Sunday, August 18, 2024

TAKUKURU PWANI KUTOA ELIMU KUELEKEA UCHAGUZI


KATIKA kukabiliana na vitendo vya rushwa kwenye mchakato wa uchaguzí Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imejipanga kuzuia na kupambana na vitendo hivyo kwa kutoa elimu kwa makundi mbalimbali.

Hayo yalisemwa na Naibu Kamanda wa Takukuru mkoani humo Ally Haji wakati akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha wanatarajia kuyafikia makundi yote yanayohusika na masuala ya uchaguzi.

Haji alisema kuwa baadhi ya makundi ni pamoja nan a vyama vya siasa, wasimamizi wa uchaguzi,
waandishi wa habari wananachi na jamii kwa ujumla.

"Kwa kipindi hichi cha mchakato wa uchaguzi tumeshaanza kufanya ufuatiliaji wa vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji utakaofanyika mwaka huu na uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani,"alisema Haji.

Alisema kuwa wanatoa elimu ya madhara ya rushwa ambapo ni kosa kisheria endapo ikitumika
itasababisha kupatikana víongozi ambao siyo wazuri na hawataweza kuongoza wananchi kwa
weledi ambapo kauli mbiu inasema Kuzuia Rushwani Jukumu lako na langu Tutimize wajibu wetu. 

"Malengo ya kutoa elimu kwa makundi hayo ni kujiandaa kufanya uchaguzi usiokuwa na vitendo vya rushwa ili kupata viongozi bora wasiotokana na vitendo vya rushwa kwani ni adui wa haki na watu wote wana wajibu wa kupambana na vitendo hivyo,"alisema Haji.

Aidha alisema kuwa wataendelea kufanya udhibiti wa mapato ya serikali na usimamizi wa rasilimali za umma ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Tunatoa wito kwa wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada za kufichua vitendo vya rushwa na wala rushwa kwa kutoa taarifa sahihi zitakazowezesha kuwachukulia hatua wahusika hasa katika kipindi hichi tunapoelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu,"alisema Haji.

Aliwataka watumishi wa umma na wa sekta binafsi watakeleze majukumu yao kwa kuzingatia sheria,
kanuni na taratibu za kazí zao ili kuzuia vitendo vya rushwa na kuleta tija katika kuhudumia wananchi ili
kuwaonyesha njia kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

mwisho.

No comments:

Post a Comment