
Tuesday, August 27, 2024
HALMASHAURI KIBAHA YATAKA MBWA WACHANJWE

Sunday, August 25, 2024
WAHITIMU WAASWA KUEPUKA VISHAWISHI
Thursday, August 22, 2024
HALIMA JONGO ACHAGULIWA MAKAMU MWENYEKITI BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBAHA.
BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha limemchaguaHalima Jongo kuwa makamu mwenyekiti baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Shomari Mwinshehe kumaliza muda wake.
Wednesday, August 21, 2024
DC KIBAHA ATAKA MADIWANI KUKAGUA NA SI KUTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO
Sunday, August 18, 2024
TAKUKURU PWANI KUTOA ELIMU KUELEKEA UCHAGUZI
waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha wanatarajia kuyafikia makundi yote yanayohusika na masuala ya uchaguzi.
Haji alisema kuwa baadhi ya makundi ni pamoja nan a vyama vya siasa, wasimamizi wa uchaguzi,
waandishi wa habari wananachi na jamii kwa ujumla.
"Kwa kipindi hichi cha mchakato wa uchaguzi tumeshaanza kufanya ufuatiliaji wa vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji utakaofanyika mwaka huu na uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani,"alisema Haji.
Alisema kuwa wanatoa elimu ya madhara ya rushwa ambapo ni kosa kisheria endapo ikitumika
itasababisha kupatikana víongozi ambao siyo wazuri na hawataweza kuongoza wananchi kwa
weledi ambapo kauli mbiu inasema Kuzuia Rushwani Jukumu lako na langu Tutimize wajibu wetu.
Friday, August 16, 2024
MUHARAKANI/MKUZA WAITAKA TARURA KUBORESHA BARABARA YA MTAA HUO
Wednesday, August 14, 2024
SERIKALI YATAKIWA KUWA NA VITUO VYA KULEA VIPAJI VYA WACHEZAJI WA UMISSETA NA UMITASHUMTA ILI KUINUA MICHEZO NCHINI

WANANCHI PWANI WATAKIWA KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KWENYE DAFTARI LA MPIGAPICHA
WANANCHI Mkoani Pwani wametakiwa kujitokeza kwenye hatua za awali za kujiandikisha au kuboresha taarifa zao kwenye daftari la mpiga kura ili waweze kushiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani.
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Vijana (YPC) Kibaha Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha.Ilunde alisema kuwa Ypc imepeta mradi wa michakato ya uchaguzi (K-VOTE) ambao unawahamasisha uwepo wa vijana kwenye masuala ya umma, elimu ya mpiga kura, uraia, kuwapatia elimu vijana wanaotaka kuwania nafasi za uongozi."Usipojiandikisha hutaruhusiwa kupiga kura na viongozi wabaya huwekwa madarakani na raia wema wasiojitokeza kupiga kura hivyo kuna haja ya wananchi kutumia fursa hiyo ya kujiandikisha au kuboresha taarifa zao mara zoezi hilo litakapofanyika Mkoani Pwani,"alisema Ilunde.Alisema kuwa vijana milioni tano wataandikishwa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ambapo Tume Huru ya ya Uchaguzi iko kwenye uandikishaji na uboreshaji wa daftari la wapiga kura kwa ajili ya wapiga kura."Tutakuwa tukitoa elimu juu ya elimu ya mpiga kura kwa kushirikiana na mitandao mbalimbali lengo ni kuwahamasisha wananchi kushiriki uchaguzi kwani ni haki yao ya msingi ya kuchagua au kuchaguliwa,"alisema Ilunde.Aidha alisema pia elimu hiyo wataitoa ndani na nje ya shule na vyuo ambapo watawahamasisha hata wale ambao walijiandikisha lakini hawapigi kura kwani wasipopiga kura watachaguliwa viongozi ambao watawaamulia na watu wengine."Ushiriki wa vijana kwa mwaka 2004 uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2005 vijana walikuwa ni asilimia nane na uchaguzi wa 2015 waliongezeka na kufikia asilimia 50 na tunatarajia mwaka huu na mwakani wataongezeka,"alisema Ilunde.Aliongeza kuwa vijana hao waligombea nafasi mbalimbali kuanzia serikali za mitaa, udiwani na ubunge na baadhi walichaguliwa kuwa Manaibu Mawaziri wakiwemo Dk Zainab Katimba, Salome Makamba ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum."Vijana wapambane kugombea nafasi husika lakini wasinunue kura kwani zinavunja heshima ya nchi na zinaliaibisha taifa kwani wakiingia kwa njia hiyo uongozi wao utakuwa wa kulipa madeni hivyo wafanye siasa safi za heshima na siyo za matusi,"alisema Ilunde.Aliwataka watoe hoja kwa kuweka utu mbele kwa kuijali jamii na wajue kuwa kuna kushinda na kushindwa na wakubali matokeo kwa kutokufanya fujo ambapo TAMISEMI na Tume Huru ya Uchaguzi watasimamia vyema vyema uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani.
Tuesday, August 13, 2024
WIZARA YA MAJI IMEJIPANGA MABWAWA YA MAJI NA TOPE SUMU YANAKIDHI VIGEZO.
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Wizara ya Maji kupitia Idara ya Rasilimali za Maji ina jukumu la kuhakikisha mabwawa ya maji na tope sumu yanakidhi vigezo vya usalama wa mabwawa kwa mujibu wa Sheria ya Rasilimali za Maji ili kuepusha madhara yatakayojitokeza katika jamii.
Hayo yamesemwa leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Maji uliopo Mtumba Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri, amesema Wizara ya Maji imeandaa mafunzo ya siku mbili katika kuhakikisha usalama wa mabwawa ya maji na tope sumu unaimarishwa.
Aidha Mhandisi Waziri amesema kuwa mafunzo yatahusisha watalaam kutoka wamiliki wa migodi kwa ajili ya usalama wa mabwawa ya tope sumu, wamiliki wa mabwawa makubwa ya maji, wataalam wa mabwawa waliosajiliwa na wataalam kutoka Serikalini.
Sambamba na hayo Mhandisi Waziri ameongeza kuwa mafunzo hayo yameandaliwa kwa kushirikiana na Tanzania Chamber of Mines na yatafanyika mkoani Mwanza .
TAKUKURU PWANI YAOKOA BILIONI 1.6
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 1.6 kutoka vyanzo mbalimbali vya Halmashauri ya Mji Kibaha.
Hayo yamesemwa na Naibu Kamanda wa Takukuru Mkoa huo Ally Haji wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha juu ya kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu.
Haji amesema kuwa walibaini hayo wakati wa ufuatiliaji wa ukusanyaji wa ushuru wa huduma kama mbalimbali kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili kwa kushindwa kuwajibika.
"Katika ufuatiliaji tuligundua kuwa baadhi ya watumishi wa Halmashauri kwenye kitengo cha ukusanyaji wa mapato watumishi kushindwa kufuata sheria, kanuni, na taratibu za ukusanyaji na kufanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1.6 zilizokuwa zinapotea,"amesema Haji.
Monday, August 12, 2024
VIJANA WAJA NA SERA MPYA
SERIKALI imezindua Sera mpya ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007 toleo la 2024, ambayo inakwenda kujibu changamoto mbalimbali za vijana na kutoa mwongozo wa kuanzishwa rasmi kwa Baraza la Taifa la Vijana.
Hayo yamebainishwa leo Agosti 12,2024 Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu,Mhe. Ridiwani Kikwete, wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya vijana kimataifa.
“Serikali imekwisha kamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Vijana ya mwaka 2007 na marekebisho yake imefanyiwa mwaka 2024 na leo hii tunakwenda kuizindua muda mfupi ujao.
“Ndugu washiriki changamoto nyingi zinazoelezwa kwa vijana zinatokana na ukweli kwamba yako baadhi ya maeneo hayana miongozo yake kupitia sera hii ya vijana ambayo tutaizundua leo nina hakika kabisa vilio vya vijana wengi vinakwenda kupataiwa ufumbuzi baada ya kupitishwa kwa sera hii”ameeleza.
Aidha, amesema kuwa sera hiyo inaeleza uelekeo na njia ambazo wanakwenda kuzitumia kwa pamoja ili kufikia malengo ambayo yanatatua matatizo waliyonayo vijana.
“Sera hii inakwenda kuanzisha baraza la taifa la vijana uanzishaji wa baraza hili la vijana unakwenda kuwa muarobani wa kutambua na kutatua changamoto nyingi za vijana.
“Vijana wamekosa maeneo ya kueleza changamoto zao vijana walikosa watu wa kuwasikiliza, vijana walikosa msukumo wa kufikisha changamoto zao na kuzitafutia majawabu kwa pamoja”amesema Mhe.Ridhiwan.
Amesema, ujio wa sera hiyo ya vijana na uudwaji wa baraza la taifa la vijana unaonesha wazi azma ya Rais Samia kujidhatiti na changamoto zote zinazo wakabili vijana zinapatiwa majibu.
Hata hivyo amesema kuwa sera hiyo pia inakwenda kutambua vijana katika sekta zote wanaofanya kazi katika maeneo hatarishi ikiwemo ya madini, maeneo ya uzalishaji mali ikiwemo mashambani na kwenye mifugo.
“Wapo vijana wanaofanya kazi za sanaa ikiwemo wabunifu, muziki, michezo, ubunifu na utungaji wa sanaa mbalimbali sera hii inakwenda katika maeneo hayo.
Pia ametoa wito kwa maafisa kazi kutambua kuwa nafasi zao siyo za kukaa ofisini wakisubiri vijana waje kulia na kueleza changamoto zao.
Kwa upande wake Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Mary Maganga,amesema katika kuadhimisha siku ya vijana, wameendesha kongamano la siku mbili lililokutanisha vijana zaidi ya 3,000 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania.
“Katika kongamano hilo, vijana wamechangia juu ya mada za Sera ya Maendeleo ya 2050, fursa za kidigitali, vijana na uchumi, afya ya akili na saikolojia ya vijana na kusisitiza kuwa serikali imechukua maoni ya vijana katika eneo la elimu, afya, ajira na uwezeshaji.”amesema Bi.Maganga
Naye Mwakilishi wa Vijana, Charles Ruben amempongeza Rais Samia kwa jitihada zake kuwainua na kuwasaidia vijana wa kitanzania na kuwa vijana wamepata elimu na ujuzi wa kazi unaofanya vijana kushiriki katika shughuli za kiuchumi na kuwapo ongezeko la vijana kwenye uongozi.
“Ajira za vijana zimeongezeka ambapo kuanzia mwaka 2023 hadi 2024 ajira 607675 zimezalishwa huku ajira 204,000 zikitokana na miradi ya kimkakati inayotekelezwa hapa nchini huku akitenga Sh bilioni 1.1 kwa ajili ya miradi ya jenga kesho iliyobora BBT ambayo inawalenga vijana.”amesema Ruben
Friday, August 9, 2024
SELF MICROFINANCE WATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Katika kuadhimisha kilele cha siku ya wakulima na wafugaji Nane Nane, Mfuko wa Fedha wa (SELF MICROFINANCE) ulio chini ya Wizara ya Fedha umewataka wananchi wote wanaojishughulisha na shuguli za Kilimo, Ufugaji na Uvuvi kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na mfuko huo ili kukuza na kuongeza uzalishaji.
Wito huo umetolewa na Bi. Linda Mshana ambaye ni meneja masoko na uhamasishaji kutoka mfuko wa SELF wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la SELF lililopo katika maonesho ya Kitaifa ya Nanenane Jijini Dodoma.
Bi. Linda amesema, Mfuko huo una vifurushi mbalimbali kwaajili ya Wakulima, Wavuvi na wafugaji hivyo amewahimiza kujitokeza kwa wingi na kukopa mikopo hiyo ambayo imewekwa maalumu kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi.
Aidha, Linda ameongeza kuwa mbali na Mikopo hiyo pia Mfuko wa Self unatoa Mikopo kwa taasisi ndogondogo za kifedha kwaajili ya kuwakopesha wakulima, wafugaji na wavuvi sambamba na mikopo mingine inayolenga kukuza uchumi wa watu mbalimbali.
"Self ina mikopo ya aina mbalimbali, tuna mkopo kwa ajili ya taasisi zinazokopesha, hivyo tunawakaribisha wakope na baadaye wawakopeshe wakulima, wafugaji na wavuvi,"amesema.
Linda amewakaribisha wananchi wote kutembelea banda lao lililopo katika maonesho hayo ili kupata elimu na kujua namna gani wanaweza kunufaika na Mikopo mbalimbali inayotolewa na Mfuko wa SELF.
Thursday, August 8, 2024
OFISI MAKAMU WA RAIS YAPONGEZWA UBUNIFU UTENGANISHAJI TAKA
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MWENYEKITI wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu ameipongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa utoaji wa elimu ya ubunifu wa mifumo ya utenganishaji taka ambao ni fursa ya ajira.
Mhe. Jaji Mwaimu ametoa pongezi hizo leo Jumatano Julai 7, 2024) wakati alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais katika maonesho ya Kitaifa ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma.
Ameeleza kuwa taka zinazozalishwa nchini kwa sasa zimekuwa ni fursa kutokana na malighafi hiyo kutumika katika shughuli za uzalishaji mali na hivyo kuchangia katika ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kuchochea maendeleo ya kaya, familia na jamii kwa ujumla.
“Taka ni fursa na pia ni vyanzo vya malighafi muhimu katika shughuli za uzalishaji kutoka. Nawapongeza kwa ubunifu wa utoaji wa elimu kuhusu fursa zilizopo katika taka kwani mbinu mbadala ya kukuza kipato cha jamii na kuhamasisha utunzaji wa mazingira” amesema Mhe. Jaji Mwaimu.
Aidha Jaji Mwaimu amewataka wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kutembelea Banda la Ofisi ya Makamu wa Rais na kujifunza teknolojia na bunifu mbalimbali zinazosaidia masuala ya uhifadhi wa mazingira kwani zipo fursa zinazoweza kusaidia ukuaji wa kipato katika ngazi ya kaya na jamii kwa ujumla.
Ameongeza kuwa taka ni fursa iliyojificha na hivyo elimu kuhusu fursa na manufaa yake wananchi wanapaswa kuitambua kwani sio kila kitu kinachotambulika kama takataka kinatakiwa kutupwa kwenye madampo, bali taka hizo zinaweza kutumika na kuwa fursa kujipatia kipato.
“Taka zinaweza kuwa fursa endapo zitachambuliwa kuanzia sehemu ya uzalishaji mpaka mtu wa mwisho anayetumia bidhaa husika, ili kuweza kuchangamkia fursa hiyo tunatakiwa kujua taka ambazo tunazalisha majumbani na namna zinavyotakiwa kutenganishwa” amesema Jaji Mwaimu.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sarah Kibonde amesema Ofisi hiyo imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali za kuemilisha umma kuhusu masuala ya Muungano na Mazingira ikiwemo maonesho, mikutano ya wadau na vyombo vya habari.
Ameongeza kuwa katika kupanua wigo wa elimu kwa umma kuhusu masuala ya Muungano na Mazingira kupitia maonesho hayo, Ofisi ya Makamu wa Rais imeanisha maeneo matano ya kimkakati kwa ajili ya kuwafikia wananchi na wadau mbalimbali wanaotembelea banda la ofisi hiyo.
Ametaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na masuala ya nishati safi ya kupikia, mabadiliko tabianchi, uchumi wa buluu, fursa zitokanazo na taka, biashara ya kaboni na elimu kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Kupitia maonesho tuna nyaraka mbalimbali ambazo ni vitabu ikiwemo Kitabu cha Miaka 60 ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), vipeperushi, majarida ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na wadau nk” amesema Kibonde.
Ofisi ya Makamu wa Rais imeungana na Wizara, Idara, Taasisi na Wakala za Serikali na sekta binafsi kushiriki maonesho ya kitaifa ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma kuanzia tarehe 1-8 Agosti, 2024.
Maonesho hayo yanaongozwa na kauli mbiu isemayo “Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.
DIB KULINDA AMANA ZA WATEJA
Bodi ya Bima ya Amana (DIB) ikiwa na jukumu la kusimamia amana za wateja zinapokuwa kwenye mabenki endapo benki ikifilisika inaweza kumlinda mteja aliyeweka amana zake asiweze kupata hasara.
Hayo yameelezwa na mwenyekiti wa bodi ya Amana (DIB) Emmanuel Tutuba wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la maonyesho ya nanenane Zuguni Jijini Dodoma huku akiwataka wananchi waliokuwa wateja wa benki zilizofilisika waweze kufika katika taasisi hiyo ili kuhakikiwa na kupewa stahiki zao.
Amesema DIB mpaka sasa imeongeza zaidi ya shilingi trilioni 1 ambazo wanaendelea kuwekeza sehemu mbalimbali ambazo fedha hizo ni za wateja endapo benki ikifilisika mteja aweze kupata gawio lake kulingana na alivyowekeza.
"Tangu kuanzishwa DIB ilipewa mtaji mwaka 1994 na benki kuu ya Taifa (BOT) walipewa kiasi cha shilingi bilioni1.5 kwa sasa wana atirioni 1.2.3 fedha hizo zinaendele kuongezeka kwa sababu wanaendelea kuwekeza sehemu mbalimbali fedha hizo zipo kwa ajiri ya kukinga amana za wateja hata kama bank ikitokea bahati mbaya ikafilisika kila aliyekuwa na account kwenye benki atalipwa kulingana na kiwango ambacho alichokuwa anaweza kulingana na kiwango cha asilimia atarejeshewa,"amesema Tutuba.
Pia ametoka wito kwa wateja wa benki FDME kama kuna mtu ajapewa mgawanyo wa asilimia 30 aweze kufika kwenye bodi ya bima ya Amana ili aweze kupatiwa utaratibu.
"Wametoa wito kwa wateja kwenye benki FDME kama kuna mtu ajapewa mgawanyo wa asilimia 30 cha awali aweze kufika taasisi hii ya bima ya amana ili aweze kupitia taratubu zote kujiludhisha Ili arejeshewa kiwango 30 Cha awali." Amesema Tutuba.
Aidha Tutuba hakusita kueleza mfano wa faida ya mfuko huo unaosimamiwa na DIB kupitia mfano wa zile benki ambazo zilizowahi kufilisika nchini.
Amewapongeza kusimamia shughuli zao za kusimamia amana za wateja na cha msingi DIB kazi yake ni kuweka na kuendelea kuwekeza bima ili kukinga viatarishi ambavyo vitajitokeza endapo benki itafilisika, pia kuna baadhi ya watu ambao benki zao zilifilisika mwanzano wanatakiwa wafiki DIB" Amesema Tutuba.
Wednesday, August 7, 2024
FILBERT BAYI WATAMBA KUFANYA VEMA FEASSA
BRELA YAZUIYA KUTAPELIWA KWA WATEJA
Na Wellu Mtaki,Dodoma.
Tuesday, August 6, 2024
MSONGO WA MAWAZO HUSABABISHA MAZIWA YA AKINAMAMA WANAONYONYESHA YASITOKE
IMEELEZWA kuwa moja ya sababu zinazosababisha maziwa ya akinamama wanaonyonyesha kushindwa kutoka ni msongo wa mawazo.
Aidha wanaume ambao wake zao wananyonyesha wameshsuriwa wasiwaudhi wake zao ili wasisababishe maziwa yashindwe kutoka na kushindwa kunyonyesha watoto wao.
TEAC IMELENGA KUSAIDIA MKULIMA NA MFUGAJI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma.
Mkuu wa Kanda ya kati ya Tume ya Nguvu za Atom Tanzania ( TEAC ) Machibya Anthony Matulanya amesema kuwa Tume imelenga kusaidia wakulima na wafugaji kupata mavuno makubwa ambayo yataongeza pato la uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja .
Hayo ameyasema Leo Tarehe 5 Agost 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika Banda la Tume ya Nguvu za Atom Tanzania Katika viwanja vya nanenane Zuguni jijini Dodoma huku akiwasihi wananchi kutembelea Banda ilo Ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuza na kuboresha kilimo na ufugaji.
Adha amesema kuwa Tume inajishughulisha na swala la uhamasishaji wa Matumizi ya Nuclear nchini ambayo inalenga kuhakikisha teknologia ya nuclear inakunza uchumi wa nchi.
"Tume ya nguvu za Atom Tanzania zinajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama ambapo wanalenga kuhakikisha kwamba teknologia ya Nuclear nchini inatumika vizuri na inakuza uchumi wa nchi." Amesema Matulanya
Pia meeleza kuwa teknologia ya nuclear imeweza kutumika kuangamiza wadudu aina ya Mbung'o ambao wanang'ata Mifugo na kusababusha Hali ya upungufu wa Maziwa kwa ng'ombe pamoja na kukosa nyama iliyo Bora.
"Kwa upande wamifugoTeknologia ya Nuclear imetumika imeangamiza wadudu aina ya Mbung'o , Mb'ung'o ni wadudu atali ambao wanang'ata Mifugo
Hawa wadudu waking'ata kwa mfano Ng'ombe wanamsababishia Hali ya upungufu wa Maziwa na pia uwezi kupata nyama nzuri" amesema Matulanya.
Mayulanya amesema kuwa zipo mbegu Bora za Mpunga ambazo zinatumika Tanzania bara na nzazibar ambazo zinauwezo Mkubwa wa kuimili ukame na ahitaji maji Mengi katika kuzalisha na unafanya mmea usivunjike .
"Pia kwa upande wa kilimo teknologia ya Nuclear imetumiaka huko nzazibar na bara, mbegu ya mpunga aina ya super DC ambayo inatumika Mbegu hizi ambazo zimeboreshwa uwezo Mkubwa wa kuimili ukame ambayo mbegu hiyo ukiilima aitaji maji Mengi Katika kutoa matunda yake" Amesema Matulanya
"Baada ya kuboreshwa mbengu hiyo imekuwa na stimilivu na yenye kutoa faida kubwa kwa mkulima pamoja na mmea kustaimili usivunjike na huo mpunga baada ya kuuvuna na kuukoboa unakuwa mtamu" Amesema Matulanya
Ikumbukwe kuwa Tume ya Atom Tanzania inajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama.
TEAC IMELENGA KUSAIDIA MKULIMA NA MFUGAJI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma.
Mkuu wa Kanda ya kati ya Tume ya Nguvu za Atom Tanzania ( TEAC ) Machibya Anthony Matulanya amesema kuwa Tume imelenga kusaidia wakulima na wafugaji kupata mavuno makubwa ambayo yataongeza pato la uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja.
Hayo ameyasema Leo Tarehe 5 Agost 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari Katika Banda la Tume ya Nguvu za Atom Tanzania Katika viwanja vya nanenane Zuguni jijini Dodoma huku akiwasihi wananchi kutembelea Banda ilo Ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuza na kuboresha kilimo na ufugaji.
Adha amesema kuwa Tume inajishughulisha na swala la uhamasishaji wa Matumizi ya Nuclear nchini ambayo inalenga kuhakikisha teknolojia ya nuclear inakunza uchumi wa nchi.
"Tume ya nguvu za Atom Tanzania zinajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama ambapo wanalenga kuhakikisha kwamba teknologia ya Nuclear nchini inatumika vizuri na inakuza uchumi wa nchi." Amesema Matulanya.
Pia meeleza kuwa teknologia ya nuclear imeweza kutumika kuangamiza wadudu aina ya Mbung'o ambao wanang'ata Mifugo na kusababusha Hali ya upungufu wa Maziwa kwa ng'ombe pamoja na kukosa nyama iliyo Bora.
"Kwa upande wamifugoTeknologia ya Nuclear imetumika imeangamiza wadudu aina ya Mbung'o , Mb'ung'o ni wadudu atali ambao wanang'ata Mifugo
Hawa wadudu waking'ata kwa mfano Ng'ombe wanamsababishia Hali ya upungufu wa Maziwa na pia uwezi kupata nyama nzuri" amesema Matulanya.
Mayulanya amesema kuwa zipo mbegu Bora za Mpunga ambazo zinatumika Tanzania bara na nzazibar ambazo zinauwezo Mkubwa wa kuimili ukame na ahitaji maji Mengi katika kuzalisha na unafanya mmea usivunjike .
"Pia kwa upande wa kilimo teknologia ya Nuclear imetumiaka huko nzazibar na bara, mbegu ya mpunga aina ya super DC ambayo inatumika Mbegu hizi ambazo zimeboreshwa uwezo Mkubwa wa kuimili ukame ambayo mbegu hiyo ukiilima aitaji maji Mengi Katika kutoa matunda yake" Amesema Matulanya
"Baada ya kuboreshwa mbengu hiyo imekuwa na stimilivu na yenye kutoa faida kubwa kwa mkulima pamoja na mmea kustaimili usivunjike na huo mpunga baada ya kuuvuna na kuukoboa unakuwa mtamu" Amesema Matulanya
Ikumbukwe kuwa Tume ya Atom Tanzania inajishughulisha na swala la uhamasishaji ya matumizi Nuclear nchini lakini kwa usalama.
Monday, August 5, 2024
BRELA KUANZA KUSAJILI WAKULIMA
Na Wellu Mtaki, Dodoma
OFISA Usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Gabriel Gilangay amesema wakala huo umejipanga kuanza kuwasajili Wakulima kwa kuwapa nembo ambayo itawatambulisha kibiashara.
Gilangay amesema hayo Jijini Dodoma kwenye maonesho ya Wakulima Nanenane wakati akizungumza na Waandishi wa habari na kueleza kuwa Wakala huo unashughulikia mambo mengi kwa wakulima nchini ikiwemo usajili wa Biashara.
Mbali na hayo amesema BRELA hutoa huduma hizo ili kuhakikisha biashara za kilimo zinakubalika kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri kuhusu jinsi ya kufuata taratibu za kisheria katika biashara ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kanuni za usajili, sheria za biashara, na masharti ya leseni.
Kwa upande mwingine Wakala huo hushughulikia Kampuni za Umma,Kampuni zinazoshiriki soko la hisa,Kampuni za Kibinafsi na Kampuni zinazomilikiwa na watu wachache.
TIMU ZA UMISSETA NA UMITASHUMTA MKOA WA PWANI ZAKABIDHI VIKOMBE
TIMU za Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) za Mkoa wa Pwani zimekabidhi makombe ilivyoshinda kwenye mashindano ambayo yaliyomalizika Mkoani Tabora hivi karibuni.
Sunday, August 4, 2024
YPC YAWATAKA VIJANA KUJITOKEZA KUWANIA NAFASI ZA UONGOZI
Thursday, August 1, 2024
DK BITEKO AMWAKILISHA RAIS MKUTANO MKUU (TLS)
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko leo Agosti 1, 2024 amemwakilisha Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Miaka 70 wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) unaofanyika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma.
Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Pindi Chana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Feleshi, pamoja na Wanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika.
Itakumbukwa kuwa TLS ilianzishwa mnamo mwaka 1954 ikiwa na mawakili takribani 141 wakiwa ni wakoloni hadi ilipofika mnamo Oktoba 31,1961 ilipopata wakili wa kwanza Mtanganyika.
Hadi sasa TLS ina jumla ya mawakili takribani 12,471 wanaofanya kazi za usaidizi wa kisheria katika taasisi mbalimbali za kisheria nchini.
MH.RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA TRENI YA KISASA (SGR)
Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam – Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam, leo 1 Agosti, 2024.
WAZIRI MKUU AFUNGUA MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 01, 2024 afungua maonesho ya Kimataifa ya Wakulima ya Nanenane ambayo kitaifa yanafanyika kwenye viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma,
Kauli mbiu ya Maonesho hayo ni Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.