Tuesday, August 6, 2024

TEAC IMELENGA KUSAIDIA MKULIMA NA MFUGAJI.

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma.

Mkuu wa Kanda ya kati ya Tume ya Nguvu za Atom Tanzania ( TEAC ) Machibya Anthony Matulanya amesema kuwa Tume imelenga  kusaidia wakulima na wafugaji kupata mavuno makubwa ambayo yataongeza pato la uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja .

Hayo ameyasema Leo Tarehe 5 Agost 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika Banda la Tume ya Nguvu za Atom Tanzania Katika viwanja vya nanenane Zuguni jijini Dodoma huku akiwasihi wananchi kutembelea Banda ilo Ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuza na kuboresha kilimo na ufugaji.

Adha amesema kuwa Tume inajishughulisha na swala la uhamasishaji wa Matumizi ya Nuclear nchini ambayo inalenga kuhakikisha teknologia ya nuclear inakunza uchumi wa nchi.

"Tume ya nguvu za Atom Tanzania zinajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama  ambapo wanalenga kuhakikisha kwamba teknologia ya Nuclear nchini  inatumika vizuri na inakuza uchumi wa nchi." Amesema Matulanya

Pia meeleza kuwa teknologia ya nuclear imeweza kutumika kuangamiza  wadudu aina ya Mbung'o ambao wanang'ata Mifugo na  kusababusha Hali ya upungufu wa Maziwa kwa ng'ombe pamoja na kukosa nyama iliyo Bora.

"Kwa upande wamifugoTeknologia ya Nuclear imetumika imeangamiza wadudu aina ya Mbung'o , Mb'ung'o ni wadudu atali ambao wanang'ata Mifugo 

Hawa wadudu waking'ata kwa mfano Ng'ombe wanamsababishia Hali ya upungufu wa Maziwa na pia uwezi kupata nyama nzuri" amesema Matulanya.

Mayulanya amesema kuwa zipo mbegu Bora za Mpunga ambazo zinatumika Tanzania bara na nzazibar ambazo zinauwezo Mkubwa wa kuimili ukame na ahitaji maji Mengi katika kuzalisha na unafanya mmea usivunjike .

"Pia kwa upande wa kilimo teknologia ya Nuclear imetumiaka huko nzazibar na bara, mbegu ya mpunga aina ya   super DC  ambayo inatumika Mbegu hizi ambazo zimeboreshwa  uwezo Mkubwa wa kuimili ukame ambayo mbegu hiyo ukiilima aitaji maji Mengi Katika kutoa matunda yake" Amesema Matulanya 

"Baada ya kuboreshwa mbengu hiyo imekuwa na stimilivu na yenye kutoa faida kubwa kwa mkulima pamoja na mmea kustaimili usivunjike na huo mpunga baada ya kuuvuna na kuukoboa unakuwa mtamu" Amesema Matulanya 

Ikumbukwe kuwa  Tume ya Atom Tanzania  inajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama.

No comments:

Post a Comment