BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha limemchaguaHalima Jongo kuwa makamu mwenyekiti baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Shomari Mwinshehe kumaliza muda wake.
Sambamba na uchaguzi huo wa makamu mwenyekiti ambaye alipata kura zote 17 pia kamati mbalimbali nazo zilichaguwa wenye viti wake.
Jongo ameshukuru madiwani wenzake kwa kumchagua kwa kura nyingi na kusema atashirikiana nao pamoja na watumishi wa Halmashauri ili kuleta maendeleo kwa wananchi.
Amesema kuwa ataendeleza yale ambayo aliyoyafanya mtangulizi wake ili Halmashauri iweze kupata mafanikio ambayo itakuwa ni sehemu ya wananchi kujiletea maendeleo.
"Katika ukusanyaji mapato tumefanya vizuri kwenye awamu hii iliyopita kwa kushirikiana na wenzangu, wataalamu na wananchi kuhakikisha tunakuwa na makusanyo makubwa,"amesema Jongo.
Amesema kuwa jambo kubwa ni kupambana kuleta maendeleo kwa wananchi ambao wanawategemea kuwaonyesha njia.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Regina Bieda amesema kuwa anampongeza Makamu mwentekiti aliyepita na anamkaribisha Makamu mpya katika kuendeleza jitihada za maendeleo.
Bieda amesema watashirikiana wote kwa pamoja ili kuwapambania wananchi lengo waweze kupata maendeleo.
No comments:
Post a Comment