Saturday, June 25, 2016

WAKANUSHA KUPAKA KINYESI NA KUVUNJA OFISI YA KATA

Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI wa Mtaa wa Machinjioni Loliondoa au Sagulasagula waliobomolewa nyumba zao na Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani kwa tuhuma za kujenga nyumba kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko wamekanusha kuapaka kinyesi na kuvunja vioo vya ofisi ya kata ya Maili Moja.

Akizungumza na waandishi wa habari moja ya wahanga wa tukio la bomoa bomoa hiyo iliyofanyika Juni 16 na 17 mwaka huu ambapo watu hao walifanya uharibifu huu siku moja baada ya bomobomoa hiyo huku jumla ya nyumba 18 zilibomolewa, Said Tekelo amesema kuwa wao hawahusiki na tukio hilo na wamesikitishwa na kitendo hicho.

Tekelo amesema kuwa kitendo hicho kimefanywa na watu ambao walikuwa na malengo yao na hawaungi mkono watu waliofanya uharibifu huo kwani ni tukio ambalo ni kinyume cha sheria na hakistahili kuunga mkono.

Amesema kuwa wao kama wahanga wa bomobomoa hiyo hawawezi kufanya hivyo kwa sababu bado wako katika kutafuta haki yao waliyoipoteza baada ya nyumba zao kubomolewa pasipo kupewa fidia yoyote hivyo wasingeweza kufanya uharibifu.

Aidha amesema kuwa vi vema vyombo vya kisheria vikafanya yake ili kubaini wale waliofanya hivyo na kuwachukulia hatua kazi za kisheria kwani hao ni wahalifu kama wahalifu wengine na hawahusiani na waliobomolewa nyumba zao.

Amebainisha kuwa suala lao liko mahakamani tangu zoezi la kubomolewa nyumba zao lilipofanyika na hawaungi mkono watu waliofanya hivyo na wanawalaani vikali watu hao ambao wamejificha kwenye mwamvuli wa uhalifu.


MWISHO

ZEGERENI KUJENGA SHULE YA MSINGI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha umefayatua matufali 2,500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa shule ya Msingi katika mtaa huo ambao unategemea mtaa wa Visiga kuwapeleka watoto wao umbali wa kilometa nane.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa zoezi la kuwapa zawadi wanafunzi wa darasa la saba ambao wamefanya vizuri na kuwa kwenye 10 bora mwenyekiti wa mtaa huo Rashid Likunja amesema kuwa wanatarajia kuanza ujenzi wa shule hiyo kuanzia Julai Mwaka huu ili ifikapo mwakani watoto wao waanze kusoma kwenye shule hiyo.

Likunja amesema kuwa fedha za kununulia kiwanja chenye ukubwa wa hekari sita zimetokana na mchango wa shilingi 5,000 kila kaya ambapo hatua ya ujenzi itaanza kwa kutumia tofaali hizo huku wakiwa na mifuko 12 ya simenti wakianza na madarasa mawili, ofisi na matundu manne ya vyoo.

Amesema kuwa kwa sasa wako kwenye harakati za kupata kibali cha ujenzi pamoja na ramani toka Halmashauri ya Mji ili waweze kuanza ujenzi huo na utawapunguzia watoto wao kwenda kusoma mbali pia huwabidi kuvuka barabara ya Morogoro ambapo ni hatari kwao kwani wengine ni wadogo sana.

Aidha amewataka wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili waweze kutekeleza azma yao ya ujenzi wa shule hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa watoto wanaotoka mtaa huo ambao wanafikia zaidi ya 200 wanaosoma madarasa mbalimbali kutoka mtaa huo ambao wanasoma shule jirani ya Visiga.


Mwisho.   

Thursday, June 23, 2016

MILIKINI MAENEO KIHALALI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI-RC

Na John Gagarini, Kibaha

MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wakazi wa mkoa huo kufuta taratibu na sheria za kumiliki ardhi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo kwa sasa imeshamiri na inaweza kuhatarisha amani.

Aidha amesema kuwa mkoa hautasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu ambao wanavamia maeneo ya watu na kuyauza kama wanavyofanya baadhi ya watu kwani ni kinyume cha sheria na watachukuliwa hatua kali ili waachane na tabia hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na baadhi wananchi kutoka wilaya ya Mkuranga Ndikilo alisema kuwa kumekuwa na migogoro mingi ambayo imesababisha wananchi kutokuelewana wao kwa wao.

“Moja ya mfano ni Kijiji cha Kazole Kitongoji cha Magodani Kata ya Vikindu wilaya ya Mkuranga kuna baadhi ya watu wanajifanya kamati ya ardhi ya Kijiji hicho kulivamia shamba la kampuni ya Soap Allied Industry ambalo lina ukubwa wa hekari 1,750 likiwa na hati ya umiliki 271 ambayo iliipata tangu mwaka 1988 ambalo lilitengwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,”alisema Ndikilo.

Ndikilo alisema kuwa kamati hiyo ambayo imekuwa ikiuza viwanja kwenye eneo hilo inafanya makosa kwa kuwauzia watu kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria kwani eneo hilo lina mmiliki halali ambaye anamiliki kisheria.

“Kama haitoshi watu hao walikwenda kwenye vyombo vya sheria lakini walishindwa na kuambiwa kuwa eneo hilo ni mali ya mtu hivyo hawapaswi kuingie kwenye eneo hilo lakini wanakamati hao bado wanaendelea kuwauzia watu na kujipatia mamilioni ambayo yote yanaingia mifukoni mwao na wamejinufaisha kupitia shamba hilo lakini wanawaibia watu kwani mmiliki mwenyewe yupo,” alisema Ndikilo.

Aidha alisema kuwa suala la shamba hilo linachukuliwa kisiasa lakini mwisho wa siku linaweza kusababisha uvunjifu wa amani kwani watu waliotoa fedha zao watakapoambiwa waondoke watadai fedha zao na hakuna mtu wa kuwarejeshea hivyo kuleta migogoro ambayo haitakiwi.

Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Bonaventura Mushongi alisema kuwa ni vema watu wakafuata sheria bila ya shuruti kwani eneo hilo limeshatolewa maamuzi baada ya watu waliouziwa kwenda mahakamani na kuonekana kuwa kampuni hiyo ndiyo yenye uhalali wa kumiliki eneo hilo hivyo watu kuingia humo ni kuvunja sheria na wanaweza kukamatwa na polisi

Mushongi alisema kuwa watu hawapaswi kuingia kwenye eneo hilo ambapo hivi karibuni zaidi ya watu 20 waliingia kwenye shamba na kukamatwa na kwa kuwa hati ya umiliki bado haijatenguliwa watu wasiingie na kama wanaona wana haki ni vema wakaenda mahakama za juu kudai haki yao lakini si kulivamia.


Mwisho.       


KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho

Monday, June 20, 2016

MWENYEKITI WA MTAA AWAZAWADIA WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha mkoani Pwani umewapa zawadi mbalimbali wanafunzi wa darasa la saba waliofanya vizuri kwenye mitihani yao ya katikati ya muhula.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi hao Rashid Likunja alisema kuwa ameweka utartibu huo kwa wanafunzi wa darasa la saba ili kuwapa hamasa ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza darasa la saba.

Likunja alisema kuwa zawadi anazotoa ni mfuko wake aliouanzisha kwa ajili ya kuwapa hamasa ya wanafunzi wa mtaa huo kusoma kwa bidii na kuongeza ufaulu.

“Unajua mtaa huu hakuna shule ya msingi ambapo wanafunzi huwabidi kwenda kusoma mtaa jirani wa Visiga ambapo wengine wanatembea kilometa nane kila siku hivyo kuwakatisha tamaa watoto hivyo kutotilia makazo elimu,” alisema Likunja.
Aidha alisema kuwa kabla ya kuanza utaratibu huo wanafunzi wa mtaa huo walikuwa wakishika nafasi za nyuma kuanzia 35 na kushuka chini lakini a kwa sasa wameanza kuhamasika na wameweza kuingia kwenye 10 zaidi ya wanafunzi watano.

“Nimeanzisha mfuko wa kuwasaidia wanafunzi wa mtaa wetu naomba na wadau wengine wajitokeze kusaidia ili zawadi ziwe kubwa kwani nianazotoa ni ndogo lakini naamini wadau zaidi watajitokeza kuniunga mkono juu ya suala la elimu ambalo nimelipa kipaumbele cha kwanza,” alisema Likunja.

Moja ya wazazi ambao mwanae kapewa zawadi baada ya kuwa moja ya wanafunzi walioingia kwenye 10 bora Mwajabu Suleiman alisema kuwa mwenyekiti wao amewapa changamoto kubwa ya kuwahamasisha wanafunzi kusoma kwa bidii.

Suleiman alisema kuwa watamuunga mkono mwenyekiti wao kwa kuwahamasisha watoto wao kusoma kwa bidii ili wawe chachu ya wanafunzi wenzao wanaoanza madarasa ya awali.


Mwisho.    

SIDO YATUMIA DOLA MILIONI 2

Na John Gagarini, Kibaha

SHIRIKA la Kuendeleza  Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kwa kushirikiana na wafadhili wake limetumia kiasi cha dola milioni mbili za Kimarekani kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uzalishaji bidha za vyakula zisizo na madhara kwa wajasiriamali zaidi ya 700.

Mratibu wa mafunzo hayo Happines Mchomvu alisema kuwa mafunzo hayo ambayo yametolewa kwa kipindi cha miaka miwili kwa lengo la kuhakikisha bidhaa wanazozalisha zinakuwa hazina madhara kwa watumiaji zinakuwa na usalama.

Mchomvu alisema kuwa mbali ya kuwa na usalama pia zinakuwa na viwango vya wa ubora wa kimataifa ili viweze kuuzwa sehemu yoyote ile duniani.

“Mafunzo hayo yalikuwa na malengo ya kuboresha bidhaa za maembe, viungo na asali ambapo wameweza kuwajengea uwezo wajasiriamali hao kutoka mikoa ya Tabora, Singida, Shinyanga, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam,” alisema Mchomvu.

Aidha alisema lengo ni kuhakikisha wajasiriamali kote nchini kuanzia ngazi ya mikoa hadi kwenye mitaa wanazalisha bidhaa zenye ubora na viwango kwa lengo la kuwa na soko la uhakikka la ndani na nje ya nchi ambapo bidhaa za Tanzania zinapendwa kutokana na uhalisia wake.

Kwa upande wake ofisa udhibiti wa ubora kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Magdalena Sademaki alisema kuwa kupitia mafunzo hayo wajasiriamali hao wameweza kutengeneza mifumo yao kimataifa kwa kupambana na vihatarishi ili visiweze kuingia kwenye vyakula.
Sademaki alisema kuwa katika kuhakikisha wajasiriamali hao wanatengeneza bidhaa zenye viwango wanashirikiana na SIDO kuwatambua ili waweze kufikia viwango vya uzalishaji wa bidhaa bora ili ziendane na viwango vya kimataifa.

Na mmoja wa wajasiriamli ambaye amehudhuria mafunzo hayo Zaloki Mohamed ameishukuru SIDO kwa kuwapatia elimu juu ya viwango vya bidhaa  wanazozalisha kwa kuzingatia  utaratibu wa viwango vya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO).

Mohamed  ameiomba serikali iwapunguzie tozo zinazotozwa kwa wajasiriamali ili wapate hati ya viwango ya bidhaa wanazozalisha na kuweza kufikia malengo  ya Tanzania ya kuwa na viwanda.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ufadhili wa Shirika la Biashara la Kimataifa (ITC) kupitia mpango wa kuendesha biashara wa shirika la World Trade Organisation (WTO) kwa kushirikiana na SIDO.

Mwisho. 





 

   




Saturday, June 18, 2016

WAVUNJUA VIOO VYA MADIRISHA WAPAKA KINYESI OFISI YA KATA

BOMOABOMOA YALIZA WENGI KIBAHA

MIGOGORO YA NDOA ISIWANYIME HAKI ZA MSINGI WATOTO

Tuesday, June 14, 2016

WATATU WASHIKILIWA KWA MAUAJI YA DEREVA WA NOAH

Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya dereva wa gari la abiria aina ya Toyota Noah Mohamed Ramadhan (21) mkazi wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa Polisi mkoani humo Bonaventura Mushongi alisema kuwa watu hao walimkodisha dereva huyo.
Mushongi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 13 mwaka huu majira ya saa 19:45 usiku eneo la Vigwaza Tarafa ya Chalinze wilaya ya Bagamoyo.
“Watu hao walimuua dereva huyo kwa kumkaba shingoni kisha kupora gari hilo lenye namba za usajili T 119 DDM rangi nyeupe lililokuwa likitumiwa na marehemu baada ya kumkodi wakimataka awapeleke Kanisa la Pentekoste Vigwaza,” alisema Mushongi.
Alisema kuwa watu hao kabla ya kumuua marehemu walimkaba wakiwa njiani ambapo alipiga kelele kuomba msaada na madereva bodaboda walizisikia na kuamua kufuatilia gari hilo barabara ya vumbi kwenye njia kuu ya umeme wa Tanesco.
“Watu wale walipoona taa za bodaboda waliamua kusimama na kutoka ndani ya gari na kuanza kukimbia kutokomea porini lakini mmoja wao alikamatwa palepale na walipoangalia ndani walikuta mwili wa marehemu ukiwa umewekwa kiti cha nyuma kwa lengo la kwenda kuutupa mwili huo porini ili kuondoka na gari hilo,” alisema Mushongi.
Aidha alisema kuwa juhudi za wananchi, dereva bodaboda na polisi zilifanikisha kukamatwa watuhumiwa wawili ambao majina ya watuhumiwa hao yamehifadhiwa ili kutoharibu upelelezi kwani watu hao ni mtandao wa majambazi ambao wengine wako Jijini Dar es Salaam.
Alibainisha kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Tumbi kusubiri ndugu na uchunguzi wa daktari kwa ajili ya mazishi.
Aliwataka madereva wa vyombo vya moto hasa wale wanaofanya biashara za usafirishaji nyakati za usiku kuwa makini ili kujiepusha na matukio kama hayo ya wizi.
Mwisho.         

    

Thursday, June 9, 2016

RC ATAKA MKATABA WA UWEKEZAJI KUPITIWA UPYA

Na John Gagarini, Mafia
MKUU wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo ametaka kupitiwa upya mkataba wa kuuziwa mwekezaji eneo la Magofu ya Chole wilaya ya Mafia mkoani Pwani ambapo kampuni ya Chole Mjini Conservation and Development Ltd imemilikishwa ambapo eneo hilo kuna gereza walilokuwa wanafungwa watumwa enzi za ukoloni wakati wa Utawala wa Wajerumani.
Aidha ameunda tume ya kufuatilia undani wa mkataba huo na amezuia marekebisho yaliyokuwa yanafanywa na kampuni hiyo kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi pale ufumbuzi wa kujua namna mkataba huo ulivyoingiwa baina ya Kijiji cha Chole na mwekezaji huyo kama umezingatia taratibu.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chole Mjini kata ya Jibondo kwenye mkutano wa hadhara Ndikilo alisema kuwa mkoa hauna nia mbaya na mwekezaji huyo ambaye amepewa hati miliki ya eneo hilo kwa kipindi cha miaka 33.
Ndikilo alisema kuwa eneo hilo ambalo lina kumbukumbu mbalimbali ambalo liko jirani na Bahari ya Hindi lilikuwa likitumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na soko la Watumwa pamoja na gereza lina ukubwa wa hekta 3.7 ambapo eneo hilo liko chini ya Wizara ya maliasili na Utalii Idara ya Malikale.
“Mkataba huo ambao ulisainiwa mwaka 2007 shamba namba 2031 baina ya mwekezaji  Dk Jean de Villiers na Kijiji hicho ambapo mwenyekiti wa Kijiji hicho Maburuki Sadiki alisaini kwa niaba ya Kijiji na kushuhudiwa na mkuu wa wilaya wakati ule Manzie Mangochi pasipo kuishirikisha Halmashauri ya wilaya ambayo haipati mapato yoyote kutokana na uwekezaji huo licha ya kutoa huduma za kijamii kwa wakazi wa Kijiji cha Chole” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo amemtaka mwekezaji huyo kusimamisha ukarabati na kuunda tume ya kufanya uchunguzi na itatoa majibu baada ya mwezi mmoja ili kujiridhisha na kumilikishwa eneo hilo mtu binafsi eneo la serikali la kihistoria na kujengwa hoteli ya kitalii kwa kukarabati jengo la zamani.
Alibainisha kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii ilituma barua ambayo iliyosainiwa na John Kimaro kwa niaba ya katibu mkuu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kuhirikiana na mwekezaji na kusema kuwa sheria ya Mambo ya Kale ya mwaka 1964 na marekebisho yake ya mwaka 1979 na sera ya Malikale ya mwaka 2008 inasema Malikale au Magofu yanaweza kumilikiwa na mtu binafs, taasisi na serikali.
Barua hiyo inaendelea kusema kuwa jukumu la serikali (Idara ya Mambo ya Kale) ni kuhakikisha kuwa mmiliki hatabomoa au kufanya chochote katika magofu hayo kinyume cha sheria.
Akitoa maelezo juu ya umiliki wake mkurugenzi wa Chole Mjini Conservation and Development Company Ltd Anne De Villiers amesema kuwa kampuni hiyo iliingia Mafia na kukuta hali ya majengo hayo ya kale yakiwa kwenye hali mbaya ndipo walianza mchakato wa kuyakarabati.
Dk Villiers alisema kuwa lengo la kuchukua eneo hilo ni kuhakikisha uasili wa mahali hapo haupotei kwa kuyafanyia ukarabati magofu hayo ambapo moja lilibaki ukuta mmoja na kutumia fedha nyingi kwa ajili ya ukarabati huo.
Naye mkuu wa wilaya ya Mafia Dk Nasoro Hamid alisema kuwa serikali haishirikishwi jambo lolote wala haijui ni watalii wangapi wanaoingia hapo wala mapato yanayopatikana kwenye eneo hilo.
Dk Hamid amesema kuwa Kijiji cha Chole ndicho kiliingia mkataba na mwekezaji huyo ambapo hugawana asilimia kutokana na watalii wanaoingia kwenye eneo hilo la makumbusho lakini tatizo haijulikani kinachopatikana hapo ni kiasi gani katika mgawanyo huo wa mapato.
Awali baadhi ya wanakijiji wakizungumzia suala hilo wakiongozwa na Ally Sikubali na Hemed Ally walisema kuwa moja ya changamoto iliyokuwepo ni mkataba Kiswahili unasema kuwa endapo kutakuwa na kutoeleweka mkataba wa Kiingereza ndiyo utakaotumika.
Waliomba mkataba huo uangaliwe upya na kufanya marekebisho ili kila upande unufaike kwani kwa sasa inaonekana kuwa pande nyingine hazinufaiki na mkataba huo.     
Mwisho.
   

 
   


WATAKA TAARIFA KUHUSU ENEO LA UWEKEZAJI BAADA YA MRADI WA MIWA KUFUTWA

Na John Gagarini, Bagamoyo
HALMASHAURI ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani imetakiwa kutoa taarifa rasmi kwenye vijiji vilivyokuwa kwenye mradi wa kilimo cha miwa chini ya kampuni ya Eco Energy uliosimamishwa na serikali ili eneo hilo lisije kuchukuliwa na mtu mwingine ili hali wananchi hao hawajalipwa fidia.
Mradi huo ulisimamishwa kupitia majibu ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa anajibu swali la kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe aliyetaka kujua ni kwanini serikali imeshindwa kuweka jitihada za makusudi ili mradi huo ukamilike ambao ulibainika kuwa ungetumia maji mengi ya Mto Wami na kuathiri usatawi wa wanyama kwenye Mbuga ya Saadani.
Akizungumza na waandishi wa Habari mjini Bagamoyo katibu wa kamati ya ardhi ya Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Mkombozi Bakari Salum alisema kuwa     kwa kuwa kauli ya Waziri Mkuu ni agizo ni vema Halmashauri ingetoa tangazo rasmi kwa wananchi husika.
“Kwa kuwa wakati anakuja mwekezaji kuchukua maeneo ya wananchi kwa ajili ya mradi huo kulikuwa na taarifa rasmi na wananchi walitoa maeneo yao kwa ajili ya kilimo hicho cha miwa ambacho baadaye kungejengwa kiwanda kwa ajili ya kuzalisha sukari hivyo baada ya kushindikana wangewajulisha wananchi,” alisema Salum
Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Jackson Mkango alisema kuwa eneo ambalo lilichukuliwa na mwekezaji ni hekari zaidi ya hekta 22,000 wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya kuwa tathmini kufanyika mwaka 2011 hadi leo hawajalipwa.
Mkango alisema kuwa sheria inasema kuwa tathmini ikifanyika walengwa wanapaswa kulipwa ndani ya kipindi cha miezi sita lakini sasa imepita miaka mitano sasa.
“Tunaiomba Halmashauri kutoa tamko juu ya ardhi hiyo ya wananchi ambayo toka imechukuliwa wananchi hawakufanya chochote licha ya kuwa eneo hilo walikuwa wakitegemea kwa ajili ya kilimo na hawajui hatma yao kwani walitegemea wangelipwa fidia,” alisema Mkango.
Vijiji vilivyokuwa kwenye mpango huo ni Razaba, Matipwili, Kitame, Fukayosi, Makaani na Gongo ambapo kuna jumla ya wananchi zaidi ya 700 ambao walikuwa wakiishi kwenye maeneo hayo yaliyoingizwa kwenye mradi huo ambao ulikuwa na lengo la kukabiliana na upungufu wa sukari hapa nchini.

Mwisho.