Tuesday, August 13, 2024

TAKUKURU PWANI YAOKOA BILIONI 1.6

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 1.6 kutoka vyanzo mbalimbali vya Halmashauri ya Mji Kibaha.

Hayo yamesemwa na Naibu Kamanda wa Takukuru Mkoa huo Ally Haji wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha juu ya kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu.

Haji amesema kuwa walibaini hayo wakati wa ufuatiliaji wa ukusanyaji wa ushuru wa huduma kama mbalimbali kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili kwa kushindwa kuwajibika.

"Katika ufuatiliaji tuligundua kuwa baadhi ya watumishi wa Halmashauri kwenye kitengo cha ukusanyaji wa mapato watumishi kushindwa kufuata sheria, kanuni, na taratibu za ukusanyaji na kufanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1.6 zilizokuwa zinapotea,"amesema Haji.


No comments:

Post a Comment