Sunday, August 9, 2026

WATANZANIA WAASWA KUSAIDIA ELIMU WATOTO WA VITUO WENYE UHITAJI





JAMII imeaswa kugharamia suala la elimu kwenye vituo vya watoto wenye uhitaji ili kwa kutatua changamoto za kielimu kwa watoto hao waweze  kutimiza ndoto zao.

Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.

Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.

"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.

Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.

"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.

Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.

Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.

Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.

Thursday, August 6, 2026

AHUKUMIWA MAISHA JELA KWA ULAWITI MWINGINE MIAKA 20 NA FAINI M 1 KWA KUDHALILISHA MTOTO

SALIM Mang'ombe (29) mkazi wa Wilaya ya Bagamoyo amehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kulawiti mtoto mwenye umri wa miaka (10) ambaye alikuwa ni jirani yake.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwezi Julai.

Kwenye tukio lingine Salim Masanja (33) Mkazi wa Wilayani Kibaha amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni moja kwa tuhuma za kumdhalilisha mtoto wa kike (6).

Morcase amesema kuwa mshtakiwa huyo ni baba mdogo wa mhanga ambaye alikuwa akiishi naye nyumbani kwake na kesi hizo ni za ukatili wa kijinsia.

Amesema kuwa kesi zilizofikishwa mahakamani kwa kipindi hicho zilikuwa 117 huku kesi 63 zilisikilizwa na kumalizika ambapo kesi 48 zimepata mafanikio.

Amesema kuwa jamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanapaswa kushirikiana ili kukabiliana na vitendo vya ukatili kwa watoto.

Wednesday, August 5, 2026

POLISI YAWAREJESHA SHULENI WANAFUNZI 114

JESHI la Polisi Mkoani Pwani limefanikisha kuwarejesha Shuleni wanafunzi 114 ambao walishindwa kuripoti shule kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase amesema kuwa jumla ya wanafunzi 573 walikuwa hawajaripoti shuleni.

Morcase amesema kuwa kati ya wanafunzi hao ambao hawakuripoti Shule za Msingi walikuwa 251 na wa Sekondari walikuwa ni 322 ambao walibainika katika kipindi hicho licha ya kuwa wanafunzi hao kuwa na wa miaka tofauti tofauti.

Amesema kuwa changamoto nyingine ni mimba za utotoni ukosefu wa mahitaji ya msingi kama vile sare za Shule na madaftari  na changamoto za kiafya na kiuchumi.

Amewataka wazazi na walezi kushirikina na viongozi wa dini na wa kiserikali katika kupambana na viashiria vya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ndani ya jamii.


Saturday, August 1, 2026

HALMASHAURI YA MANISPAA KIBAHA YAZINDUA MAGARI MRADI WA (TACTIC)

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imezindua magari mawili yatakayotumika kwenye mradi wa ujenzi wa barabara za lami kwenye kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu ya Miji na Vijiji (TACTIC) wenye thamani ya shilingi bilioni 19.8

Akindua magari hayo ambayo yatatumika kwenye mradi huo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema magari hayo yatawezesha utekelezaji mradi kuwa rahisi.

Mawazo alisema kuwa magari hayo ni moja ya makubaliano mkataba wa mradi huo na yakimaliza kutumika yanarudi Halmashauri kwa ajili ya shughuli zingine za kutoa huduma kwa wananchi kupitia wataalamu.

"Mradi huu unaenda kuleta mabadiliko chanya na uboreshaji wa miundo mbinu mbalimbali ya Manispaa ya Kibaha na kuwa na mwonekano mzuri na kuleta urahisi wa usafiri na usafirishaji,"alisema Mawazo.

Alisema kuwa katika miradi hiyo ya Tactic wanakwenda kuitekeleza kwa ubora zaidi na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaenda kuwa ya kwanza na mfano kwa Halmashauri zingine katika utekelezaji na usimamizi wa miradi hii nchini.

"Wananchi wa Kibaha wanapaswa kujivunia na kutangaza maendeleo yanayofanywa na serikali hii kwani Manispaa ya Kibaha ina neemeka na dira ya Rais na mmeona maendeleo yanavyokuja kwa kasi na tutakuwa Halmashauri ya mfano kwa kila kitu,"alisema Mawazo.

Akisoma taarifa ya mradi huo Ofisa Utumishi  Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuleta miradi yenye fedha nyingi na usimamizi mzuri wa viongozi wa Wilaya na Mkoa kwa utekelezaji wa Ilani kwa maslahi ya Manispaa ya Kibaha.

Mlela alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri wa masuala mbalimbali ya mapato usimamizi wa miradi pamoja na tija katika utendaji wa Halmashauri.

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha imepokea magari hayo mawili kutoka kwenye Mkataba wa mradi wa Tactic ambapo yatatumika katika mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 4.8 Tughe-Anglikana barabara ya Picha ya Ndege - Lulanzi na soko la Loliondo Mnarani.

MADARASA JANJA KUPUNGUZA CHANGAMOTO UPUNGUFU WA WALIMU NCHINI

MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo amezindua Darasa Janja (Live Teaching) Shule ya Sekondari Bundikani na kuiomba Serikali kuanzisha madarasa hayo kote nchini ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Mawazo alitoa ombi hilo wakati akizindua darasa hilo shuleni hapo ambapo shule hiyo ni Sekondari ya Kata ya Maili Moja Wilayani Kibaha na kuwa darasa janja yatasaidia kuwafanya wanafunzi kuwa na ari ya kusoma.

Amesema kuwa mwalimu mmoja anayefundisha kupitia darasa janja moja anaweza kufundisha shule zote ambazo zitakuwa zimeunganishwa kwenye mfumo huo wa darasa la aina hiyo kote nchini kwa wakati mmoja.

"Mfumo huu wa darasa janja ni mzuri kwa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa walimu kwani mwalimu mmoja anauwezo kufundisha shule zote ambazo zimeunganishwa kwenye mfumo huo,"amesema Nicas.

Aidha amesema kuwa pia mbali ya kufundisha wakati mmoja pia yale aliyofundisha mwalimu huyo yanaweza kurekodiwa na kuwafundisha wanafunzi wengine kwa ubora ule ule.

"Jambo zuri ni kuwa walimu wote wanaofundisha kupitia madarasa janja wote ni wale wenye umahiri wa kufundisha hivyo watawajengea wanafunzi uwezo mkubwa wa kujifunza na kupata ujuzi,"amesema Mawazo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela amesema kuwa wataendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa janja kwenye shule za sekondari.

Mlela amesema kuwa wameendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga shule tatu za mfumo wa Kiingereza na shule hizo zote zimejengwa kutokana na fedha za mapato ya ndani na kutengeneza madawati viti na meza 4,000 kwa shule za msingi na sekondari.

Naye Mkuu wa Shule ya Bundikani Bernard Muyenjwa amesema kuwa wanaishukuru Serikali kwa kuwapatia darasa hilo janja kwani litarahisisha katika ufundishaji na kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu.

Muyenjwa amesema kuwa kuanzishwa kwa darasa janja hilo shuleni kwao kutasaidia walimu kufundisha bila ya kuchoka wala kutumia nguvu kubwa na kuwapa wanafunzi umahiri na kujua namna ya kutumia teknolojia.

mwisho

Thursday, July 30, 2026

BINTI ATUHUMIWA KUMUUA MAMA YAKE MZAZI KWA KUMKATAZA KWENDA KWENYE SHEREHE YA KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAFIKI YAKE.

BINTI mwenye umri wa miaka (16) Mkulima na Mkazi wa Kijiji cha Msoga Chalinze Wilayani Bagamoyo anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mama yake mzazi baada ya kumzuia kuhudhuria sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa rafiki yake.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase kuwa Mama yake Hadija Shaha ambaye ni mlemavu wa miguu.

Morcase amesema kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 mwaka huu majira ya saa 5:00 usiku huko katika Kijiji cha Msoga Chalinze ambapo mtuhumiwa alimuua mama yake kwa kumchoma kwa kitu chenye ncha kali.

"Chanzo cha tukio hilo ni kuwa marehemu alimkataza binti yake Rahma Tito kwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake (birthday party) iliyokuwa inafanyika maeneo ya jirani na Hospitali ya Msoga,"amesema Morcase. 

Amesema kuwa baada ya binti huyo kuzuiwa kwenda kwenye sherehe alianza kumshambulia mama yake kisha kumchoma na kitu chenye ncha kali kichwani.

"Julai 29 mwaka huu  majira ya saa 1:00 asubuhi fundi ujenzi alifika nyumbani kwa Shaha kufuata mfuko wa saruji na fedha yake ya ujenzi ndipo alipogonga mlango na kufunguliwa na binti  wa marehemu jirani huyo aligundua kuna mwili wa marehemu ukiwa umelala sakafuni ukiwa na majeraha kichwani yanayotiririsha damu,"amesema Morcase.

Amesema kuwa mwili wa marehemu ulipelekwa Hospitali ya Msoga ambapo ulifanyiwa uchunguzi wa daktari kisha ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi. 

"Mara baada ya upelelezi kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo na Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linatoa rai kwa wazazi walezi viongozi wa dini na jamii kwa ujumla kushirikiana katika malezi ya watoto,"amesema Morcase.

Aidha amesema kuwa ushirikiano huo utasaidia kubaini tabia na changamoto za watoto wao kwenye makuzi ili hatua zichukuliwe mapema kabla hayajatokea madhara yoyote.

Tuesday, July 28, 2026

MAGANYA ATAKA WANACHAMA WASICHAFUANE.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Fadhili Maganya amewataka wanachama waache kuchafuana kuelekea uchaguzi wa ndani mwakani.

Maganya aliyasema hayo Mjini Kibaha alipokuwa  akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo pamoja na wanachama wa CCM Kibaha Mjini wakati wa ziara yake kutembelea Mkoa wa Pwani kukagua uhai wa chama na miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa chama hakina shida nao bali wafuate miongozo na utaratibu wa chama kama unavyoelekeza.

"Mwakani tunaingia kwenye uchaguzi wa ndani baadhi wameanza kuchafuana tusikubali hali hiyo asitokee mtu wa kutoa maelekezo bali chama ndiyo kinatoa maelekezo,"alisema Maganya.

Aidha alisema kuwa watu wanaanza kukinzana na uchaguzi wa mwakani na unabeba taswira ya uchaguzi wa 2030 hivyo chama kitangulizwe mbele na siyo mtu.

"Tuwaacheni walioko madarakani wafanye kazi kwani muda wa uchaguzi bado watu wasubiri hadi muda utakapofika,"alisema Maganya.

Alibainisha kuwa kuna baadhi ya watu wanasiasa wa upinzani na wanaharakati wamekuwa wakibeza na kutoa lugha za maudhi na kudhalilisha wasipewe nafasi kwani wakidai eti serilali iliyopo ni haramu.

"Tusiruhusu tabia hiyo kwani Rais Dk Samia Suluhu anafanya kazi kubwa kwa kushirikiana na chama chake kwani Tume ya Uchaguzi iliita vyama vyote na kutaka visaini sheria za uchaguzi lakini baadhi vilikataa,"alisema Maganya.

Aliongeza kuwa uchaguzi ulikuwa wazi kwa kila chama na viongozi walichaguliwa kwa utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi hivyo havina haja ya kulalamika.

"Kamati za siasa za chama zinapaswa kutatua migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na serikali ambayo inafanya kazi kubwa kutatua migogoro hiyo,"alisema Maganya.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya (CCM-NEC) kupitia Jumuiya ya Wazazi na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa alisema kuwa Jumuiya imekuwa mstari wa mbele kuimarisha chama.

Jumaa alisema kuwa kwa sasa Jumuiya hiyo imeimarika sana na kuwa mhimili mkubwa wa chama katika utekelezaji wa ilani.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa Jumuiya ya Wazazi imefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa ilani.

Koka alisema kuwa kwenye uchaguzi Mkuu Jumuiya hiyo iliongoza kwa kupiga kura na kuufanya Mkoa wa Pwani kuongoza kwenye suala la kura.

Awali akitoa taarifa ya Wilaya Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa alisema kuwa uptikanaji wa huduma kwa sasa kwa wananchi ni asilimia 98.

Magogwa alisema kuwa Hslmashauri ya Manispaa imekuwa ikifanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ambapo asilimia 60 yanatokana kodi na ushuru mbalimbali wa huduma.

Alisema kuwa ujenzi wa barabara ya njia sita kutoka Maili Moja hadi Picha ya Ndege unatarajia kuanza na barabara kwa ajili ya magari ya mizigo nao utaanzia Picha ya Ndege.

ZAHANATI YA KILIMAHEWA YAWAPUNGUZIA UMBALI WANANCHI KUPATA HUDUMA

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Fadhili Maganya amepongeza ujenzi wa Zahanati ya Kilimahewa Kata ya Tangini Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kuitaka kuweka dirisha la Wazee ili waweze kupata huduma kwa urahisi wakati wa kupata matibabu.

Maganya ameysema hayo Mjini Kibaha alipotembelea Zahanati hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mkoa wa Pwani kuimarisha uhai wa chama na kutembelea miradi ya maendeleo na kusema kuwa ujenzi huo ni wa mapato ya ndani.

Amesema kuwa wazee waliambiwa kuwa watatengewa dirisha kwa ajili ya kuwapatia huduma hivyo ni vema dirisha hilo likawepo kwa ajili ya kuwahudumia na siyo kusema kuwa wapishwe ili wahudumiwa bali wawe na dirisha lao maalum.

"Tuliahidi kuwa tutawawekea dirisha lao maalum kwa ajili ya kupata huduma hivyo Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha lazima ihakikishe inawawekea dirisha lao ili wapate huduma za afya kwani wao lazima wahudumiwe vizuri pasipokuwa na changamoto,"amesema Maganya. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Catherine Saguti alisema kuwa lengo ni kurahisha upatikanaji wa huduma za afya kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na ulianzishwa kutokana ongezeko la mahitaji ya huduma za afya kwenye eneo hilo.

Saguti amesema kuwa ujenzi ulianza Juni 2024 Halamshauri ilipokea kiasi cha shilingi milioni 233.5 na wananchi walichangia kiasi cha shilingi milioni 1 na shilingi milioni 50 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba hivyo kufanya gharama za mradi kuwa shilingi milioni 284.6.

Amesema kuwa serikali imeajiri wauguzi 32 ambapo Zahanati hiyo ina watumishi saba wanaotoa huduma na Zahanati hiyo imepatiwa watumishi wawili hivyo hakuna upungufu wa watumishi.

Zahanati ilianza kutoa huduma Aprili 2026 na hadi sasa imeshatoa huduma kwa watu 1,103 na inatoa huduma mbalimbali.


Monday, July 27, 2026

HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA YAPONGEZWA UKUSANYAJI MAPATO NA UTOAJI MIKOPO KWA VIKUNDI

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Fadhili Maganya ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuweza kufanikisha ukusanyaji wa mapato.

Maganya ameyasema hayo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wakati akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo wanaccm na uongozi wa Halmashauri wakati wa ziara yake Mkoani Pwani.

Amesema kuwa Halmashauri hiyo imeonyesha jinsi gani inavyopambana katika ukusanyaji wa mapato ambayo yanasaidia katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

"Tunaipongeza Halmashauri kwa jitihada zake za ukusanyaji wa mapato na kuifanya kuwa moja ya Halmashauri zinazofanya vizuri nchini kwenye siala la ukusanyaji wa mapato,"amesema Maganya.

Aidha ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuvipatia mikopo ya asilimia 10 vikundi vya wajasiriamali kwa ajili ya kuendesha shughuli zao.

"Kama mmeweza kutoa mikopo na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukopa fedha hizo mnafanya jambo zuri ndivyo serikali inavyotaka wananchi wakopeshwe ili wafanye shughuli zao za kiuchumi,"amesema Maganya.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa mwaka 2024/2025 walitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 kwa vikundi 400 vyenye watu zaidi ya 3,000.

Shemwelekwa amesema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya vikundi kutokuwa na sifa za kukopa lakini fedha zipo kwa vile vinavyokidhi vigezo vinakopeshwa.

Alisema kuwa baada ya mikopo kurejeshwa kulikuwa na madeni yaliyofikia kiasi cha shilingi bilioni 1.2 lakini wamefanya jitihada ya kufanikisha kurejesha na madeni yaliyobakia ni milioni 300.

Tuesday, July 21, 2026

WANANCHI WAJITOLEA KUFUFUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.

MASAUNI AWATAKA WANANCHI KUTUMIA FURSA YA HEWA UKAA




Na Mwandishi Wetu, Rufiji

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Hamad Masauni amewataka wananchi kutumia miradi ya utunzaji wa mazingira ili kupata hewa ukaa na kujiongezea kipato.

Masauni aliyasema hayo Wilayani Rufiji alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa ziara yake Mkoani Pwani kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuwa hewa ukaaa ni jambo kubwa la kiuchumi hivyo wananchi watumie kila fursa inayogusa hewa ukaa watumie rasilimali vizuri kupitia misitu. 

"Rufiji ina fursa nyingi za uzalishaji hewa ukaa kupitia, misitu migomba mikorosho kwani hii ni biashara nzuri watumieni wataalam ili wawape moingozo ili kuongeza kipato kwa kutumia fursa hii,"alisema Masauni.

Aidha alisema kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni chanzo cha biashara kupitia mkataba wa Paris baada ya kukubaliana nchi zenye rasilimali za kupunguza hewa ukaa zilipwe.

"Kupitia kilimo madini na faida ya kuhifadhi miti tutalipwa hiyo ni changamoto muifanyie kazi kwani mna rasilimali za kutosha za kuwa miradi ya hewa ukaa,"alisema Masauni

Aliongeza kuwa Watanzania wanapaswa kutunza amani iliyopo na kuachana na yale yanayoweza kuharibu amani ya nchi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

"Kipindi cha nyuma kulitokea changamoto hata wanaccm walikuwa hawavai sare za chama lakini sasa watu wana amani hivyo tunzeni amani kwani  umuhimu wa amani unajulikana na vijana wanasababu ya kuenzi umoja na kurithisha watoto wetu na Muungano ndiyo kiungo cha amani kupitia  waasisi wa taifa letu wametuachia msingi wa amani,"alisema Masauni.

Aliipongeza Wilaya ya Rufiji kwa kutekeleza kikamilifu kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye miradi mbali mbali ya maendeleo ya elimu afya miundombinu kilimo maji.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao alisema kuwa Wilaya hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo ukilinganisha na zamani kupitia uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mlao alisema kuwa kwa ujumla Mkoa umepiga hatua kubwa ya maendeleo hivyo watu wanapaswa kuona jinsi gani maendeleo yaliyopatikana chini ya CCM.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge 
alisema kuwa mwaka wa fedha Mkoa ulipangiwa kukusanya bilioni 88 lakini hadi Juni 30 mwaka huu tayari zimekusanywa bilioni 135 na kuwa mkoa wa pili baada ya Dar es Salaam. 

Kunenge alisema kuwa Mkoa unajivunia Rais kwa kuwatumikia Watanzania na Rufiji ina miradi mikubwa ya uwekezaji na moja mradi alionyesha Urusi ni kilimo cha ndizi kupitia moja ya kampuni kubwa afrika.

Alisema kuwa kwa sasa kuna mifugo mingi na kuna ranchi ndogo na uchumi usitegemee chanzo kimoja ili kuwa salama kwa kutumia bahari na utalii kwani huwezi kushindana na mabadiliko ya dunia ni kijini na dira 2050 inataka kuwa na ajira milioni nane pato la Taifa trilioni moja pato la mwnanchi milioni 18 kwa mwaka.

Akikaribisha ugeni wa Waziri Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Fredrick Komba alisema kuwa Wilaya hiyo imefanikiwa kupanda miti ya mikorosho ipatayo milioni 1.5.

POLISI KATA MAILIMOJA AMTEMBELEA MZEE NA KUTOA MSAADA.





Na Mwandishi Wetu, Kibaha

Polisi Kata wa Mailimoja, Mkaguzi wa Polisi, Tupilike Mwabulambo ameambatana na Stesheni Sajenti Lusekelo Mwakalinga wa Wilaya ya Kibaha kumtembelea mzee Hamisi Nampatima wa mtaa wa Uyaoni ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuwafikia wahitaji waliopo kwenye kata yake na kutoa msaada.

Akikabidhi baadhi ya mahitaji kwa mzee huyo Julai 20, 2026 INSP Tupilike alieleza kuwa kuna makundi mbalimbali katika jamii ambao wana changamoto ikiwemo za kiusalama na mahitaji muhimu hivyo anatembelea kaya hizo kuwasikiliza na kutoa kile alichojaliwa kwa wakati huo.

Kwa upande wake Mzee Hamis Nampatima, alilishukuru Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa msaada wanaompatia kwani sio mara ya kwanza kufika kwake, Mara kadhaa Sajenti wa Polisi Salum Ally wa Polisi Wilaya ya Kibaha amekua akimsaidia kwa kumpatia pesa na mahitaji mbalimbali ya nyumbani.

Naye, Mwenyekiti wa Mtaa wa Uyaoni, Katani humo, Bw. Fadhili Kindamba alipongeza Jeshi la Polisi kwa namna wanavyoshirikiana na wananchi kuimarisha ulinzi na usalama na kutatua changamoto zao zingine za kijamii.

Sunday, July 19, 2026

WANANCHI MTAA WA MACHINJIONI WAJITOLEA KUFUNGUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.

Friday, July 17, 2026

NSSF YAWATAKA WAAJIRI KUTUMIA MSAMAHA WA TOZO

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetangaza nafuu kwa waajiri wenye malimbikizo ya michango kwa kuwapatia fursa ya msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango, huku ukiwataka kuchangamkia fursa hiyo ili kupunguza mzigo wa madeni, kuimarisha uzingatiaji wa sheria na kulinda haki za wafanyakazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema kuwa msamaha huo, ulioanza kutekelezwa tarehe 1 Juni 2026, utaendelea hadi 31 Desemba 2026. 

Bw. Mshomba alieleza kuwa tangu kuanza kwa msamaha huo, waajiri wameonyesha mwitikio chanya ambapo hadi sasa zaidi ya waajiri 6,000 wamejitokeza kutumia fursa hiyo na Mfuko umekwishakusanya zaidi ya shilingi bilioni 46 za michango tangu kuanza kwa msamaha huo tarehe 1 Juni 2026.

“Tunawasihi waajiri wote kutumia fursa hii mapema. Fedha ambazo wangezilipa kama tozo wanaweza kuzielekeza katika shughuli za uzalishaji, upanuzi wa biashara, kuongeza tija na kuboresha ustawi wa wafanyakazi,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema msamaha huo utaendelea hadi tarehe 31 Desemba 2026, ambapo waajiri watakaolipa malimbikizo yote ya michango ya msingi ifikapo tarehe 31 Agosti 2026 watanufaika na msamaha wa asilimia 100 ya tozo.

Alifafanua kuwa waajiri watakaokamilisha malipo yao kati ya Septemba na Oktoba 2026, watanufaika na msamaha wa asilimia 75, huku wale watakaolipa kati ya Novemba na Desemba 2026 wakipata msamaha wa asilimia 50.

Aidha, alisema waajiri ambao hawakuwa na malimbikizo ya michango hadi tarehe 31 Mei 2026 lakini walikuwa na tozo pekee, watanufaika na msamaha wa asilimia 100 endapo wataendelea kuwasilisha michango yao kwa wakati hadi mwezi Desemba 2026.

Bw. Mshomba alisema fursa hiyo imetolewa ili kuwapa waajiri nafasi ya kurekebisha hali ya ulipaji wa michango na kutumia fedha ambazo zingelipwa kama tozo katika shughuli za uzalishaji, kuongeza tija na kuboresha mazingira ya kazi.

“Fedha ambazo waajiri wamekuwa wakizilipa kwa ajili ya kufidia tozo zinaweza kuelekezwa katika kuboresha maeneo yao ya kazi, kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji.

Ndiyo maana fursa hii imetolewa ili waajiri wanufaike,” alisema.
Alisema ulipaji wa michango kwa wakati ni muhimu kwa kuwa unamwezesha mfanyakazi kupata haki zake za hifadhi ya jamii wakati anapopata majanga mbalimbali ikiwemo kustaafu.

NSSF YAENDELEA KUIMARIKA
Katika hatua nyingine, Bw. Mshomba alisema NSSF imeendelea kuimarika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, ambapo thamani ya Mfuko imeongezeka kutoka shilingi trilioni 4.8 mwezi Machi 2021 hadi kufikia zaidi ya shilingi trilioni 11.6 Juni 2026.

Alisema ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la wanachama na michango, uwekezaji wenye tija, mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma.

Alieleza kuwa kupitia mifumo ya TEHAMA, waajiri na wanachama sasa wanaweza kufuatilia na kuwasilisha michango, kufuatilia madai ya mafao na kupata huduma mbalimbali bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Kuhusu ulipaji wa mafao, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuboresha mifumo yake ambapo kwa sasa mafao mengi hulipwa ndani ya siku 20, tofauti na siku 60 zinazotakiwa kisheria.

“Lengo letu ni kuhakikisha mwanachama anapata stahiki zake kwa wakati. Endapo kuna ucheleweshaji mara nyingi chanzo huwa ni mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati,” alisema.

UWEKEZAJI WENYE TIJA, SKIMU YA HIFADHI KUONGEZA WANUFAIKA
Akizungumzia uwekezaji, alisema NSSF inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati inayochangia ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira, akitolea mfano Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kimeendelea kuongeza uzalishaji, kutoa ajira na kuwawezesha wakulima wanaokizunguka.

Kuhusu Skimu ya Hifadhi, Bw. Mshomba alisema mpango huo umewezesha wananchi waliojiajiri kujiunga na mfumo wa hifadhi ya jamii na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi pamoja na huduma za matibabu.

“Tunawahimiza waliojiajiri kujiunga kupitia Skimu ya Hifadhi kwa sababu mpango huu unabadilisha maisha yao na kuwapa uhakika wa kunufaika na mafao mbalimbali. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa Staa wa Mchezo katika kujilinda dhidi ya changamoto za maisha,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema NSSF itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha mfumo wa hifadhi ya jamii nchini na kuhakikisha unaleta manufaa kwa Watanzania wengi zaidi.

Wednesday, July 8, 2026

DKT. NICAS MAWAZO AKUTANA NA BALOZI KAIRUKI NCHINI UINGEREZA, WAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI KIBAHA

London, Uingereza | Julai 8, 2026
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Nicas Mawazo ambaye yupo nchini Uingereza katika ziara nchini humo, leo Julai 8, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Balozi Kairuki.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Kairuki amepongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha diplomasia ya uchumi, kuvutia uwekezaji na kusukuma mbele agenda ya maendeleo ya taifa.

Aidha, Balozi Kairuki ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa mafanikio yake katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo na ukusanyaji wa mapato ya ndani, akieleza kuwa halmashauri hiyo imeendelea kuwa miongoni mwa halmashauri zinazofanya vizuri nchini.

Mazungumzo kati ya viongozi hao yamejikita katika kutafuta fursa za ushirikiano wa kiuchumi kwa Manispaa ya Kibaha, ikiwemo namna ya kuvutia wahisani, wawekezaji na wadau wa maendeleo kutoka Uingereza ili kuwekeza katika sekta mbalimbali zenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya manispaa hiyo.

Dkt. Mawazo amesema kuwa mazungumzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuitangaza Manispaa ya Kibaha kimataifa na kufungua milango ya ushirikiano itakayochochea uwekezaji, ukuaji wa uchumi na uboreshaji wa huduma kwa wananchi.

Friday, July 3, 2026

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA MICHEZO KWA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.



Mpya







MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

Thursday, July 2, 2026

PWANI KUMUUNGA MKONO RAIS DK SAMIA UKUSANYAJI MAPATO

MKOA wa Pwani umesema utashirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha inakusanya mapato ili kuinua uchumi kupitia uwekezaji wa viwanda kumuunga Mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Hayo yelisemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Pili Mnyema wakati wa sherehe za kutimiza miaka 30 ya TRA kimkoa ambapo walushuhudia moja kwa moja maadhimisho hayo Kitaifa ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Dk Samia.

Mnyema alisema kuwa kama Rais alivyotaka TRA kufanya vizuri ili akistaafu Mamlaka hiyo iwe kwenye hali nzuri ndiyo itakuwa furaha yake.

"Tutamuunga mkono Rais kwa kushirikiana na TRA kuhakikisha walipa kodi wanalipa kodi pasipo kukwepa kodi ili kuinua uchumi hasa ikizingatiwa Pwani ni mkoa wa kimkakati kwa kuwa na viwanda vingi,"alisema Mnyema.

Alisema kuwa ukusanyaji mzuri unaofanyika unatokana ushirikiano uliopo baina ya mamlaka na walipa kodi ambapo hicho ni kiashiria cha ukuaji wa uchumi.

"Pia ukusanyaji utaendana na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050 ambayo ndo inaanza kazi kuanzia sasa na hapa tunashirikiana na sekta binafsi katika kuchangia uchumi,"alisema Mnyema.

Aidha alisema kuwa Mkoa utasimamia kuhakikisha malengo ya nchi yanatimia kwa kuwa na uwezo wa kukusanya mapato kwa walipa kodi kulipa kwa hiyari ikiwa ni maono ya Rais.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Salim Makame alisema kuwa Mamlaka imejipanga kuhakikisha wale wote wanastahiki kulipa wanalipa kwa hiyari.

Makame alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na Rais ya namna ya kuboresha ukusanyaji wa Mapato pia kutumia mifumo ya teknolojia.

Wednesday, July 1, 2026

NASHUKURU SANA MTANDAO NAJUKWAA KUBWA BELLE NAIJA

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 

Jukwaa kubwa la kidijitali nchini Nigeria linalojihusisha na masuala ya burudani, mitindo, mitindo ya maisha (lifestyle), na harusi za Kiafrika. Ilianzishwa mnamo mwezi Julai mwaka 2006 na mjasiriamali wa Nigeria anayeitwa Uche Pedro (jina la kuzaliwa Uche Eze).

NASHUKURU KUPOSTI PICHA YANGU NA STAA MKUBWA NCHINI NIGERIA NI HESHIMA KUBWA KUTAMBUA MCHANGO WANGU KATIKA AFRIKA 

Layi Wasabi (jina lake halisi ni Isaac Ayomide Olayiwola) ni mchekeshaji, mwigizaji, na mtengeneza maudhui maarufu wa mtandaoni kutoka nchini Nigeria. 

Anajulikana sana kwa uchekeshaji wake wa kipekee na wa akili (philo-comedy) kupitia video fupi (skits) kwenye mitandao ya kijamii