
Aidha imetakiwa kuwezesha shule au vituo vya watu binafsi ambavyo vinakuza vipaji vya wanafunzi ili kuja kupata wanamichezo wenye uwezo na kuliletea sifa Taifa.
Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya ushiriki wa Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa hususani ya Olimpiki.
Bayi alisema kuwa ili kuwa na timu bora ambazo zitashindana kwenye mashindano za kimataifa lazima kuwe na vituo ambavyo vitawaandaa vijana mahiri ambapo wataandaliwa.
"Siri ya kufanya vizuri ni kuwa na vituo maalum au shule ambazo zitawachukua vijana hao ambao wanafanya vizuri kwenye mashindano hayo na kuwaandaa kwa muda mrefu ili waweze kufanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali ikiwa ni pamoja na Olimpiki,"alisema Bayi.
Alisema kuwa kuwe na uwekezaji kwenye kambi maalum siyo kwa ajili ya kushiriki mashindano makubwa bali kuwaandaa wale wenye vipaji ambapo kwa sasa hao wanaofanya vizuri haijulikani wanaenda wapi.
"Tuliambiwa kutakuwa na vituo au shule 56 lakini jatujui imeishia wapi kwani kwa sasa michezo inakwenda kisayansi ambapo wenzetu wamewekeza kwa vijana wao wenye vipaji ambap ndiyo wanaleta mafanikio,"alisema Nyambui.
Alibainisha kuwa fedha zinazorudishwa kwa wananchi kupitia uwekezaji zipelekwe kwenye masuala ya michezo ambapo asilimia tano ya michezo ya kubahatisha inapelekwa Baraza la Michezo BMT lakini ni ndogo inapaswa kuongezwa ili ilete matokeo.
"Kuna shule au vituo kama vile Allince, Kipingu, Makongo, Bagamoyo na Filbert Bayi ni sehemu ambazo zinafanya jitihada kuandaa vijana ni vema vikawezeshwa na serikali ili viweze kuandaa vizuri vijana kwani wanawagharamia vijana hao kwani wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha,"alisema Bayi.
Akizungumzia timu iliyoshiriki mashindano ya Olimpiki yaliyomalizika huko Ufaransa alisema wachezaji waliokwenda walikuwa na viwango vizuri lakini ilitokea tu bahati mbaya lakini waliandaliwa vizuri na kushinda au kushindwa ni matokeo tu.
No comments:
Post a Comment