Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yatafunguliwa Desemba 17 na yatafanyika kwenye viwanja vya iliyokuwa stendi ya zamani ya Maili Moja Kibaha.
"Maonyesho hayo ni ya nne kufanyika ambapo kwa mara ya kwanza yalifanyika mwaka 2018, 2019, 2022 na mwaka huu ambapo watu watatoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi,"amesema Kunenge.
Amesema kuwa wakati wa maonyesho watu watakaohudhuria watapata fursa za kujifunza, kuona fursa zilizopo, kuona teknolojia gani zinatumika na kupata ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili katika Biashara na kujipatia bidhaa.
Ameongeza kuwa mkoa umejipanga vizuri hasa ikizingatiwa kuwa Mkoa una viwanda 1,553 na tangu Rais aingie madarakani viwanda vikubwa ni 78.
No comments:
Post a Comment