Monday, August 5, 2024

BRELA KUANZA KUSAJILI WAKULIMA

Na Wellu Mtaki, Dodoma

OFISA Usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Gabriel Gilangay amesema wakala huo umejipanga kuanza kuwasajili  Wakulima kwa kuwapa nembo ambayo itawatambulisha kibiashara. 

Gilangay amesema hayo Jijini Dodoma kwenye maonesho ya Wakulima Nanenane wakati akizungumza na Waandishi wa habari na kueleza kuwa Wakala huo unashughulikia mambo mengi  kwa wakulima nchini ikiwemo usajili wa Biashara. 

Mbali na hayo amesema  BRELA hutoa huduma hizo ili kuhakikisha  biashara za kilimo zinakubalika kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri kuhusu jinsi ya kufuata taratibu za kisheria katika biashara ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kanuni za usajili, sheria za biashara, na masharti ya leseni.

Kwa upande mwingine Wakala huo hushughulikia Kampuni za Umma,Kampuni zinazoshiriki soko la hisa,Kampuni za Kibinafsi na Kampuni zinazomilikiwa na watu wachache.

TIMU ZA UMISSETA NA UMITASHUMTA MKOA WA PWANI ZAKABIDHI VIKOMBE






TIMU za Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) za Mkoa wa Pwani zimekabidhi makombe ilivyoshinda kwenye mashindano ambayo yaliyomalizika Mkoani Tabora hivi karibuni.

Mchatta akipokea vikombe na tuzo na kuwapongeza wachezaji hao ofisini kwake Mjini Kibaha ambapo timu za riadha zilifanya vizuri kwenye michezo ya riadha na kutupa mkuki kwenye michezo hiyo.

Amesema kuwa wachezaji hao wameuletea sifa mkoa wa Pwani na hiyo imetokana na kutumia vyema vipaji vyao na kuwa na nidhamu na kuzingatia yale waliyofundishwa na walimu wao.

"Nimeambiwa wachezaji tisa watashiriki mashindano ya sekondari kwa nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika hivi karibuni nchini Uganda nawasihi mlinde viwango vyenu,"amesema Mchatta.

Aidha amesema kuwa wanariadha hao waige mfano wa mchezaji wa riadha Steven Akwari ambaye licha ya kuumia lakini alikimbia na kumaliza mbio licha ya maumivu makali.

Naye Mkurugenzi wa Filbert Bayi Elizabeth Mjema amesema kuwa shule inaomba kusaidiwa baadhi ya mahitaji ikiwa ni pamoja na lishe, maji na matunda.

Mjema amesema kuwa inawagharamia baadhi ya wanafunzi wenye vipaji ambao wazazi wao hawana uwezo ambapo lengo la Filbert Bayi ni kutaka wanariadha kufanya makubwa kwenye mchezo huo.

 Kwa upande wake mwalimu wa riadha wa timu za Filbert Bayi Ally Nyonyi amesema kuwa timu hiyo inafanya vizuri kutokana na kuwa na maandalizi mazuri na nidhamu.

Nyonyi amesema kuwa wao ni mabingwa kwa miaka mitatu mfululizo kwenye mashindano ya Umisseta na Umitashumta Taifa hiyo inatokana na kuwa na mazingira rafiki ya kufanyia michezo ambapo wanakuwa na muda mwingi wa kufanya mazoezi baada ya masomo.

Wakielezea jinsi walivyojiandaa na mashindano hayo huko Uganda wachezaji hao wamesema kuwa wamejiandaa vya kutosha na wanaamini watailetea nchi ushindi.

Sunday, August 4, 2024

YPC YAWATAKA VIJANA KUJITOKEZA KUWANIA NAFASI ZA UONGOZI

VIJANA wa kike na kiume wametakiwa kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Vijana (YPC) ya Kibaha Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na Habarileo ofisini kwake.

Ilunde alisema kuwa wameanzisha mradi uitwao (K-Vote) unaohamasisha ushiriki wa vijana kwenye masuala ya umma, elimu ya mpiga kura, uraia, kuwasaidia na kuwaelimisha vijana wanaotaka kuwania nafasi za uongozi kwenye chaguzi hizo.

"Tume Huru ya Uchaguzi inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya vijana milioni tano na wale ambao hawakuwahi kupiga kura miaka ya nyuma tunawasihi wajitikeze kuhakiki taarifa zao itakapofika muda wa kufanya hivyo ili waweze kushiriki kwenye uchaguzi,"alisema Ilunde.

Alisema vijana wanapaswa kushiriki zoezi hilo ambalo ni muhimu sana kwani wasipojiandikisha au kuboresha taarifa zao watakuwa watazamaji na hawataruhusiwa kupiga kura.

"Idadi ya vijana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi serikali za mitaa mwaka 2004 na uchaguzi mkuu mwaka 2005 ilikuwa ni asilimia 8 tu na mwaka 2015 iliongezeka na kufikia asilimia 50 na mwaka huu na mwakani itaongezeka,"alisema Ilunde.

Aidha alisema kuwa baadhi ya vijana hao walichaguliwa kwenye nafasi za uongozi ikiwa ni pamoja na ubunge, udiwani, wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa.

"Tuna mfano wa Dk Zainab Katimba ni Naibu Waziri na mbunge Salome Makamba walifanya vizuri na pia kuachana na dhana kuwa uchaguzi mtaji ni fedha bali ni watu, nidhamu, uchapakazi, kujali watu,"alisema Ilunde.

Aliwataka vijana kutonunua kura kwani zinavunja heshima na zinaaibisha Taifa na uongozi unakuwa wa kulipa madeni pia wafanye siasa za heshima bali ziwe za hoja na kuweka utu mbele na kutofanya vurugu wanaposhindwa na waijali jamii.


Thursday, August 1, 2024

DK BITEKO AMWAKILISHA RAIS MKUTANO MKUU (TLS)

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko leo Agosti 1, 2024 amemwakilisha Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Miaka 70 wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) unaofanyika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma. 

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Pindi Chana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Feleshi, pamoja na Wanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika. 

Itakumbukwa kuwa TLS ilianzishwa mnamo mwaka 1954 ikiwa na mawakili takribani 141 wakiwa ni wakoloni hadi ilipofika mnamo Oktoba 31,1961 ilipopata wakili wa kwanza Mtanganyika.

Hadi sasa TLS ina jumla ya mawakili takribani 12,471 wanaofanya kazi za usaidizi wa kisheria katika taasisi mbalimbali za kisheria nchini.

MH.RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA TRENI YA KISASA (SGR)



Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam – Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam, leo 1 Agosti, 2024.

WAZIRI MKUU AFUNGUA MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 01, 2024 afungua maonesho ya Kimataifa ya Wakulima ya Nanenane ambayo kitaifa yanafanyika  kwenye viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma,

Kauli mbiu ya Maonesho hayo ni Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Saturday, July 27, 2024

RIZIWANI KIKWETE NDANI YA BARAZA LA MADIWANI UCHAGUZI MAKAMU MWENYEKITI HALMASHAURI YA CHALINZE

Nimeshiriki kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua diwani atakayegombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze kilichofanyika Chalinze ,mapema leo.#KaziInaendelea