Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya wiki ya Uwekezaji na Biashara Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya PMM Group Dk Judith Spendi amesema matumizi yanayopaswa kutumika kwa kupikia ni ya nishati safi.
Dk Spendi amesema kuwa Dar es Salaam na Pwani inatumia mkaa tani milioni 2.4 kwa mwaka hali ambayo ni hatari kwa misitu.
"Tunahamasisha matumizi ya majiko sanifu ambapo tutaanza uzalishaji wa majiko sanifu na upandaji miti ili kuepuka mabadiliko ya tabianchi,"amesema Dk Spendi.
Waziri wa Viwanda na Biashara Suleiman Jaffo aliipongeza kampuni ya PPM Group kwa jitihada zake za kukabiliana na uharibifu wa mazingira na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
No comments:
Post a Comment