Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Mafia Juma
Ally kwenye kikao cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Pwani kilichofanyika Mjini
Kibaha.
Ally lisema kuwa wanaishukuru serikali kuwapatia boti kwenda
Mafia lakini boti hiyo hutumia masaa mengi ambapo ni kati ya masaa sita au saba
tofauti na boti zinazoenda Zanzibar ambazo hutumia nusu ya masaa hayo.
“Usafiri tunaotumia unasaidia lakini ungeboreshwa kwa kupata
boti ambazo zinatumia injini badala ya hizoi ambazo zinatumia kasi ili tusafiri
kwa haraka tofauti na ilivyosasa,”alisema Ally.
Alisema kuwa boti hizo za sasa zinatumia pangaboi lakini
tunashauri tupatiwe zile ambazo ni jeti ambazo mwendo wake ni wa kasi.
“Tukipata boti za mwendo kasi hata watalii wataongezeka
lakini kwa sasa wtaalii ni wachache kwani tunapata watalii 10,000 lakini
usafiri huo ukipatikana wataongezeka na tutakuwa na watalii wengi hivyo
kuongeza mapato ya Halmashauri yetu,”alisema Ally.
Aidha alisema kuwa kutokana na kutokuwa na boti hizo za
mwendokasi kabla ya kufanya safari lazima kuwe na maji mengi jambo ambalo ni
changamoto kubwa lakini ingekuwa boti za kasi zingefanya safari tu bila ya
kusubiri maji kuwa mengi.
“Ombi letu lingine tunaomba Bandari ya Kisiju Wilayani
Mkuranga iboreshwe ili itumika kwani kula ni rahisi tofauti na Bandari ya
Nyamisati iliyopo Wilayani Kibiti hilo nalo tunaomba lifanyiwe kazi kikubwa ni
kurahisisha usafiri wa wakazi wa Mafia,”alisema Ally.
Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa pwani akitoa ushauri alisema
kuwa jambo kubwa ni kuangalia maslahi mapana ya wananchi hivyo miradi
mbalimbali izingatie vipaumbele kutokana na maeneo na vitakavyoendana na
vipaumbele vya Rais.
Kunenge alisema kuwa wajumbe wanapaswa kuangalia vipaumbele
kwa uhalisia kwani fedha ni ndogo hasa ikizingatiwa nchi ilfanya uchaguzi ambao
umetumia gharama kubwa hivyo kuwe na vipaumbele katika utekelezeji wa miradi.
No comments:
Post a Comment