Aidha benki hiyo imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kumkumbuka mpigania Uhuru wa Tanzania Bibi Titi Mohamed kupitia tamasha la (Bibi Titi Mohamed Festival) linalofanyika kila mwaka.
Akipokea vifaa hivyo hospitalini hapo Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa ameishukuru benki hiyo kwa kutoa msaada huo.
Mchengerwa amesema kuwa benki hiyo imemuenzi mwasisi huyo ambaye pia ni Mbunge wa kwanza wa Rufiji na imeonyesha uzalendo kwa kuwasaidia wakinamama wajawazito kwenye hospitali hiyo ya Wilaya ya Utete.
No comments:
Post a Comment