KATIKA kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limewataka Watanzania kutumia Mkaa wa Rafiki Briquettes.
Thursday, December 19, 2024
STAMICO YATAKA WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA NISHATI SAFI NA SALAMA YA MKAA WA RAFIKI BRIQUETTES
KATIKA kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limewataka Watanzania kutumia Mkaa wa Rafiki Briquettes.
TAASISI YA ANJITA YATAKA USHIRIKIANO KUKABILIANA NA UKATILI WA KIJINSIA
Wednesday, December 18, 2024
KINGLION KUTOA AJIRA
KIWANDA cha kuzalisha malighafi zitumikazo kwenye uzalishaji vyuma na mabati na usambazaji wa pikipiki cha Kinglion kinatarajia kutoa ajira kwa watu 1,500 ajira za kudumu na ajira za muda zaidi ya 5,000.
MLEZI WA KAMATI YA USALAMA BARABARANI ACP MORCASE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI
Mlezi wa Kamati ya usalama barabarani Mkoa wa Pwani, Kamishina Msaidizi wa Polisi Salim Morcase Disemba 17 amekiongoza kikao cha kamati ya usalama barabarani ambacho kimejadili maswala mbalimbali ikiwemo kuondoa msongamano wa foleni kwenye barabara kuu za Mkoa wa Pwani na kuweka mikakati ya pamoja ya kumaliza foleni hizo ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa madereva watakaobainika kupandisha nauli za mabasi kwenye kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka pamoja na madereva wanaokaidi kutii Sheria za usalama barabarani kwa watumiaji wengine wa barabara.
Saturday, December 14, 2024
VITENDO VYA UKATILI PWANI VYAPUNGUA
CATHERINE MWENYEKITI MTAA WA SOFU NA MKAKATI WA KUJENGA OFISI SERIKALI YA MTAA.
Lyimo akizungumza na mwandishi wa habari hizi amesema kuwa hilo ndiyo jambo ambalo ni kipaumbele chake mara baada ya kuchguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mita uliofanyika hivi karibuni na yeye kushinda nafasi hiyo.
Amesema kuwa eneo tayari wanalo wanachofanya ni kuwaandikia wadau wa maendeleo kwenye mtaa huo kwa kushirikiana na wananchi kufanya ujenzi huo ambao ni ndoto yake kuhakikisha mkakati wa kuwa na ofisi unafanikiwa.
“Mpango mkakati wa mtaa kwa sasa ni kuwa na ofisi yake badala ya kutumia ofisi za watu wengine tunataka tuwe na ofisi yetu wenyewe ili tufanye kazi kwa uhuru badala ya kutegemea wengine kwani kutumia ofisi za watu wengine kuna changamoto zake,”amesema Lyimo.
Aidha amesema kuwa anamatumaini ofisi itajengwa kutokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wananchi na wadau wa maendeleo kwani anaamini ushirikiano huo utafanikisha kupatikana kwa ofisi ya mtaa huo.
“Nataka kwa kushirikiana wananchi na wadau kuhakikisha tunaacha alama ya uongozi kwa kujenga ofisi yetu kwani tukiwa na ofisi yetu tutakuwa na uhuru na tutajenga kutokana na mahitaji ya mtaa wetu ambapo itakuwa na vyumba kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi,”amesema Lyimo.
Amebainisha kuwa jambo lingine ambalo atahakikisha linafanyika ni kuwagawia wananchi eneo la kufanyiabiashara kwa ananchi wa mtaa huo ili waweze kupata huduma ya soko karibu kwani wanataka liwe soko dogo ili kuwaongezea wananchi kipato na kutoa huduma.
“Tunahitaji tuwe na eneo ambalo litakuwa kama soko ambapo wananchi watauza bidhaa zao badala ya kwenda mbali kufuata mahitaji yao nyumbani tunataka wapate hapa jirani na pia itakuwa ni sehemu ya kujiongezea kipato,”amesema Lyimo.
Lyimo alifanikiwa kushinda nafasi hiyo baada ya kumshinda aliyekuwa mwenyekiti wa Mtaa huo Lazaro Joseph ambaye aliongoza kwa vipindi viwili vya miaka 10 huku yeye akiwa ni mjumbe wa serikali ya mtaa huo ambapo alishindwa kwenye nasafi hiyo na mtangulizi wake mwaka 2019 na alikuwa ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Kata ya Sofu na Mjumbe wa mtaa.
Friday, December 13, 2024
MBONI MWANAMKE WA SHOKA AWEKA MIKAKATI YA UJENZI WA MATUNDU YA VYOO VYA SEKONDARI BAMBA
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Mwenyekiti wa Mtaa huo Mboni Mkomwa amesema kuwa shule hiyo shule hiyo ina madarasa manne yamekamilika isipokuwa wana mahitaji ya matundu nane ili ikamilke na kuanza masomo kwa wanafunzi wanaotoka mtaa huo.
Mkomwa amesema kuwa kwa sasa anaandaa mpango wa kukutana na wadau wa maendeleo wa mtaa huo ili kufanya harambee ya kuchangia kukamilisha ujenzi wa vyoo hivyo kabla ya mwaka huu kwisha ili hadi Januari viwe vimekamilika na wanafunzi kuanza kusoma.
“Wanafunzi wanaotoka kwenye mtaa huu wanasoma shule za sekondari za Mwambisi na Miembe Saba ambako ni mbali hivyo baada ya kuona changamoto hiyo tulikaa na wananchi na kukubaliana kujenga madarasa ambapo manne yamekamilika kilichobaki ni vyoo matundu nane yakikamilika hayo shule inaanza,”amesema Mkomwa.
Amesema kuwa wanaishukuru serikali ambayo ilitoa kiasi cha shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi huo pia wananchi nao walichangia kila kaya 2,000 na kufanikisha ujenzi huo kufikia hapo na kubaki hatua ndogo ili ianze.
“Tuliomba tena fedha ila walituambia kuwa wasubiri hadi kipindi cha bajeti ambapo malengo yetu hayatafikia kwani bajeti ni katikati ya mwaka ambapo mwanzo wa mwaka tunataka wanafunzi wanaotoka kwenye mtaa wetu waanze kusoma hapo pia itasaidia maeneo ya mitaa jirani ambao nao watanufaika,”amesema Mkomwa.
Aidha amesema kuwa changamoto nyingine ambayo iko kwenye mipango yake katika kuitatua ni baadhi ya wakazi wa mtaa wake wapatao 23 hawana huduma ya maji kabisa hali ambayo inawasababisha kupata shida ya kupata maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kawaida.
“Wakazi hao waliandika barua baada ya kukaa kikao lakini wakifika Dawasa wanaambia watoe milioni mbili au wasubiri mradi upite maeneo yao jambo ambalo kwao bado ni mtihani na wanahitaji bomba kubwa la nchi sita ili wananchi waweze kuvuta maji kwa urahisi ambapo kwa sasa wanapotaka kuvuta maji kwa majirani huwabidi kuwalipa na kuilipa Daawasa hivyo kujikuta wakilipa mara mbili,”amesema Mkomwa.
Mkomwa alishinda kwenye uchaguzi wa wenyeviti uliofanyika hivi karibuni na alichaguliwa akiwa anatoka kuwa mjumbe wa mtaa huo kwa kipindi cha miaka mitano pia alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) tawi la Bamba ambapo mtaa huo una jumla ya wananchi 7,546 yeye ni mjane akiwa na watoto watatu na alifiwa na mume wake mwaka 2015 na ni mjasiriamali.