Friday, December 6, 2024

MAFIA WALILIA BOTI ZA MWENDOKASI


WANANCHI wa Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani wameiomba Serikali kuwapatia huduma ya boti zinzokwenda haraka badala ya kutumia boti ambazo hutumia masaa mengi baharini ambapo kwa sasa usafiri wa baharini umerahisishwa kama ilivyo kwa wasafiri wanaoenda Zanzibar.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Mafia Juma Ally kwenye kikao cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Pwani kilichofanyika Mjini Kibaha.

Ally lisema kuwa wanaishukuru serikali kuwapatia boti kwenda Mafia lakini boti hiyo hutumia masaa mengi ambapo ni kati ya masaa sita au saba tofauti na boti zinazoenda Zanzibar ambazo hutumia nusu ya masaa hayo.

“Usafiri tunaotumia unasaidia lakini ungeboreshwa kwa kupata boti ambazo zinatumia injini badala ya hizoi ambazo zinatumia kasi ili tusafiri kwa haraka tofauti na ilivyosasa,”alisema Ally.

Alisema kuwa boti hizo za sasa zinatumia pangaboi lakini tunashauri tupatiwe zile ambazo ni jeti ambazo mwendo wake ni wa kasi.

“Tukipata boti za mwendo kasi hata watalii wataongezeka lakini kwa sasa wtaalii ni wachache kwani tunapata watalii 10,000 lakini usafiri huo ukipatikana wataongezeka na tutakuwa na watalii wengi hivyo kuongeza mapato ya Halmashauri yetu,”alisema Ally.

Aidha alisema kuwa kutokana na kutokuwa na boti hizo za mwendokasi kabla ya kufanya safari lazima kuwe na maji mengi jambo ambalo ni changamoto kubwa lakini ingekuwa boti za kasi zingefanya safari tu bila ya kusubiri maji kuwa mengi.

“Ombi letu lingine tunaomba Bandari ya Kisiju Wilayani Mkuranga iboreshwe ili itumika kwani kula ni rahisi tofauti na Bandari ya Nyamisati iliyopo Wilayani Kibiti hilo nalo tunaomba lifanyiwe kazi kikubwa ni kurahisisha usafiri wa wakazi wa Mafia,”alisema Ally.

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa pwani akitoa ushauri alisema kuwa jambo kubwa ni kuangalia maslahi mapana ya wananchi hivyo miradi mbalimbali izingatie vipaumbele kutokana na maeneo na vitakavyoendana na vipaumbele vya Rais.

Kunenge alisema kuwa wajumbe wanapaswa kuangalia vipaumbele kwa uhalisia kwani fedha ni ndogo hasa ikizingatiwa nchi ilfanya uchaguzi ambao umetumia gharama kubwa hivyo kuwe na vipaumbele katika utekelezeji wa miradi.


No comments:

Post a Comment