Tuesday, August 27, 2024

HALMASHAURI KIBAHA YATAKA MBWA WACHANJWE


HALMASHAURI ya Wilaya ya Kibaha imeagiza kuuwawa mbwa wote wanaozurura ambao wamekuwa wakingata watu na kuwaletea madhara.

Aidha imetaka kufanyika sensa ya wanyama hao ili idadi yake iweze kutambulika kwa wale wanaowafuga kwa utaratibu unaotambulika rasmi na kisheria.

Akitoa azimio hilo kwenye kikao cha Baraza la Madiwani kwa kipindi cha robo ya Aprili hadi Juni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Erasto Makala alisema kuwa mbwa hao wamekuwa kero kwa watu.

Makala alisema kuwa mbwa hao wanaozurura hawana chanjo na wamekuwa wakingata watu hivyo kuhatarisha afya zao.

"Madhara ya mtu kungatwa na mbwa ni makubwa hivyo lazima kuwamaliza mbwa wanaozurura ambao hawana mwenyewe kwani hawana chanjo ya kuwakinga na magonjwa,"alisema Makala.

Alisema kuwa sensa ni muhimu kwa wanayama hao na Halmashauri ikiona kuna changamoto kuna haja ya kumpa mzabuni kwa ajili ya kuchanja mbwa ili kuwafikia mbwa wengi.

Akiibua hoja kuhusiana na mbwa wengi kutochanjwa Diwani wa Viti Maalum ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Halima Jongo alisema mbwa hawajachanjwa ni wengi ukilinganisha na mbwa waliopo.

Jongo alitoa mfano wa Kata ya Ruvu kuna mbwa 361 lakini waliochanjwa ni 35 na Mtambani kuna mbwa 53 lakini hawajachanjwa ambapo Kata za Kwala na Magindu hakuna taarifa ya kuchanjwa mbwa.

Naye Diwani wa Kata ya Kilangalanga Mwajuma Denge alisema kuwa mbwa wasio na wamiliki ambao huzurura ndiyo wanaoleta madhara.

Mwajuma alisema kuwa ikifanyika sensa itakuwa vizuri kwani itakuwa rahisi kujua idadi na kutoa chanjo kwa mbwa na kwa wale wanaozurura wauliwe ili kuepusha madhara kwa wananchi.

Sunday, August 25, 2024

WAHITIMU WAASWA KUEPUKA VISHAWISHI

WANAFUNZI wanaohitimu masomo ya kidato cha nne na darasa la saba nchini watakiwa kuepukana na tamaa na vishawishi ili visikatishe ndoto zao za kuendelea na masomo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chuo cha Diplomasia Jacob Nduye wakati wa mahafali ya Darasa la saba na Kidato cha nne Shule za Filbert Bayi.

Nduye alisema kuwa ili wanafunzi hao waweze kufikia ndoto zao wanapaswa kujiepusha na tamaa na vishawishi ambavyo vimekuwa kikwazo kufikia kule walikopanga kufika.

"Epukeni tamaa na vishawishi na vitu ambavyo havina maadili kwani ili ufikie malengo yako unapaswa kukaa mbali navyo ili ufikie ndoto zako ambazo umejiwekea,"alisema Nduye.

Alisema kuwa wazazi wanawasomesha wanatumia gharama kubwa wanajinyima ili wasome lakini baadhi wamekuwa wakikatisha masomo kutokana na kujiingiza kwenye vishawishi.

"Nyie ni tegemeo la Taifa kwa siku za baadaye lakini ili muwe tegemeo lazima msome na kuachana na matendo yasiyofaa ndani ya jamii hivyo lazima mjilinde,"alisema Nduye.

Aidha alisema kuwa wazazi nao wanapaswa kuwalea watoto wao kwenye maadili mema na washirikiane na walimu katika kuwalea watoto ili wawe na maadili mema kwani ni viongozi wa baadaye.

Naye Mwenyekiti wa bodi Taasisi ya Filbert Bayi alisema kuwa mbali ya shule hizo kufanya vizuri lakini inakabiliwa na changamoto ya ubovu wa barabara.

Bayi alisema barabara inayotoka Picha ya Ndege kwenda Jamaica na kutoka Jamaica kwenda Picha ya Ndege barabara hiyo ambayo inapita kwenye shule hizo ni mbaya na haijachongwa muda mrefu hivyo jamii inayozunguka shule inapata changamoto kubwa kwenda kupata huduma ya afya kwenye zahanati ya Bayi.

Akisoma risala ya wahitimu wa kidato cha nne Mariam Msabaha alisema kuwa mbali ya masomo ya kawaida pia walisoma masomo ya ujasiriamali ambayo yatawasaidia mara wamalizapo shule.

Msabaha alisema kuwa masomo hayo ni pamoja na ususi, mapishi, upambaji na utunzaji wa mazingira na masuala ya michezo ambapo shule imekuwa ikifanya vizuri kitaifa na kimataifa.



Thursday, August 22, 2024

HALIMA JONGO ACHAGULIWA MAKAMU MWENYEKITI BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBAHA.

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha limemchaguaHalima Jongo kuwa makamu mwenyekiti baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Shomari Mwinshehe kumaliza muda wake.

Sambamba na uchaguzi huo wa makamu mwenyekiti ambaye alipata kura zote 17 pia kamati mbalimbali nazo zilichaguwa wenye viti wake.

Jongo ameshukuru madiwani wenzake kwa kumchagua kwa kura nyingi na kusema atashirikiana nao pamoja na watumishi wa Halmashauri ili kuleta maendeleo kwa wananchi.

Amesema kuwa ataendeleza yale ambayo aliyoyafanya mtangulizi wake ili Halmashauri iweze kupata mafanikio ambayo itakuwa ni sehemu ya wananchi kujiletea maendeleo.

"Katika ukusanyaji mapato tumefanya vizuri kwenye awamu hii iliyopita kwa kushirikiana na wenzangu, wataalamu na wananchi kuhakikisha tunakuwa na makusanyo makubwa,"amesema Jongo.

Amesema kuwa jambo kubwa ni kupambana kuleta maendeleo kwa wananchi ambao wanawategemea kuwaonyesha njia.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Regina Bieda amesema kuwa anampongeza Makamu mwentekiti aliyepita na anamkaribisha Makamu mpya katika kuendeleza jitihada za maendeleo.

Bieda amesema watashirikiana wote kwa pamoja ili kuwapambania wananchi lengo waweze kupata maendeleo.



Wednesday, August 21, 2024

DC KIBAHA ATAKA MADIWANI KUKAGUA NA SI KUTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO











MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amewataka Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Kibaha kukagua miradi ya maendeleo na siyo kuitembelea.

John ameyasema hayo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya nne Aprili hadi Juni kilichofanyika Mlandizi.

Amesema kuwa kukagua miradi ni tofauti na kutembelea ambapo unapokagua unaupata taarifa za kina tofauti na unapoitembelea.

"Tusitembelee miradi bali tuikague kwani pale tutapata fursa ya kujua mambo mengi tofauti na ukitembelea hupati taarifa za kina juu ya miradi ya maendeleo kwa wananchi,"amesema John.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala amesema kuwa wataongeza nguvu katika ukusanyaji mapato ili waweze kufikia malengo.

Makala amesema mafanikio kwenye ukusanyaji mapato ni mkubwa na kadri makusanyo yanavyoongezeka na miradi nayo inaongezeka hivyo kusogeza maendeleo kwa wananchi.

Wakati huo huo Baraza hilo limemchagua Diwani Halima Jongo kuwa makamu mwenyekiti baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Shomari Mwinshehe kumaliza muda wake.

Sambamba na uchaguzi huo wa makamu mwenyekiti ambaye alipata kura zote 17 pia kamati mbalimbali nazo zilichaguwa wenye viti wake.

Jongo alishukuru madiwani wenzake kwa kumchagua kwa kura nyingi na kusema atashirikiana nao pamoja na watumishi wa Halmashauri ili kuleta maendeleo kwa wananchi.


Sunday, August 18, 2024

TAKUKURU PWANI KUTOA ELIMU KUELEKEA UCHAGUZI


KATIKA kukabiliana na vitendo vya rushwa kwenye mchakato wa uchaguzí Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imejipanga kuzuia na kupambana na vitendo hivyo kwa kutoa elimu kwa makundi mbalimbali.

Hayo yalisemwa na Naibu Kamanda wa Takukuru mkoani humo Ally Haji wakati akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha wanatarajia kuyafikia makundi yote yanayohusika na masuala ya uchaguzi.

Haji alisema kuwa baadhi ya makundi ni pamoja nan a vyama vya siasa, wasimamizi wa uchaguzi,
waandishi wa habari wananachi na jamii kwa ujumla.

"Kwa kipindi hichi cha mchakato wa uchaguzi tumeshaanza kufanya ufuatiliaji wa vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji utakaofanyika mwaka huu na uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani,"alisema Haji.

Alisema kuwa wanatoa elimu ya madhara ya rushwa ambapo ni kosa kisheria endapo ikitumika
itasababisha kupatikana víongozi ambao siyo wazuri na hawataweza kuongoza wananchi kwa
weledi ambapo kauli mbiu inasema Kuzuia Rushwani Jukumu lako na langu Tutimize wajibu wetu. 

"Malengo ya kutoa elimu kwa makundi hayo ni kujiandaa kufanya uchaguzi usiokuwa na vitendo vya rushwa ili kupata viongozi bora wasiotokana na vitendo vya rushwa kwani ni adui wa haki na watu wote wana wajibu wa kupambana na vitendo hivyo,"alisema Haji.

Aidha alisema kuwa wataendelea kufanya udhibiti wa mapato ya serikali na usimamizi wa rasilimali za umma ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Tunatoa wito kwa wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada za kufichua vitendo vya rushwa na wala rushwa kwa kutoa taarifa sahihi zitakazowezesha kuwachukulia hatua wahusika hasa katika kipindi hichi tunapoelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu,"alisema Haji.

Aliwataka watumishi wa umma na wa sekta binafsi watakeleze majukumu yao kwa kuzingatia sheria,
kanuni na taratibu za kazí zao ili kuzuia vitendo vya rushwa na kuleta tija katika kuhudumia wananchi ili
kuwaonyesha njia kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

mwisho.

Friday, August 16, 2024

MUHARAKANI/MKUZA WAITAKA TARURA KUBORESHA BARABARA YA MTAA HUO

KUFUATIA changamoto ya ubovu wa barabara ya Jamaika kupitia shule ya Filbert Bayi wakazi wa Mtaa wa Muharakani Kata ya Picha ya Ndege Wilayani Kibaha wameitaka Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) kuifanyia matengenezo barabara hiyo ili kuwaondolea adha.

Wakizungumza na waandishi wa habari Mtaani hapo Mohamed Lukemo, Mathias John na Felix Swai walisema kuwa kutokana na ubovu huo umesababisha kalavati lililopo kwenye barabara hiyo kuwa hatarini kuvunjika ambapo kipindi cha mvua magari yalikuwa yakishindwa kupita.

Walisema kuwa barabara hiyo ilichongwa miaka sita iliyopita hali ambayo imeiacha barabara hiyo kwenye hali mbaya na kufanya wakazi hao kupata changamoto hasa kipindi cha mvua kutokana na kuwa na mashimo mengi.

"Tunawaomba Tarura waikumbuke barabara yetu kwani imeharibika vibaya sana na kwa wagonjwa ni changamoto kubwa sana hata magari yanayobeba wanafunzi yapita kwa taabu pale kwenye kalavati,"walisema wakazi hao

Aidha walisema magari yanapata ubovu na kwa wale wanaotumia pikipiki hupandishiwa nauli hasa kipindi cha mvua au wakati mwingine wanakataa kabisa kubeba abiria wanaopita barabara hiyo.

Ally Mohamed alisema kuwa wanashirikiana na wananchi ambapo wanajitolea kuikarabati barabara hiyo kwa baadhi ya maeneo korofi ili ipitike.

Mohamed alisema kuwa taarifa juu ya ubovu wa barabara hiyo wamezipeleka sehemu husika lakini utekelezaji ndo imekuwa changamoto ambapo waliambiwa wasubiri bajeti ya mwaka huu.

Naye meneja wa Tarura Wilaya ya Kibaha Mhandisi Samwel Ndoveni alikiri kuwa barabara hiyo ina changamoto lakini iko kwenye mpango wa kuchongwa.

Ndoveni alisema kuwa tayari wameshapeleka wataalamu kufanya tathmini na wiki ijayo watachonga barabara pamoja na kukarabati sehemu ya kalavati hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi.


Wednesday, August 14, 2024

SERIKALI YATAKIWA KUWA NA VITUO VYA KULEA VIPAJI VYA WACHEZAJI WA UMISSETA NA UMITASHUMTA ILI KUINUA MICHEZO NCHINI

SERIKALI imetakiwa kuwa na vituo vya kuwaandaa wachezaji wenye vipaji wanaoshinda kwenye michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA ili viweze kushindana kwenye mashindano ya kimataifa.

Aidha imetakiwa kuwezesha shule au vituo vya watu binafsi ambavyo vinakuza vipaji vya wanafunzi ili kuja kupata wanamichezo wenye uwezo na kuliletea sifa Taifa.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya ushiriki wa Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa hususani ya Olimpiki.

Bayi alisema kuwa ili kuwa na timu bora ambazo zitashindana kwenye mashindano za kimataifa lazima kuwe na vituo ambavyo vitawaandaa vijana mahiri ambapo wataandaliwa.

"Siri ya kufanya vizuri ni kuwa na vituo maalum au shule ambazo zitawachukua vijana hao ambao wanafanya vizuri kwenye mashindano hayo na kuwaandaa kwa muda mrefu ili waweze kufanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali ikiwa ni pamoja na Olimpiki,"alisema Bayi.

Alisema kuwa kuwe na uwekezaji kwenye kambi maalum siyo kwa ajili ya kushiriki mashindano makubwa bali kuwaandaa wale wenye vipaji ambapo kwa sasa hao wanaofanya vizuri haijulikani wanaenda wapi.

"Tuliambiwa kutakuwa na vituo au shule 56 lakini jatujui imeishia wapi kwani kwa sasa michezo inakwenda kisayansi ambapo wenzetu wamewekeza kwa vijana wao wenye vipaji ambap ndiyo wanaleta mafanikio,"alisema Nyambui.

Alibainisha kuwa fedha zinazorudishwa kwa wananchi kupitia uwekezaji zipelekwe kwenye masuala ya michezo ambapo asilimia tano ya michezo ya kubahatisha inapelekwa Baraza la Michezo BMT lakini ni ndogo inapaswa kuongezwa ili ilete matokeo.

"Kuna shule au vituo kama vile Allince, Kipingu, Makongo, Bagamoyo na Filbert Bayi ni sehemu ambazo zinafanya jitihada kuandaa vijana ni vema vikawezeshwa na serikali ili viweze kuandaa vizuri vijana kwani wanawagharamia vijana hao kwani wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha,"alisema Bayi.

 Akizungumzia timu iliyoshiriki mashindano ya Olimpiki yaliyomalizika huko Ufaransa alisema wachezaji waliokwenda walikuwa na viwango vizuri lakini ilitokea tu bahati mbaya lakini waliandaliwa vizuri na kushinda au kushindwa ni matokeo tu.

WANANCHI PWANI WATAKIWA KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KWENYE DAFTARI LA MPIGAPICHA

 

WANANCHI Mkoani Pwani wametakiwa kujitokeza kwenye hatua za awali za kujiandikisha au kuboresha taarifa zao kwenye daftari la mpiga kura ili waweze kushiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Vijana (YPC) Kibaha Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha.

Ilunde alisema kuwa Ypc imepeta mradi wa michakato ya uchaguzi (K-VOTE) ambao unawahamasisha uwepo wa vijana kwenye masuala ya umma, elimu ya mpiga kura, uraia, kuwapatia elimu vijana wanaotaka kuwania nafasi za uongozi.

"Usipojiandikisha hutaruhusiwa kupiga kura na viongozi wabaya huwekwa madarakani na raia wema wasiojitokeza kupiga kura hivyo kuna haja ya wananchi kutumia fursa hiyo ya kujiandikisha au kuboresha taarifa zao mara zoezi hilo litakapofanyika Mkoani Pwani,"alisema Ilunde.

Alisema kuwa vijana milioni tano wataandikishwa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ambapo Tume Huru ya ya Uchaguzi iko kwenye uandikishaji na uboreshaji wa daftari la wapiga kura kwa ajili ya wapiga kura.

"Tutakuwa tukitoa elimu juu ya elimu ya mpiga kura kwa kushirikiana na mitandao mbalimbali lengo ni kuwahamasisha wananchi kushiriki uchaguzi kwani ni haki yao ya msingi ya kuchagua au kuchaguliwa,"alisema Ilunde.

Aidha alisema pia elimu hiyo wataitoa ndani na nje ya shule na vyuo ambapo watawahamasisha hata wale ambao walijiandikisha lakini hawapigi kura kwani wasipopiga kura watachaguliwa viongozi ambao watawaamulia na watu wengine.

"Ushiriki wa vijana kwa mwaka 2004 uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2005 vijana walikuwa ni asilimia nane na uchaguzi wa 2015 waliongezeka na kufikia asilimia 50 na tunatarajia mwaka huu na mwakani wataongezeka,"alisema Ilunde.

Aliongeza kuwa vijana hao waligombea nafasi mbalimbali kuanzia serikali za mitaa, udiwani na ubunge na baadhi walichaguliwa kuwa Manaibu Mawaziri wakiwemo Dk Zainab Katimba, Salome Makamba ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum.

"Vijana wapambane kugombea nafasi husika lakini wasinunue kura kwani zinavunja heshima ya nchi na zinaliaibisha taifa kwani wakiingia kwa njia hiyo uongozi wao utakuwa wa kulipa madeni hivyo wafanye siasa safi za heshima na siyo za matusi,"alisema Ilunde.

Aliwataka watoe hoja kwa kuweka utu mbele kwa kuijali jamii na wajue kuwa kuna kushinda na kushindwa na wakubali matokeo kwa kutokufanya fujo ambapo TAMISEMI na Tume Huru ya Uchaguzi watasimamia vyema vyema uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani.


Tuesday, August 13, 2024

WIZARA YA MAJI IMEJIPANGA MABWAWA YA MAJI NA TOPE SUMU YANAKIDHI VIGEZO.

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Wizara ya Maji kupitia Idara ya Rasilimali za Maji ina jukumu la kuhakikisha mabwawa ya maji na tope sumu yanakidhi vigezo vya usalama wa mabwawa kwa mujibu wa Sheria ya Rasilimali za Maji ili kuepusha madhara yatakayojitokeza katika jamii.

Hayo yamesemwa leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Maji uliopo Mtumba Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri, amesema Wizara ya Maji imeandaa mafunzo ya siku mbili katika kuhakikisha usalama wa mabwawa ya maji na tope sumu unaimarishwa.

Aidha Mhandisi Waziri amesema kuwa mafunzo yatahusisha watalaam kutoka wamiliki wa migodi kwa ajili ya usalama wa mabwawa ya tope sumu, wamiliki wa mabwawa makubwa ya maji, wataalam wa mabwawa waliosajiliwa na wataalam kutoka Serikalini.

Sambamba na hayo Mhandisi Waziri ameongeza kuwa mafunzo hayo yameandaliwa kwa kushirikiana na Tanzania Chamber of Mines na yatafanyika mkoani Mwanza .

TAKUKURU PWANI YAOKOA BILIONI 1.6

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 1.6 kutoka vyanzo mbalimbali vya Halmashauri ya Mji Kibaha.

Hayo yamesemwa na Naibu Kamanda wa Takukuru Mkoa huo Ally Haji wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha juu ya kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu.

Haji amesema kuwa walibaini hayo wakati wa ufuatiliaji wa ukusanyaji wa ushuru wa huduma kama mbalimbali kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili kwa kushindwa kuwajibika.

"Katika ufuatiliaji tuligundua kuwa baadhi ya watumishi wa Halmashauri kwenye kitengo cha ukusanyaji wa mapato watumishi kushindwa kufuata sheria, kanuni, na taratibu za ukusanyaji na kufanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1.6 zilizokuwa zinapotea,"amesema Haji.


Monday, August 12, 2024

VIJANA WAJA NA SERA MPYA

SERIKALI imezindua Sera mpya ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007 toleo la 2024, ambayo inakwenda kujibu changamoto mbalimbali za vijana na kutoa mwongozo wa kuanzishwa rasmi kwa Baraza la Taifa la Vijana.

Hayo yamebainishwa leo Agosti 12,2024 Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu,Mhe. Ridiwani Kikwete, wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya vijana kimataifa.

“Serikali imekwisha kamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Vijana ya mwaka 2007 na marekebisho yake imefanyiwa mwaka 2024 na leo hii tunakwenda kuizindua muda mfupi ujao.

“Ndugu washiriki changamoto nyingi zinazoelezwa kwa vijana zinatokana na ukweli kwamba yako baadhi ya maeneo hayana miongozo yake kupitia sera hii ya vijana ambayo tutaizundua leo nina hakika kabisa vilio vya vijana wengi vinakwenda kupataiwa ufumbuzi baada ya kupitishwa kwa sera hii”ameeleza.

Aidha, amesema kuwa sera hiyo inaeleza uelekeo na njia ambazo wanakwenda kuzitumia kwa pamoja ili kufikia malengo ambayo yanatatua matatizo waliyonayo vijana.

“Sera hii inakwenda kuanzisha baraza la taifa la vijana uanzishaji wa baraza hili la vijana unakwenda kuwa muarobani wa kutambua na kutatua changamoto nyingi za vijana.

“Vijana wamekosa maeneo ya kueleza changamoto zao vijana walikosa watu wa kuwasikiliza, vijana walikosa msukumo wa kufikisha changamoto zao na kuzitafutia majawabu kwa pamoja”amesema Mhe.Ridhiwan.

Amesema, ujio wa sera hiyo ya vijana na uudwaji wa baraza la taifa la vijana unaonesha wazi azma ya Rais Samia kujidhatiti na changamoto zote zinazo wakabili vijana zinapatiwa majibu.

Hata hivyo amesema kuwa sera hiyo pia inakwenda kutambua vijana katika sekta zote wanaofanya kazi katika maeneo hatarishi ikiwemo ya madini, maeneo ya uzalishaji mali ikiwemo mashambani na kwenye mifugo.

“Wapo vijana wanaofanya kazi za sanaa ikiwemo wabunifu, muziki, michezo, ubunifu na utungaji wa sanaa mbalimbali sera hii inakwenda katika maeneo hayo.

Pia  ametoa  wito kwa maafisa kazi kutambua kuwa nafasi zao siyo za kukaa ofisini wakisubiri vijana waje kulia na kueleza changamoto zao.

Kwa upande wake Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Mary Maganga,amesema katika kuadhimisha siku ya vijana, wameendesha kongamano la siku mbili lililokutanisha vijana zaidi ya 3,000 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania.

“Katika kongamano hilo, vijana wamechangia juu ya mada za Sera ya Maendeleo ya 2050, fursa za kidigitali, vijana na uchumi, afya ya akili na saikolojia ya vijana na kusisitiza kuwa serikali imechukua maoni ya vijana katika eneo la elimu, afya, ajira na uwezeshaji.”amesema Bi.Maganga

Naye Mwakilishi wa Vijana, Charles Ruben amempongeza Rais Samia kwa jitihada zake kuwainua na kuwasaidia vijana wa kitanzania na kuwa vijana wamepata elimu na ujuzi wa kazi unaofanya vijana kushiriki katika shughuli za kiuchumi na kuwapo ongezeko la vijana kwenye uongozi.

 “Ajira za vijana zimeongezeka ambapo kuanzia mwaka 2023 hadi 2024 ajira 607675 zimezalishwa huku ajira 204,000 zikitokana na miradi ya kimkakati inayotekelezwa hapa nchini huku akitenga Sh bilioni 1.1 kwa ajili ya miradi ya jenga kesho iliyobora BBT ambayo inawalenga vijana.”amesema Ruben

Friday, August 9, 2024

SELF MICROFINANCE WATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Katika kuadhimisha kilele cha siku ya wakulima na wafugaji Nane Nane, Mfuko wa Fedha wa (SELF MICROFINANCE) ulio chini ya Wizara ya Fedha umewataka  wananchi wote wanaojishughulisha na shuguli za Kilimo, Ufugaji na Uvuvi kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na mfuko huo ili kukuza na kuongeza uzalishaji.

Wito huo umetolewa na Bi. Linda Mshana ambaye ni meneja masoko na uhamasishaji kutoka mfuko wa SELF wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la SELF lililopo katika maonesho ya Kitaifa ya Nanenane Jijini Dodoma.

Bi. Linda amesema, Mfuko huo una vifurushi mbalimbali kwaajili ya Wakulima, Wavuvi na wafugaji hivyo amewahimiza kujitokeza kwa wingi na kukopa mikopo hiyo ambayo imewekwa maalumu kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi.

Aidha,  Linda ameongeza kuwa mbali na Mikopo hiyo pia Mfuko wa Self unatoa Mikopo kwa taasisi ndogondogo za kifedha kwaajili ya kuwakopesha wakulima, wafugaji na wavuvi sambamba na mikopo mingine inayolenga kukuza uchumi wa watu mbalimbali.

"Self ina mikopo ya aina mbalimbali, tuna mkopo kwa ajili ya taasisi zinazokopesha, hivyo tunawakaribisha wakope na baadaye wawakopeshe wakulima, wafugaji na wavuvi,"amesema.

Linda amewakaribisha wananchi wote kutembelea banda lao lililopo katika maonesho hayo ili kupata elimu na kujua namna gani wanaweza kunufaika na Mikopo mbalimbali inayotolewa na Mfuko wa SELF.

Thursday, August 8, 2024

OFISI MAKAMU WA RAIS YAPONGEZWA UBUNIFU UTENGANISHAJI TAKA

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MWENYEKITI wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu ameipongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa utoaji wa elimu ya ubunifu wa mifumo ya utenganishaji taka ambao ni fursa ya ajira.

Mhe. Jaji Mwaimu ametoa pongezi hizo leo Jumatano Julai 7, 2024) wakati alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais katika maonesho ya Kitaifa ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa taka zinazozalishwa nchini kwa sasa zimekuwa ni fursa kutokana na malighafi hiyo kutumika katika shughuli za uzalishaji mali na hivyo kuchangia katika ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kuchochea maendeleo ya kaya, familia na jamii kwa ujumla.

“Taka ni fursa na pia ni vyanzo vya malighafi muhimu katika shughuli za uzalishaji kutoka. Nawapongeza kwa ubunifu wa utoaji wa elimu kuhusu fursa zilizopo katika taka kwani mbinu mbadala ya kukuza kipato cha jamii na kuhamasisha utunzaji wa mazingira” amesema Mhe. Jaji Mwaimu.

Aidha Jaji Mwaimu amewataka wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kutembelea Banda la Ofisi ya Makamu wa Rais na kujifunza teknolojia na bunifu mbalimbali zinazosaidia masuala ya uhifadhi wa mazingira kwani zipo fursa zinazoweza kusaidia ukuaji wa kipato katika ngazi ya kaya na jamii kwa ujumla.

Ameongeza kuwa taka ni fursa iliyojificha na hivyo elimu kuhusu fursa na manufaa yake wananchi wanapaswa kuitambua kwani sio kila kitu kinachotambulika kama takataka kinatakiwa kutupwa kwenye madampo, bali taka hizo zinaweza kutumika na kuwa fursa kujipatia kipato.

“Taka zinaweza kuwa fursa endapo zitachambuliwa kuanzia sehemu ya uzalishaji mpaka mtu wa mwisho anayetumia bidhaa husika, ili kuweza kuchangamkia fursa hiyo tunatakiwa kujua taka ambazo tunazalisha majumbani na namna zinavyotakiwa kutenganishwa” amesema Jaji Mwaimu.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sarah Kibonde amesema Ofisi hiyo imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali za kuemilisha umma kuhusu masuala ya Muungano na Mazingira ikiwemo maonesho, mikutano ya wadau na vyombo vya habari.

Ameongeza kuwa katika kupanua wigo wa elimu kwa umma kuhusu masuala ya Muungano na Mazingira kupitia maonesho hayo, Ofisi ya Makamu wa Rais imeanisha maeneo matano ya kimkakati kwa ajili ya kuwafikia wananchi na wadau mbalimbali wanaotembelea banda la ofisi hiyo.

Ametaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na masuala ya nishati safi ya kupikia, mabadiliko tabianchi, uchumi wa buluu, fursa zitokanazo na taka, biashara ya kaboni na elimu kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

“Kupitia maonesho tuna nyaraka mbalimbali ambazo ni vitabu ikiwemo Kitabu cha Miaka 60 ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), vipeperushi, majarida ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na wadau nk” amesema Kibonde.

Ofisi ya Makamu wa Rais imeungana na Wizara, Idara, Taasisi na Wakala za Serikali na sekta binafsi kushiriki maonesho ya kitaifa ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma kuanzia tarehe 1-8 Agosti, 2024.

Maonesho hayo yanaongozwa na kauli mbiu isemayo “Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.



DIB KULINDA AMANA ZA WATEJA


Na Wellu Mtaki, Dodoma

Bodi ya Bima ya Amana (DIB) ikiwa na jukumu la kusimamia amana za wateja zinapokuwa kwenye mabenki endapo benki ikifilisika inaweza kumlinda mteja aliyeweka amana zake asiweze kupata hasara.

Hayo yameelezwa na mwenyekiti wa bodi ya Amana (DIB) Emmanuel Tutuba wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la maonyesho ya nanenane Zuguni Jijini Dodoma huku akiwataka wananchi waliokuwa wateja wa benki zilizofilisika waweze kufika katika taasisi hiyo ili kuhakikiwa na kupewa stahiki zao.

Amesema DIB mpaka sasa imeongeza zaidi ya shilingi trilioni 1 ambazo wanaendelea kuwekeza sehemu mbalimbali ambazo fedha hizo ni za wateja endapo benki ikifilisika mteja aweze kupata gawio lake kulingana na alivyowekeza.

"Tangu kuanzishwa DIB ilipewa mtaji  mwaka 1994 na benki kuu ya Taifa (BOT)  walipewa kiasi cha  shilingi bilioni1.5 kwa sasa wana atirioni 1.2.3 fedha hizo zinaendele kuongezeka kwa sababu wanaendelea kuwekeza sehemu mbalimbali fedha hizo zipo  kwa ajiri ya kukinga  amana za wateja hata kama bank ikitokea bahati mbaya  ikafilisika kila  aliyekuwa na account kwenye benki atalipwa kulingana na kiwango  ambacho alichokuwa anaweza kulingana na kiwango  cha asilimia atarejeshewa,"amesema Tutuba. 

Pia ametoka wito kwa wateja wa benki FDME  kama kuna mtu ajapewa mgawanyo wa asilimia 30 aweze kufika kwenye  bodi ya bima ya Amana ili aweze kupatiwa utaratibu.

"Wametoa wito kwa wateja  kwenye benki FDME kama kuna mtu ajapewa mgawanyo wa asilimia  30 cha awali aweze kufika taasisi hii ya bima ya amana ili aweze kupitia taratubu zote kujiludhisha Ili  arejeshewa kiwango 30 Cha awali." Amesema Tutuba.

Aidha Tutuba hakusita kueleza mfano wa faida ya mfuko huo unaosimamiwa na DIB kupitia mfano wa zile benki ambazo zilizowahi kufilisika nchini.

Amewapongeza kusimamia shughuli zao za kusimamia amana za wateja na cha msingi DIB  kazi yake ni kuweka  na kuendelea kuwekeza bima ili kukinga viatarishi ambavyo  vitajitokeza endapo benki itafilisika, pia  kuna baadhi ya watu ambao benki zao zilifilisika mwanzano wanatakiwa wafiki DIB" Amesema Tutuba.

Wednesday, August 7, 2024

FILBERT BAYI WATAMBA KUFANYA VEMA FEASSA

WANARIADHA tisa kutoka Shule ya Sekondari ya Filbert Bayi ambao wataiwakilisha nchi kwenye mashindano ya shule za sekondari Afrika Mashariki na Kati (FEASSA) yanayotarajiwa kufanyika mwezi huu nchini Uganda wameahidi ushindi.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi vikombe walivyoshinda huko Tabora kitaifa kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta ofisini kwake Mjini Kibaha mwalimu wa timu hiyo Ally Nyonyi alisema kuwa wanariadha hao ni wa mbio tofauti tofauti.

Nyonyi alisema kuwa wanariadha hao wanaendelea vizuri na mazoezi kwenye uwanja wa shule uliopo Kibaha Mkoani Pwani huku wakiwa na matumaini makubwa ya kufanya vizuri kwenye michuano hiyo.

"Wachezaji wetu tisa ambao walichaguliwa kwenye mashindano ya Umisseta yaliyomalizika hivi karibuni mkoani Tabora wanaendelea vizuri na mazoezi kwenye kambi iliyoko pale shule na wote wako vizuri,"alisema Nyonyi.

Alisema kuwa kambi inaendelea vizuri na hakuna mchezaji ambaye ana tatizo wote wako vizuri wanasubiri tu kuingia kwenye kambi ya mwisho itakayokuwa huko Tabora na mwaka huu wamejiandaa vizuri.

"Tangu mashindano ya Raidha ya Taifa yaliyofanyika mkoani Tabora timu iliingia kambini na hadi sasa inaendelea na mazoezi na hawana muda wa kusubiri kwani sisi ndiyo utaratibu wetu wa kufanya mazoezi kila siku,"alisema Nyonyi.

Aidha alisema kuwa wana mazoezi ya kutosha na wana morali ya hali ya juu na hakuna changamoto yoyote inayowakabili na wako vizuri wakiwa na afya nzuri.

"Sisi ni mabingwa wa Umisseta hapa nchini kwa miaka mitatu mfululizo siri kubwa ya wachezaji wangu kufanya vizuri ni nidhamu na kufuata maelekezo ya mwalimu na vifaa vipo mazingira ni rafiki,"alisema Nyonyi.

Aliomba wadau wa mchezo huo kuwaunga mkono kwa kuwasaidia baadhi ya vitu ikiwa ni pamoja na maji, matunda na motisha ili waweze kufanya vyema.

Kwa upande wa mwanariadha Emanuel Amos alisema kuwa amejipanga vizuri na anategemea kushinda kwani atahakikisha anafanya juhudi ili kufanikisha kushinda.

Amos alisema kuwa amepata uzoefu mkubwa kwani hayo yatakuwa mashindano yake ya pili ambapo mara ya kwanza hakuweza kufanya vizuri sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kushiriki hivyo hakuwa na uzoefu.

Naye Elizabeth Kelaryo alisema kuwa wamejiandaa vyema na watavitumia vyema vipaji vyao na watahakikisha wanapambana kwani shuleni kwao wamefundishwa kupambana.

Kelaryo alisema kuwa wanajiamini na kikubwa ni ushirikiano walionao ndiyo unaowafanya waweze kufanya vizuri na maandalizi wanayoyafanya na mbinu bora za mwalimu wao watafanya vyema.

Wachezaji wanaounda timu hiyo ni Emanuel Amos anayekimbia mbio mita 100 na 200, Kimana Kibase 100 na 200, Wiliam Makaranga kupokezana vijiti mita 400, Yohana Samwel 400, Sharifa Mawazo kupokezana vijiti mita 400.

Wengine ni Eliza Kelaryo kutupa mkuki, Sara Masalu mita 1,500, Lucia Pius mita 400 kupokezana vijiti, Salma Samwel 800 na kupokezana vijiti mita 400.



 




BRELA YAZUIYA KUTAPELIWA KWA WATEJA

Na Wellu Mtaki,Dodoma.

Wakala wa Usajili wa biashara na leseni (BRELA) imeweka mfumo wa kujisajili katika mtandao ambao utazuia mteja kuacha  kutumia mtu ambaye atasimamia katika usajili ambao utamfanya mteja kulipa kiasi cha ziada tofauti na malipo ambayo yamewekwa na BRELA

Hayo yameelezwa leo tarehe 6 Agost 2024 na Msaidizi wa Usajili Yvonne Massele wakati akizungumza na waandishi wa habari katika  maonesho ya nanenane Zuguni Jijini Dodoma huku akiwataka wananchi kutembelea banda la Brela ili kutambua huduma zinazopatika katika banda hilo.

Massele amesema kuwa mfumo wa usajili wa Brela kwa njia ya Mtandao unamsaidia mteja kurahisisha usajiri kwa mteja ambaye yupo mbali na huduma.

"Sasa hivi tunajisajiri kwa njia ya mfumo na ukiingia kwenye Mfumo unaweza kupata naomba ya malipo ( control number) na kama mteja atapata changamoto Kuna mawasiliano ambayo atawasiliana na mtoa huduma moja kwa moja,"amesema Massele.

Aidha ameelaza kuwa huduma ambazo zinatolewa katika maonesho ya nanenane ni pamoja na usajili wa kampuni,  usajili wa biashara, usajili wa harama za biashara, huduma pamoja na kutoa leseni ya biashara jina la kampuni kwa siku hiyo hiyo uliofika kujisajili.

"Ujio wao ni kwa ajili wa kutoa huduma zetu za Brela ambazo zinafanyika ni usajiri wa kampuni, usajili wa biashara , usajili wa harama za biashara na huduma pamoja na kutoa leseni la biashara la kundi A pamoja na leseni za viwanja,"amesema Massele 

Pia amesema kuwa wanaendelea kutoa Elimu kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa ili waweze kutambua namna ya kusajili biashara zao kwa wale ambao bado hawajasajili 

"Tumekuja kutoa Elimu kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ambao awajasajili biashara  waweze kusajili biashara zao na wale ambao biashara zao zishakuwa waweze kusajiri majina ya Kampuni " amesema

Tuesday, August 6, 2024

MSONGO WA MAWAZO HUSABABISHA MAZIWA YA AKINAMAMA WANAONYONYESHA YASITOKE








IMEELEZWA kuwa moja ya sababu zinazosababisha maziwa ya akinamama wanaonyonyesha kushindwa kutoka ni msongo wa mawazo.

Aidha wanaume ambao wake zao wananyonyesha wameshsuriwa wasiwaudhi wake zao ili wasisababishe maziwa yashindwe kutoka na kushindwa kunyonyesha watoto wao.

Hayo yalisemwa na Katibu wa Afya Amour Mohamed ambaye alimwakilisha mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Kibaha wakati wa Siku ya Unyonyeshaji Duniani kwa Halmashauri hiyo yaliyofanyika kwenye Zahanati ya Mwendapole.

Mohamed alisema kuwa baadhi ya wanaume wamekuwa wakiwasababishia wake zao wanaonyonyesha msongo wa mawazo hivyo maziwa kushindwa kutoka hivyo watoto kukosa maziwa.

"Wanaume tunapaswa tushiriki katika makuzi ua watoto wetu wachanga kwani ndiyo chakula chao kikuu ambapo moja ya changamoto ni maziwa kushindwa kutoka na moja ya chanzo ni wazazi kuwa na mawazo ambayo wakati mwingine husababishwa na waume zao,"alisema Mohamed.

Alisema kuwa wasiwaudhi wake zao katika kipindi hicho cha unyonyeshaji kwani hudababisha maziwa yasitoke na wanapaswa kuhakikisha wazazi wanapata lishe bora ili makuzi ya watoto yawe mazuri.

Naye Diwani wa Kata ya Kibaha Goodluck Manyama ambaye alikuwa Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alisema kuwa maziwa ya mama ni muhimu tofauti na maziwa mengine.

Manyama alisema kuwa maziwa ya mama yana kinga nyingi kujikinga na maradhi kuliko ya ng'ombe au ya kopo lakini ya mama yana ubora na ukuzaji wa mtoto kwa haraka.

Kwa upande wake Muuguzi Mkuu na Kaimu Ofisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Kibaha Asteria Massawe alisema kuwa ndani ya saa moja mama aanze kumnyonyesha mtoto.

Massawe alisema kuwa yanayoanza kutoka ni maji hivyo lazima mtoto anyonye vya kutosha ili maziwa yaishe kabisa ndipo uhamishie ziwa lingine na amnyonyeshe mara 10 kwa siku au kila baada ya saa moja.

Akitoa maelekezo juu ya unyonyeshaji sahihi Muuguzi wa Zahanati ya Mwendapole Nyasungi Pepya alisema kuwa mtoto anapaswa kupata vipimo mara tano tangu mama akiwa mjamzito lengo ni mtoto azaliwe akiwa salama.

Pepya alisema kuwa vipimo husaidia kujua hali ya mama na kama akigundulika kuwa na maambukizi atapewa dawa ili kumlinda mtoto.

 

TEAC IMELENGA KUSAIDIA MKULIMA NA MFUGAJI.

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma.

Mkuu wa Kanda ya kati ya Tume ya Nguvu za Atom Tanzania ( TEAC ) Machibya Anthony Matulanya amesema kuwa Tume imelenga  kusaidia wakulima na wafugaji kupata mavuno makubwa ambayo yataongeza pato la uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja .

Hayo ameyasema Leo Tarehe 5 Agost 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika Banda la Tume ya Nguvu za Atom Tanzania Katika viwanja vya nanenane Zuguni jijini Dodoma huku akiwasihi wananchi kutembelea Banda ilo Ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuza na kuboresha kilimo na ufugaji.

Adha amesema kuwa Tume inajishughulisha na swala la uhamasishaji wa Matumizi ya Nuclear nchini ambayo inalenga kuhakikisha teknologia ya nuclear inakunza uchumi wa nchi.

"Tume ya nguvu za Atom Tanzania zinajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama  ambapo wanalenga kuhakikisha kwamba teknologia ya Nuclear nchini  inatumika vizuri na inakuza uchumi wa nchi." Amesema Matulanya

Pia meeleza kuwa teknologia ya nuclear imeweza kutumika kuangamiza  wadudu aina ya Mbung'o ambao wanang'ata Mifugo na  kusababusha Hali ya upungufu wa Maziwa kwa ng'ombe pamoja na kukosa nyama iliyo Bora.

"Kwa upande wamifugoTeknologia ya Nuclear imetumika imeangamiza wadudu aina ya Mbung'o , Mb'ung'o ni wadudu atali ambao wanang'ata Mifugo 

Hawa wadudu waking'ata kwa mfano Ng'ombe wanamsababishia Hali ya upungufu wa Maziwa na pia uwezi kupata nyama nzuri" amesema Matulanya.

Mayulanya amesema kuwa zipo mbegu Bora za Mpunga ambazo zinatumika Tanzania bara na nzazibar ambazo zinauwezo Mkubwa wa kuimili ukame na ahitaji maji Mengi katika kuzalisha na unafanya mmea usivunjike .

"Pia kwa upande wa kilimo teknologia ya Nuclear imetumiaka huko nzazibar na bara, mbegu ya mpunga aina ya   super DC  ambayo inatumika Mbegu hizi ambazo zimeboreshwa  uwezo Mkubwa wa kuimili ukame ambayo mbegu hiyo ukiilima aitaji maji Mengi Katika kutoa matunda yake" Amesema Matulanya 

"Baada ya kuboreshwa mbengu hiyo imekuwa na stimilivu na yenye kutoa faida kubwa kwa mkulima pamoja na mmea kustaimili usivunjike na huo mpunga baada ya kuuvuna na kuukoboa unakuwa mtamu" Amesema Matulanya 

Ikumbukwe kuwa  Tume ya Atom Tanzania  inajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama.

TEAC IMELENGA KUSAIDIA MKULIMA NA MFUGAJI.

Na Wellu Mtaki, Dodoma.

Mkuu wa Kanda ya kati ya Tume ya Nguvu za Atom Tanzania ( TEAC ) Machibya Anthony Matulanya amesema kuwa Tume imelenga  kusaidia wakulima na wafugaji kupata mavuno makubwa ambayo yataongeza pato la uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja.

Hayo ameyasema Leo Tarehe 5 Agost 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika Banda la Tume ya Nguvu za Atom Tanzania Katika viwanja vya nanenane Zuguni jijini Dodoma huku akiwasihi wananchi kutembelea Banda ilo Ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuza na kuboresha kilimo na ufugaji.

Adha amesema kuwa Tume inajishughulisha na swala la uhamasishaji wa Matumizi ya Nuclear nchini ambayo inalenga kuhakikisha teknolojia ya nuclear inakunza uchumi wa nchi.

"Tume ya nguvu za Atom Tanzania zinajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama  ambapo wanalenga kuhakikisha kwamba teknologia ya Nuclear nchini  inatumika vizuri na inakuza uchumi wa nchi." Amesema Matulanya.

Pia meeleza kuwa teknologia ya nuclear imeweza kutumika kuangamiza  wadudu aina ya Mbung'o ambao wanang'ata Mifugo na  kusababusha Hali ya upungufu wa Maziwa kwa ng'ombe pamoja na kukosa nyama iliyo Bora.

"Kwa upande wamifugoTeknologia ya Nuclear imetumika imeangamiza wadudu aina ya Mbung'o , Mb'ung'o ni wadudu atali ambao wanang'ata Mifugo 

Hawa wadudu waking'ata kwa mfano Ng'ombe wanamsababishia Hali ya upungufu wa Maziwa na pia uwezi kupata nyama nzuri" amesema Matulanya.

Mayulanya amesema kuwa zipo mbegu Bora za Mpunga ambazo zinatumika Tanzania bara na nzazibar ambazo zinauwezo Mkubwa wa kuimili ukame na ahitaji maji Mengi katika kuzalisha na unafanya mmea usivunjike .

"Pia kwa upande wa kilimo teknologia ya Nuclear imetumiaka huko nzazibar na bara, mbegu ya mpunga aina ya   super DC  ambayo inatumika Mbegu hizi ambazo zimeboreshwa  uwezo Mkubwa wa kuimili ukame ambayo mbegu hiyo ukiilima aitaji maji Mengi Katika kutoa matunda yake" Amesema Matulanya 

"Baada ya kuboreshwa mbengu hiyo imekuwa na stimilivu na yenye kutoa faida kubwa kwa mkulima pamoja na mmea kustaimili usivunjike na huo mpunga baada ya kuuvuna na kuukoboa unakuwa mtamu" Amesema Matulanya 

Ikumbukwe kuwa  Tume ya Atom Tanzania  inajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama.

Monday, August 5, 2024

BRELA KUANZA KUSAJILI WAKULIMA

Na Wellu Mtaki, Dodoma

OFISA Usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Gabriel Gilangay amesema wakala huo umejipanga kuanza kuwasajili  Wakulima kwa kuwapa nembo ambayo itawatambulisha kibiashara. 

Gilangay amesema hayo Jijini Dodoma kwenye maonesho ya Wakulima Nanenane wakati akizungumza na Waandishi wa habari na kueleza kuwa Wakala huo unashughulikia mambo mengi  kwa wakulima nchini ikiwemo usajili wa Biashara. 

Mbali na hayo amesema  BRELA hutoa huduma hizo ili kuhakikisha  biashara za kilimo zinakubalika kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri kuhusu jinsi ya kufuata taratibu za kisheria katika biashara ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kanuni za usajili, sheria za biashara, na masharti ya leseni.

Kwa upande mwingine Wakala huo hushughulikia Kampuni za Umma,Kampuni zinazoshiriki soko la hisa,Kampuni za Kibinafsi na Kampuni zinazomilikiwa na watu wachache.

TIMU ZA UMISSETA NA UMITASHUMTA MKOA WA PWANI ZAKABIDHI VIKOMBE






TIMU za Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) za Mkoa wa Pwani zimekabidhi makombe ilivyoshinda kwenye mashindano ambayo yaliyomalizika Mkoani Tabora hivi karibuni.

Mchatta akipokea vikombe na tuzo na kuwapongeza wachezaji hao ofisini kwake Mjini Kibaha ambapo timu za riadha zilifanya vizuri kwenye michezo ya riadha na kutupa mkuki kwenye michezo hiyo.

Amesema kuwa wachezaji hao wameuletea sifa mkoa wa Pwani na hiyo imetokana na kutumia vyema vipaji vyao na kuwa na nidhamu na kuzingatia yale waliyofundishwa na walimu wao.

"Nimeambiwa wachezaji tisa watashiriki mashindano ya sekondari kwa nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika hivi karibuni nchini Uganda nawasihi mlinde viwango vyenu,"amesema Mchatta.

Aidha amesema kuwa wanariadha hao waige mfano wa mchezaji wa riadha Steven Akwari ambaye licha ya kuumia lakini alikimbia na kumaliza mbio licha ya maumivu makali.

Naye Mkurugenzi wa Filbert Bayi Elizabeth Mjema amesema kuwa shule inaomba kusaidiwa baadhi ya mahitaji ikiwa ni pamoja na lishe, maji na matunda.

Mjema amesema kuwa inawagharamia baadhi ya wanafunzi wenye vipaji ambao wazazi wao hawana uwezo ambapo lengo la Filbert Bayi ni kutaka wanariadha kufanya makubwa kwenye mchezo huo.

 Kwa upande wake mwalimu wa riadha wa timu za Filbert Bayi Ally Nyonyi amesema kuwa timu hiyo inafanya vizuri kutokana na kuwa na maandalizi mazuri na nidhamu.

Nyonyi amesema kuwa wao ni mabingwa kwa miaka mitatu mfululizo kwenye mashindano ya Umisseta na Umitashumta Taifa hiyo inatokana na kuwa na mazingira rafiki ya kufanyia michezo ambapo wanakuwa na muda mwingi wa kufanya mazoezi baada ya masomo.

Wakielezea jinsi walivyojiandaa na mashindano hayo huko Uganda wachezaji hao wamesema kuwa wamejiandaa vya kutosha na wanaamini watailetea nchi ushindi.

Sunday, August 4, 2024

YPC YAWATAKA VIJANA KUJITOKEZA KUWANIA NAFASI ZA UONGOZI

VIJANA wa kike na kiume wametakiwa kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Vijana (YPC) ya Kibaha Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na Habarileo ofisini kwake.

Ilunde alisema kuwa wameanzisha mradi uitwao (K-Vote) unaohamasisha ushiriki wa vijana kwenye masuala ya umma, elimu ya mpiga kura, uraia, kuwasaidia na kuwaelimisha vijana wanaotaka kuwania nafasi za uongozi kwenye chaguzi hizo.

"Tume Huru ya Uchaguzi inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya vijana milioni tano na wale ambao hawakuwahi kupiga kura miaka ya nyuma tunawasihi wajitikeze kuhakiki taarifa zao itakapofika muda wa kufanya hivyo ili waweze kushiriki kwenye uchaguzi,"alisema Ilunde.

Alisema vijana wanapaswa kushiriki zoezi hilo ambalo ni muhimu sana kwani wasipojiandikisha au kuboresha taarifa zao watakuwa watazamaji na hawataruhusiwa kupiga kura.

"Idadi ya vijana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi serikali za mitaa mwaka 2004 na uchaguzi mkuu mwaka 2005 ilikuwa ni asilimia 8 tu na mwaka 2015 iliongezeka na kufikia asilimia 50 na mwaka huu na mwakani itaongezeka,"alisema Ilunde.

Aidha alisema kuwa baadhi ya vijana hao walichaguliwa kwenye nafasi za uongozi ikiwa ni pamoja na ubunge, udiwani, wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa.

"Tuna mfano wa Dk Zainab Katimba ni Naibu Waziri na mbunge Salome Makamba walifanya vizuri na pia kuachana na dhana kuwa uchaguzi mtaji ni fedha bali ni watu, nidhamu, uchapakazi, kujali watu,"alisema Ilunde.

Aliwataka vijana kutonunua kura kwani zinavunja heshima na zinaaibisha Taifa na uongozi unakuwa wa kulipa madeni pia wafanye siasa za heshima bali ziwe za hoja na kuweka utu mbele na kutofanya vurugu wanaposhindwa na waijali jamii.


Thursday, August 1, 2024

DK BITEKO AMWAKILISHA RAIS MKUTANO MKUU (TLS)

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko leo Agosti 1, 2024 amemwakilisha Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Miaka 70 wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) unaofanyika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma. 

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Pindi Chana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Feleshi, pamoja na Wanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika. 

Itakumbukwa kuwa TLS ilianzishwa mnamo mwaka 1954 ikiwa na mawakili takribani 141 wakiwa ni wakoloni hadi ilipofika mnamo Oktoba 31,1961 ilipopata wakili wa kwanza Mtanganyika.

Hadi sasa TLS ina jumla ya mawakili takribani 12,471 wanaofanya kazi za usaidizi wa kisheria katika taasisi mbalimbali za kisheria nchini.

MH.RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA TRENI YA KISASA (SGR)



Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam – Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam, leo 1 Agosti, 2024.

WAZIRI MKUU AFUNGUA MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 01, 2024 afungua maonesho ya Kimataifa ya Wakulima ya Nanenane ambayo kitaifa yanafanyika  kwenye viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma,

Kauli mbiu ya Maonesho hayo ni Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.