA UTARATIBU
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wanaotoa misaada na kufanya shughuli za maendeleo wametakiwa kufuata utaratibu ili kuepusha mkanganyiko na viongozi waliochaguliwa na wananchi.
COREFA YAZINDUA KITUO CHA SOKA KWA VIJANA KIBAHA
JAMII IMETAKIWA KUPANDA MITI KWENYE MIRADI ILI KUHIFADHI MAZINGIRA
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Switbert Mkama ameitaka jamii kupanda miti kuzunguka maeneo yenye miradi ili kuhifadhi mazingira na kuifanya kuwa endelevu.
Amesema hayo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi ya Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mfumo Mfumo Ikolojia Vijijini (EBARR) katika Wilaya ya Kaskazini ‘A‘ Mkoa wa Kaskazini, Unguja - Zanzibar.
Akikagua visima, ujenzi wa majengo ya vituo vya wajasiriamali wa ufugaji, ushonaji, utengenezaji wa sabuni pamoja na vitalu nyumba katika Shehia za Jugakuu, Mbuyutende na Kijini, Dkt. Mkama amesema ameridhishwa hatua iliyofikiwa.
Aidha, aliwahimiza viongozi wakiwemo masheha wa shehia hizo ambazo zimefaidika na miradi ya visima kuwasimamia wananchi kupanda miti na kuimwagilia.
“Binafsi nimeridhishwa na namna mnavyosimamia miradi hii na nawapongeza masheha kwa kuisimamia na wananchi kwa kuipokea na kushiriki kikamilkfu katika kuitekeleza, niwaombe mhakikishe inaendelea kuwa na ubora ule ule,“ amesisitiza.
Kwa vile ujenzi wa majengo ya wajasiriamali wa ushonaji na uzalishaji wa sabuni utahusisha mashine na vifaa, Dkt. Mkama alisema ni muhimu kuwepo na mpango mkakati ili mradi uwe endelevu hata pale utakapokwisha muda wake.
Alisema vyerehani vitakavyotolewa pamoja na vifaa vingine vikiwemo taa na mabomba ya maji vitahitaji matengenezo madogo madogo na kulipiwa umeme hivyo wanajamii waangalie namna ya kuuhudumia bila kusubiri serikali.