Thursday, May 7, 2026

RAIS SAMIA ANAENDELEA KUPELEKA FURAHA NA NEEMA KWA WATUMISHI WA UMMA TANZANIA.-KIKWETE


Nimezungumza na maafisa tawala na RasilimaliWatu , katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa AICC, Arusha na kuwakumbusha kutekeleza wajibu wao na kuleta furaha kwa watumishi wa umma ili kwa upande mwengine nao wapeleke furaha na neema kwa Watanzania . 

Nimeyaeleza hayo kufuatia maamuzi mbalimbali yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha maslahi ya Watumishi wa umma nchini yanaboreka. 

Uamuzi wa hivi karibuni wa Serikali kupandisha madaraja watumishi 219,042 ni hatua ya kihistoria katika kuimarisha utumishi wa umma nchini Tanzania. 

Hatua hii ambayo imepata ridhaa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na ongezeko la mishahara ya watumishi wa umma (2025): +35.1% , Ongezeko la kima cha chini sekta binafsi (2025/26): +33.4% 

Aidha Sekta mbalimbali zinakwenda athiriwa na maboresho haya ikiwemo afya, elimu, kilimo, mawasiliano, usafirishaji, nishati, viwanda, biashara, hoteli, michezo, uvuvi, baharini, madini ,utamaduni n.k 


Matokeo haya kitakwimu zinaonyesha kasi ya mageuzi ya kiutumishi chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ambayo inaonyesha uongozi wa kimkakati unaoweka mbele ustawi wa watumishi na ufanisi wa taasisi za umma.

Tuesday, May 5, 2026

VIJANA WATAKA MFUMO UKOPAJI UBORESHWE KUVUTIA VIJANA

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kibaha Mjini umeishauri Wizara ya Maendeleo ya Vijana kuangalia upya mfumo wanamna ya kuwapata vijana kukopa ili wengi waweze kunufaika.

Akizungumza ofisini kwake Katibu wa (UVCCM) Kata ya Tangini Lazaro Benjamin alisema kuwa Wizara inapaswa kuweka mfumo rafiki na kuweka masharti nafuu.

Benjamin alisema kuwa kuweka masharti magumu kunakwamisha vijana wengi kupata fursa ya kufikia mikopo hiyo inayowalenga vijana.

"Vijana ndio nguvu kazi ya Taifa wanapokosa mitaji wanakosa fursa ya kujiajiri na matokeo yake ni kuongezeka kwa ukosefu wa ajira umasikini na hata kukata tamaa,"alisema Benjamin.

Alisema kuwa kuna umuhimu sasa wa kuongeza bajeti ya mikopo ya vijana ili iwafikie wengi zaidi pia kutoa elimu ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha ili mikopo itumike kwa ufanisi.

"Lengo liwe ni kuwafikia vijana wengi zaidi iwezekanavyo kwani maendeleo ya Taifa letu yanategemea uwezeshaji wa vijana wake na wafanye maboresho ili kuhakikisha uwiano unazingatiwa,"alisema Benjamin.

Aidha alisema kuwa wanamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutenga kiasi cha shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuwawezesha vijana kiuchumi kwani hiyo ni hatua kubwa na ya kupongezwa na inaonesha dhamira ya kweli ya serikali katika kuinua vijana wa Taifa la Tanzania.

"Wizara ifanye utafiti kwani takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya vijana 30,384 waliomba mikopo hii lakini vijana waliokidhi vigezo vya kukopeshwa ni 1,961tu,"alisema Benjamin.

Aliongeza kuwa idadi kubwa sana ya vijana zaidi ya asilimia 90 hawakupata fursa hiyo utafiti ufanyike ili kujua ni kwa nini idadi hiyo kutokidhi vigezo na kama bajeti ni ndogo basi iongezwe ili asilimia ya vijana wanaoomba mikopo waweze kuongezeka na kupanua wigo wa ajira kwani wakipata watajiajiri.

Sunday, April 26, 2026

Shule

 


INTRNATIONAL

 


SHULE KIMATAIFA

 


ZINGATIENI DIRA YA MAENDELEO

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini

SHULE ZA KIMATAIFA ZATAKIWA KUJISAJILI KIKIDHI MATAKWA YA KISHERIA

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini


Thursday, April 23, 2026

MITAALA YA SHULE ZA KIMATAIFA YAVUTIA WANAFUNZI KUTOKIMBILIA KUSOMA NJE YA NCHI


KWA kipindi cha miaka ya nyuma baadhi ya wazazi walikuwa na kasumba ya kupeleka watoto wao kusoma nje ya nchi kwa imani huko ndiko kuna elimu bora tofauti na hapa nchini.

Aidha baada ya maboresho mbalimbali kwenye shule za kimataifa hapa nchini kwa sasa wazazi wanawapeleka watoto wao kwenye shule za hapa nchini ambazo zinatoa elimu bora.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Elimu ya Ualimu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Mathias Mvula akimwakilisha Naibu Waziri wa Elimu Wanu Ameir wakati akifungua mafunzo ya wadau wa Shule za Kimataifa nchini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kibaha.

Mvula amesema kuwa Shule hizo zinafundisha kwa kuzingatia mitaala ya nchi na ile ya kimataifa ili elimu inayotolewa kuwa na ushindani na ile inayotolewa nje.

Naye Hassan Masawe kutoka Tanzania School Leadership Institute (TSLI) amesema kuwa mafunzo hayo yana lengo la kuboresha elimu inayotolewa na shule hizo kuwa na ubora baina ya elimu ya nchini na ile ya nje ya nchi.

Kwa upande wake Calista Mungwe Mkurugenzi wa shule ya Renie International ya Jijini Dar es Salaam amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha uendeshaji wa Shule zao.


Wednesday, April 22, 2026

VIJANA WASEMA BENKI YA VIJANA ITAKUZA MITAJI YAO YA BIASHARA


MPANGO wa kuanzisha benki ya vijana ni jambo zuri kwani watanufaika na kuweza kukuza mitaji na biashara zao hivyo wataweza kujiajiri na kuajiriwa kwa wingi.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Tangini Lazaro Benjamin Wilayani Kibaha Mkoani Pwani akizungumzia kuhusu bajeti ya vijana iliyowasilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Dk Joel Nanauka Jijini Dodoma.

Benjamin amesema kuwa benki hiyo itatoa mikopo rahisi na yenye masharti nafuu ikiambatana na riba ndogo pamoja na dhamana rahisi.

"Benki hiyo itaenda kuondoa changamoto za mitaji kwa vijana na itasaidia kuongeza nafasi ya kufadhiliwa,"amesema Benjamin.

Aidha amesema kuwa benki hiyo itasaidia kuwapatia vijana elimu ya biashara na uwekezaji na matumizi sahihi ya fedha.

"Itapunguza vijana kutokuwa na ajira kwani watajiajiri kupitia mikopo ambayo itawapatia mitaji na kupata elimu ya matumizi ya fedha,"amesema Benjamin.

Saturday, April 18, 2026

MWENGE KUPITIA MIRADI YA MAENDELEO 68 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 263.1

MWENGE wa Uhuru umeanza mbio zake Mkoani Pwani ambapo utapitia miradi ya Maendeleo 68 yenye thamani ya shilingi bilion 263.1 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge aliyasema hayo Mapinga Wilayani Bagamoyo wakati akiupokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila.

Kunenge alisema kuwa kati ya hiyo miradi 23 itawekewa mawe ya Msingi miradi 21
itazinduliwa na miradi 24 itakaguliwa.

"Miradi hiyo imechangiwa na Serikali Kuu bilioni 16.2 Halmashauri za Wilaya zimechangia kiasi cha shilingi bilioni 1.62,"alisema Kunenge.

Alisema kuwa wananchi na wawekezaji wamechangia kiasi cha shilingi bilioni 180.7 wadau wa Maendeleo bilioni 64.3 na michango ya Mwenge milioni 38.8.

"Ujumbe Mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 unalenga katika ujenzi wa Amani Umoja na Mshikamano wa Kitaifa chini ya Tanzania ni yetu sote tushikamane pamoja kuleta maendeleo,"alisema Kunenge.

Alisema kuwa kauli mbiu hiyo inalenga kujenga na kuimarisha Umoja wa Kitaifa na kuutumia Mwenge wa Uhuru kuwaenzi na kuwatia moyo wazalendo wa kweli na makundi mbalimbali.

"Makundi haya yana mchango mkubwa katika kulinda Amani, Umoja na Mshikamano wa Kitaifa katika kuijenga Tanzania imara kimaadili, kidiplomasia na kiuchumi ndani na nje ya mipaka,"alisema Kunenge.

Aidha alisema Mkoa unachukua hatua kupitia ujumbe wa kudumu katika mapambano dhidi ya Vvu/Ukimwi, dawa za kulevya, malaria, rushwa na changamoto za lishe.

Naye kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Wazo Mwangonda alisema kuwa taarifa zinazoonyesha namna wanawake na makundi maalumu namna gani wanavyonufaika na zabuni.

Mwangonda kuwa Mwenge ni wawananchi yapangwe maeneo ambayo wananchi wataukimbiza.

Saturday, April 4, 2026

MKIMBIZA MWENGE KITAIFA AIPONGEZA STAMICO KWA KUIBEBA AGENDA YA KITAIFA YA NISHATI SAFI


*STAMICO YASHIRIKI UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU KITAIFA PEMBA.* 

▪️Mkimbiza Mwenge Kitaifa aipongeza STAMICO kwa kuibeba ajenda ya kitaifa ya Nishati Safi.

▪️Atoa msisitizo kwa Taasisi na Shule Mkoani Kusini Pemba kutumia Nishati ya Rafiki Briquettes 

▪️Nishati Safi ya Rafiki Briquettes  kuanza kuuzwa Kisiwani Pemba

▪️Dkt. Mwasse: STAMICO kuwawezesha kontena wanawake na Samia Mkoa wa Kusini Pemba 

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeshiriki katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge ambazo umefanyika katika viwanja vya Gombani Kisiwani Pemba.

Mgeni Rasmi katika Uzinduzi huo alikuwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tukio hilo pia lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

STAMICO imewakilishwa na Dkt Venance Mwasse, Mkurugenzi  Mtendaji ambaye aliambatana na baadhi ya maafisa kutoka kitengo cha Masoko na Mahusiano.

Katika mbio za mwaka huu za Mwenge wa Uhuru, kauli mbiu ni: “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Maendeleo.” Kauli mbiu hiyo inalenga kuhamasisha umoja, ushirikiano na mshikamano wa Watanzania katika kuchangia maendeleo ya Taifa. Mbio hizi zinatarajiwa kuendelea katika mikoa mbalimbali ya nchi, Tanzania Bara na Visiwani.

Sambamba na uzinduzi huo, pia kumefanyika maonesho ya Taasisi mbalimbali za Serikali na sekta binafsi yaliyolenga kutoa elimu na kuonesha huduma mbalimbali kwa wananchi.

 Katika maonesho hayo, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) nalo limeshiriki kwa kuonesha bidhaa na huduma zake kwa Wananchi.

Awali, Mwenyekiti wa Kikundi cha Wanawake na Samia Mkoani Kusini Pemba Bi Sabra Masoud Ally alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO  kwa ulezi na ushirikiano unaotolewa na STAMICO katika kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na usambazaji wa nishati safi ya Rafiki briquettes.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Mwasse aliahidi kuendelea kusaidia kikundi hicho kwa kuwapatia kontena  mwezi huu wa nne, ili yaweze kutumika kama vituo vya kuuzia nishati safi ya kupikia ya Rafiki Briquettes. Aidha, alisisitiza kuwa STAMICO itaendelea kufanya uhamasishaji mkubwa wa matumizi ya nishati hii safi katika mikoa ya Kaskazini na Kusini  Pemba, kwa lengo la kulinda mazingira na kupunguza matumizi ya kuni na mkaa wa kawaida.

Akitembelea banda la STAMICO,Mkimbiza Mwenge kitaifa,Ndugu Wazo Mwangonda aliipongeza STAMICO kwa kubeba kikamilifu ajenda ya Kitaifa ya nishati safi na Kusisitiza taasisi na Shule za Mkoa wa Kusini Pemba kutumia Nishati ya Rafiki Briquettes.

STAMICO  inaendelea na azma yake ya kuwa kinara katika kuhamasisha matumizi  ya Nishati Safi kwa kutekeleza kwa vitendo ajenda muhimu za Serikali.

Thursday, April 2, 2026

CCM PWANI YAISHUKURU SERIKALI YA DK SAMIA SULUHU HASSAN FEDHA MIRADI YA MAENDELEO

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani umeishukuru serikali inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuuongezea Mkoa bajeti ya fedha za miradi ya maendeleo na kufikia kiasi cha shilingi bilioni 497.1 mwaka 2026/2027.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Katibu wa Siasa Uenezi na Mafunzo wa CCM Mkoa wa Pwani Dk David Mramba alisema kuwa hiyo inaonyesha jinsi gani serikali inavyojali maendeleo ya wananchi.

Alisema kuwa fedha hizo zimeongezeka kutoka kiasi cha shilingi bilioni 473 bajeti ya mwaka 2025/2026 hivyo kufanya Mkoa kupiga mbele hatua za maendeleo.

"Fedha hizi zinakwenda kukabili changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wananchi kwenye huduma muhimu za kijamii ambapo zinatoa majawabu,"alisema Mramba.

Alisema kuwa baadhi ya miradi ikiwemo huduma za maji zimeboreshwa ambapo wananchi wanapata maji safi na salama ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

"Kwa upande wa elimu madarasa mengi yamejengwa, maabara za kutosha ili kuinua masomo ya sayansi, ujenzi wa vyoo, mabweni, nyumba za walimu na madawati,"alisema Mramba.

Aidha alisema kuwa kwa upande wa huduma za afya nazo zimeboreshwa kwani Hospitali za Rufaa, Hospitali, Zahanati na huduma za kibingwa zinatolewa hapa hapa nchini badala ya kwenda nje ya nchi.

"Kuhusu miundombinu barabara nyingi zimejengwa na kurahisisha shughuli za kiuchumi huku mazao na bidhaa zikisafirishwa kwa urahisi ambapo mikoa na wilaya zinaingiliana kwa urahisi,"alisema Mramba.

Aliongeza kuwa kuna baadhi ya changamoto ambazo zinafanyiwa kazi kwa kuendelea kutengewa bajeti ili kuhakikisha huduma za msingi kwa wananchi zinapatikana kwa urahisi.

Sunday, March 29, 2026

KITUO CHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MANISPAA YA KIBAHA KUJENGA KIWANDA CHA KUTENGENEZEA BATIKI

NGUO za Batiki zimekifanya Kituo cha Wanawake Wajasiriamali Manispaa ya Kibaha kuitangaza Tanzania kwenye soko la Kimataifa ambapo ziliongoza kwa kununuliwa kwenye maonyesho nchi jirani. 

Akizungumza ofisini kwake Mjini Kibaha Mwenyekiti wa Kituo hicho Dk Magdalena Mangi alisema kuwa walishirki maonyesho kwenye nchi za Sudan, Kenya na Burundi miaka ya hivi karibuni ambapo zilinunuliwa kwa wingi.

Mangi alisema kufuatia batiki zao kuwa na soko kubwa wamejipanga kuanzisha kiwanda cha utengenezaji wa batiki ili kuongeza ubora wa bidhaa hiyo ili kuendelea kuitangaza nchi wanapokwenda kwenye maonyesho kama hayo siku za baadaye kwani wamedhamiria kuzalisha bidhaa zenye ubora.

Mangi alisema kuwa kwa sasa wanazalisha batiki kwa kutumia mikono hali inayofanya ubora kupungua lakini wanaamini wakitumia mashine wataongeza ubora.

"Batiki tunazozalisha ni nzuri kwani tunatumia vitamba vizito ambavyo havichuji tofauti na wazalishaji wengine hali ambayo inatufanya tupate soko maeneo mbalimbali ambapo ushiriki kwenye nchi Burundi mwaka 2023, Sudan Kusini 2024, na Kenya 2025  tulipata mafanikio makubwa,"alisema Mangi.

Alisema kuwa wamekuwa wakipata masoko maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na watu binafsi na taasisi zikiwemo za watu binafsi na za serikali.

"Tuna soko japo siyo kubwa sana lakini tunataka tujitanue kwa kujitangaza kwa kutumia vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii ili kuwafikia wateja wengi,"alisema Mangi.

Aidha alisema kuwa changamoto inayowakabili ni mtaji ambapo wakipata fedha watahakikisha wanajenga kiwanda ili kuongeza ubora wa batiki zao.

"Tulikopa Halmashauri kiasi cha shilingi milioni 40 ambapo bado tunaendelea na marejesho na tunahitaji sehemu ya kutengenezea batiki kwani hapa eneo ni dogo hali inayofanya tutengenezee nyumbani,"alisema Mangi.

Aliongeza kuwa wanaishukuru serikali kwa kuendelea kuwawezesha ili waweze kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri na kuwawezesha hata kwa mikopo ya asilimia 10 ili kukuza biashara zao.

Naye Simon Kiondo mkufunzi wa masuala ya fedha na ujasiriamali alisema kuwa alikipatia elimu ya biashara mtandaoni ili kupata masoko zaidi kwani hiyo ni moja ya njia za kuongeza wateja.

Kiondo alisema kuwa baadhi ya changamoto ya vikundi vya ujasiriamali ni kukosa mipango na malengo na utunzaji wa kumbukumbu na ukosefu wa elimu ya fedha.

Alisema kuwa wajasiriamali wanapaswa kujitangaza na kwenda na wakati kwa kutumia teknolojia ya kisasa kupitia mitandao ya kijamii kuvutia masoko.

Kituo hicho kina jumla ya wanachama 10 na kinajohusisha na uzalishaji wa batiki, sabuni, mafuta mbalimbali, urembo, ushonaji nguo na khanga.

Thursday, March 26, 2026

PROGRAM YA MALEZI MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO YAPATA MAFANIKIO






PROGRAM ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto imeleta manufaa makubwa kwa kuanzishwa kadi ya alama kwa watoto inayorahisisha ufuatiliaji.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Shirika lisilo kuwa la Kiserikali la Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha wadau wa Program hiyo Mkoa wa Pwani.

Malela amesema kuwa kuanzishwa kwa kadi hiyo kwa watoto ni mafanikio makubwa ya Program hiyo katika kuhakikisha ustawi wa watoto katika makuzi yake.

Amesema kuwa kikao hicho kiliweza kujadili masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya uchechemuzi wa umuhimu wa kuwekeza kwenye Program hiyo na kusaidia serikali kutekeleza Program za malezi.

"Kuendelea kushirikiana na wadau wa nje katika kuwekeza katika malezi kuhamasisha jamii na serikali katika kuanzisha vituo vya kulea watoto wadogo mchana vya jamii,"amesema Malela.

Msajili wa mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali Elia Kabora amesema kuwa uwekezaji kwa watoto ni moja ya vipaumbele ili kuhakikisha makuzi ya watoto yanazingatia upatikanaji wa huduma muhimu.

Kabora amesema kuwa Programu hiyo inalenga kuimarisha utoaji huduma bora za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali.

Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yasiyo kuwa ya Kiserikali Kibaha Mjini (KITAN) Dk Rose Mkonyi amesema kuwa jamii kwa kushirikiana wadau wengine wanapaswa kuhakikisha watoto wanapata mahitaji muhimu ili waweze kupata huduma muhimu.

Mkonyi amesema kuwa wadau wanapaswa kuungana kufanikisha Program hiyo ili kuweza kufanikisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

Walengwa wa mradi huo walioshiriki kikao hicho ni pamoja na wazazi, walezi, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, viongozi wa dini na wataalam wa ngazi ya serikali.

mwisho.

Sunday, March 22, 2026

UKUWAWAVI WATOA MISAADA KITUO CHA YATIMA BULOMA


UMOJA wa Kusaidiana Wanajeshi Wastaafu wa Vifaru (UKUWAWAVI) wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye Kituo cha Kulea Yatima cha Buloma.
Wametoa misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Iddi el Fitri na Mfungo wa Kwaresma.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi misaada hiyo Mwenyekiti wa (UKUWAWAVI) SSGT Omari Makore amesema kuwa wameguswa kuwasaidia watoto hao ili nao waweze kufurahi kama walivyo watoto wanaoishi na familia zao.

Makore amesema wanajua kuwa watoto hao wana mahitaji mengi lakini wameona
waanze na kidogo walichojaliwa na hiyo ni sadaka na wataendelea kusaidia pale watakapojaliwa wakati mwingine.

"Tutarudi tena kwani watoto hawa wametuonyesha mapenzi makubwa na huu ni mfano na vikundi na watu mbalimbali nao wajitokeze kuwasaidia watoto hawa,"amesema Makore.

Kwa upande wake Mlezi wa (UKUWAWAVI) Brigedia Jenerali Rajabu Hanti (Mstaafu) amesema kuwa watoto hao ni Taifa la kesho wanahitaji malezi ya watu.

Hanti amesema kuwa watoto hao wanapaswa kupelekewa furaha kwa kuwashika mkono kwa misaada mbalimbali ambayo ni mahitaji yao ya msingi.

Naye Mchungaji Jackson Bukelebe amesema kuwa umoja huo umechukua jukumu la kidini kwani dini bora ni ile inayojali yatima watu wanapaswa kujotolea kuwasaidia watoto hao.

Mwasisi wa kituo hicho Anna Kyando amesema kuwa wanashukuru kwa misaada hiyo kwani wadau ndiyo wamekuwa wakiendesha kituo hicho kwani bila wao peke yake asingeweza.

Kyando amesema kuwa changamoto kubwa ni chakula kwani ndicho kinachohitajika muda wote uzio wa ukufa, vifaa vya shule, ada kwa wanafunzi walioko vyuoni kutoka kituo hicho.

Moja ya watoto wa kituo hicho Yohana Almas amesema kuwa wanashukuru kwa misaada hiyo na kuahidi kufanya vizuri kwenye masomo yao na kuomba watu waendelee kuwasaidia.

Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na mchele kilo 100, unga wa sembe kilo 50, maharage kilo 50, mafuta lita 20, madaftari 100, juisi katoni 5, maji katoni 10, doti 5 za khanga, sabuni za unga, taulo za kike na biskuti.

Saturday, March 21, 2026

DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) KUJENGA HOSPITALI YA KISASA.

TAASISI ya DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajia kujenga kituo cha taasisi chenye huduma mbalimbali za kijamii kikiwa ni pamoja Hospitali ya kisasa kwa gharama za shilingi bilioni 5.5.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu wa Taasisi hiyo Karume Amri Abeid amesema kuwa kituo hicho kitajengwa eneo la Boko Wilaya ya Kibaha.

Abeid amesema kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa makao makuu ya Taasisi ambalo lina ukubwa wa hekari 11 na tayari nyumba ya mlinzi tayari imejengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

"Eneo hilo pia kutajengwa ofisi, Msikiti, shule ya awali hadi elimu ya juu yaani kidato cha sita, chuo cha elimu ya dini Ibtidai mpaka Thanawi, kituo cha kuhifadhisha Quran kwa watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea,"amesema Abeid.

Amesema kuwa njia watakayoitumia kupata fedha ni michango mbalimbali toka kwa wadau, waumini na kufanya harambee ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 2.

"Huduma zikiwemo za afya zitatolewa kulingana na jinsi badala ya huduma kutolewa na jinsi tofauti na wanufaika kwenye sekta ya afya na ajira haitajali dini bali ni kwa dini zote kwani lengo ni kutoa huduma bora na za kisasa,"amesema Abeid.

Aidha amesema kuwa matarajio ni kuanza ujenzi Januari mwakani mara fedha zitakapopatikana na kikubwa wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia fedha ili kufanikisha ujenzi huo kwani watu wajitoe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujenga ahera yetu.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya Iddi amesema kuwa siyo kuvaa vizuri na kupendeza bali ni kwa yule mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na kukumbuka siku ya hesabu (Kiyama) ndiyo maana ya Iddi.

Ameongeza kuwa watu wamwabudu Mwenyezi Mungu na kuacha kumkasirisha na waishi maisha haya na si wakati wa mfungo peke yake ili wasimkosee.

DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) KUJENGA HOSPITALI YA KISASA.

TAASISI ya DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajia kujenga kituo cha taasisi chenye huduma mbalimbali za kijamii kikiwa ni pamoja Hospitali ya kisasa kwa gharama za shilingi bilioni 5.5.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu wa Taasisi hiyo Karume Amri Abeid amesema kuwa kituo hicho kitajengwa eneo la Boko Wilaya ya Kibaha.

Abeid amesema kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa makao makuu ya Taasisi ambalo lina ukubwa wa hekari 11 na tayari nyumba ya mlinzi tayari imejengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

"Eneo hilo pia kutajengwa ofisi, Msikiti, shule ya awali hadi elimu ya juu yaani kidato cha sita, chuo cha elimu ya dini Ibtidai mpaka Thanawi, kituo cha kuhifadhisha Quran kwa watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea,"amesema Abeid.

Amesema kuwa njia watakayoitumia kupata fedha ni michango mbalimbali toka kwa wadau, waumini na kufanya harambee ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 2.

"Huduma zikiwemo za afya zitatolewa kulingana na jinsi badala ya huduma kutolewa na jinsi tofauti na wanufaika kwenye sekta ya afya na ajira haitajali dini bali ni kwa dini zote kwani lengo ni kutoa huduma bora na za kisasa,"amesema Abeid.

Aidha amesema kuwa matarajio ni kuanza ujenzi Januari mwakani mara fedha zitakapopatikana na kikubwa wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia fedha ili kufanikisha ujenzi huo kwani watu wajitoe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujenga ahera yetu.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya Iddi amesema kuwa siyo kuvaa vizuri na kupendeza bali ni kwa yule mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na kukumbuka siku ya hesabu (Kiyama) ndiyo maana ya Iddi.

Ameongeza kuwa watu wamwabudu Mwenyezi Mungu na kuacha kumkasirisha na waishi maisha haya na si wakati wa mfungo peke yake ili wasimkosee.

Thursday, March 12, 2026

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

 MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

Wednesday, March 11, 2026

BIDHAA SOKO LA LOLIONDO BEI NZURI

BEI ya Vitunguu kwenye Soko la Loliondo Halmashauri ya Manispaa Kibaha iko juu kutoka shilingi 130,000 hadi 250,000 kwa gunia.

Aidha viazi mbatata ambavyo ni maarufu kwa ajili ya kukaangia chipsi vimeshuka bei kutoka shilingi 140,000 hadi 70,000 kwa gunia.

Akizungumza ofisini kwake Mjini Kibaha Naibu Katibu Mkuu wa soko hilo Alex Msimbe alisema kuwa kwa sasa bidhaa nyingi bei zake hazijapanda sana bali bei iko wastani.

Msimbe alisema kuwa bei hiyo ya vitungu imeongezeka sana kutokana na kipindi hichi ndiyo bei huwa inapanda sana lakini baadaye bei hiyo itashuka.

"Bei ya tenga la nyanya  imeshuka kutoka kati ya shilingi 85,000 na 70,000 hadi 35,000 huku mchele ukiuzwa kati ya shilingi 3,000, 2,500 hadi 2,700 kwa kilo na maharage yakiuzwa kati ya shilingi 2,700 hadi 3,000 kwa kilo.

Alisema kuwa bei ya unga wa sembe ni kati ya shilingi 1,400 na 1,500 kwa kilo na ngano ni shilingi 125,000 kwa kilo 50 huku sukari ikiuzwa shilingi 3,000 kwa kilo.

"Bei za bidhaa nyingi bei hazijapanda kwani kipindi hichi ni cha baadhi ya maeneo ni mavuno na mengine ndiyo wamepanda muda siyo mrefu hivyo kutoathiri sana bei,"alisema Msimbe.

Aidha alisema kuwa kwa sasa hakuna changamoto kwenye soko hilo kwani miundombinu ikiwemo ya maji, umeme na huduma muhimu kama za vyoo zote ziko vizuri kwani wanashirikiana vizuri na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ambao ndiyo wanaowasimamia.

"Kuhusu mitaji baadhi ya wafanyabiashara wananufaika na mikopo ya Halmashauri ile ya asilimia 10 na asilimia 7,"alisema Msimbe.