Wakizungumza na waandishi wa habari Mtaani hapo Mohamed Lukemo, Mathias John na Felix Swai walisema kuwa kutokana na ubovu huo umesababisha kalavati lililopo kwenye barabara hiyo kuwa hatarini kuvunjika ambapo kipindi cha mvua magari yalikuwa yakishindwa kupita.
Walisema kuwa barabara hiyo ilichongwa miaka sita iliyopita hali ambayo imeiacha barabara hiyo kwenye hali mbaya na kufanya wakazi hao kupata changamoto hasa kipindi cha mvua kutokana na kuwa na mashimo mengi.
"Tunawaomba Tarura waikumbuke barabara yetu kwani imeharibika vibaya sana na kwa wagonjwa ni changamoto kubwa sana hata magari yanayobeba wanafunzi yapita kwa taabu pale kwenye kalavati,"walisema wakazi hao
Aidha walisema magari yanapata ubovu na kwa wale wanaotumia pikipiki hupandishiwa nauli hasa kipindi cha mvua au wakati mwingine wanakataa kabisa kubeba abiria wanaopita barabara hiyo.
Ally Mohamed alisema kuwa wanashirikiana na wananchi ambapo wanajitolea kuikarabati barabara hiyo kwa baadhi ya maeneo korofi ili ipitike.
Mohamed alisema kuwa taarifa juu ya ubovu wa barabara hiyo wamezipeleka sehemu husika lakini utekelezaji ndo imekuwa changamoto ambapo waliambiwa wasubiri bajeti ya mwaka huu.
Naye meneja wa Tarura Wilaya ya Kibaha Mhandisi Samwel Ndoveni alikiri kuwa barabara hiyo ina changamoto lakini iko kwenye mpango wa kuchongwa.
Ndoveni alisema kuwa tayari wameshapeleka wataalamu kufanya tathmini na wiki ijayo watachonga barabara pamoja na kukarabati sehemu ya kalavati hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi.
No comments:
Post a Comment