Tuesday, April 30, 2024

*BMH YAHUDHURIA UFUNGUZI WA MKUTANO WA 24 BARAZA LA MAWAZIRI* *SEKTA* *YA* *AFYA* *EAC*

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imehudhuria ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa 24 wa Baraza la Mawaziri la sekta ya Afya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Dar es Dar es Salaam. 

Mkutano huo wa siku tano, ulioanza leo tarehe 29 Aprili hadi Mei 3,  unafanyika kwa njia ya mseto (video na ana kwa ana) umeanza katika ngazi ya wataalam ukilenga kufanya tathimini ya utekelezaji wa maagizo na makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa 22 wa Baraza hiloa mbapo taarifa itawasilishwa katika Mkutano wa Makatibu Wakuu.

Mkutano utafuatiwa na ngazi ya Makatibu Wakuu tarehe 2 Aprili 2024, ambapo taarifa itawasilishwa, Makatibu na kuhitimishwa na Mkutano ngazi ya Mawaziri ukaofanyika Mei 3.

Mbali na kufanya tathimini ya utekelezaji wa maagizo na makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa 22 wa Baraza hilo, Mkutano huo utajadili agenda nyingine zinazotarajiwa ikiwemo Mkutano taarifa za Vikundi Kazi (Technical Working Group – TWG) sita (06) vya Sekta ya Afya na mapendekezo ya Tanzania ya kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto na Sayansi ya Matibabu ya Magonjwa ya Damu chini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa. 

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano huo, Mganga Mkuu wa Serikali wa Tanzania Prof. Tumaini Nagu, ametoa rai kwa wataalamu wa sekta ya Afya ya EAC kutoa michango itayosaidia Jumuiya kuimarisha miundombinu ya huduma ya afya ili kukabiliana na matishio ya kiafya kwa magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza.

“Tumekuja kujadili na kutoa suluhisho na majawabu yatakayotusaidia kukabili changamoto za kiafya katika Jumuiya yetu kwa kuzingatia ubunifu na weledi katika mifumo yetu ya afya huku tukiwa wamoja na wenye nguvu zaidi” amesema Prof. Nagu

Pro. Nagu amehimiza umuhimu wa Sekta ya Afya katika Jumuiya kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi na umoja katika utekelezaji progamu mbalimbali za Afya ikiwemo miradi ya Sekta ya Afya na mikakati inayopangwa ili kufikia mafanikio yanayotarajiwa kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka, ameeleza kuwa kupitia mkutano huo nchi wanachama watapata fursa ya kusikia taarifa zitakazowasilishwa na kila nchi ili kwa pamoja kuweza kuchangia na kushauri namna bora ya kusimamia na kutekeleza programu, miradi na miundombinu ya Afya katika Jumuiya.

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo umeongozwa na Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Tumaini Nagu na wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambapo imewakilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka. 

Wengine kutoka Tanzania walioshiriki Mkutano huo ni pamoja na Wizara za Afya (Tanzania Bara na Zanzibar), Hospitali ya Benjamin Mkapa, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu cha Afrika Mashariki, Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TMDA), Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) Bohari ya Dawa (MSD), Maabara Kuu ya Taifa, Mpango wa Kitaifa wa Kudhibiti Malaria (NAMCP) na Mamlaka ya Chakula na Dawa Zanzibar (ZFDA).

Monday, April 29, 2024

MWENGE KUPITIA MIRADI YA TRILIONI 8.6

MWENGE wa Uhuru umeanza mbio zake Mkoani Pwani ukitokea Mkoani Morogoro ambapo utapitia miradi 126 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi trilioni 8.5.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge alipoupokea Mwenge huo eneo la Bwawani Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo, kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima.

Kungenge alisema kuwa kati ya miradi hiyo 18 itawekewa mawe ya msingi 22 itazinduliwa 86 itakaguliwa.

"Miradi hiyo imefanikiwa kutokana na Rais kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na ushirikiano kati ya viongozi, wananchi na wadau wa maendeleo katika kutafuta fedha hasa ikizingatiwa Pwani ni Mkoa wa kimkakati,"alisema Kunenge.

Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge Godfrey Eliakim Mzava alisema kuwa wanapofika kwenye miradi ya maendeleo wakute taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo pia nyaraka zote za msingi zinazoeleza utekelezaji wa miradi iliyoyopo na wataalamu watoe maelezo ya kina na vifaa vya upimaji ubora wa miradi viwepo.

Mwisho. 




Saturday, April 27, 2024

MKUU WA MKOA WA PWANI ABUBAKAR KUNENGE ATAKA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE WALIOMDHALILISHA DK KAWAMBWA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amelitaka jeshi la Polisi Wilayani Bagamoyo kumchukulia hatua za kisheria Hassan Usinga "Wembe" kwa tuhuma za kumdhalilisha aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo na Waziri wa Miundombinu Dk Shukuru Kawambwa.

Kunenge ameyasema hayo wakati wa kikao baina ya Dk Kawambwa na Wembe na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bagamoyo akiwemo Mkuu wa Wilaya Halima Okash na Mkurugenzi wa Halmashauri Shauri Selenda na baadhi ya wakuu wa idara mbalimbali. 

Alisema kuwa suala hilo limesababisha kuhatarisha usalama wa Mkoa na taharuki kwa baadhi ya watu nchini kutokana na kitendo hicho cha udhalilishaji ikiwa ni pamoja na kufungwa pingu kwa kiongozi huyo mstaafu ambapo serikali haikubaliani nacho.

"Mwekezaji wa machimbo hayo ya mchanga ana vibali vyote vya umiliki na uchimbaji lakini changamoto iliyotokeza ni uharibufu wa barabara uliofanywa na malori ya yanayopita hapo yanayobeba mchanga na kuharibu barabara kutokana na uzito mkubwa na kusababisha wananchi kuifunga,"alisema Kunenge.

Naye Dk Kawambwa alisema kuwa alifungwa pingu na mtuhumiwa huyo akishirikiana na mgambo Abdala Mgeni na kusukumwa hali ambayo ilimfanya ajisikie vibaya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Halima Okash alisema kuwa mwekezaji aliomba kibali cha shughuli za uchimbaji mchanga na baraza la madiwani likamkubalia baada ya kufuata taratibu zote kuanzia ngazi ya chini.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Bagamoyo Bupe Angetile alisema kuwa walizuia kutumika barabara hiyo ilifungwa kutokana na kuharibika lakini bado iliendelea kutumika kupitisha malori ya mchanga ambapo inauwezo wa kutumika na malori yenye uzito wa tani 10.

WAWILI MATATANI KUMDHALILISHA DK KAWAMBWA

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata watuhumiwa wawili Hassan Usinga au Wembe na Abdallah Mgeni kwa tuhuma za kumdhalilisha aliyewahi kuwa Waziri wa Miundombinu Dk Shukuru Kawambwa.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamtaka mtu aliyechukua na kusambaza video hiyo mitandaoni ajisalimishe kituo cha Polisi Bagamoyo
mara moja.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani (SACP) Pius Lutumo alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 24 saa 8 mchana huko Kitopeni Wilaya ya Bagamoyo.

Lutumo alisema kuwa tukio hilo lilionekana kupitia mitandao ya kijamii ambapo video ilionekana ikimwonyesha Waziri na Mbunge mstaafu Dk Shukuru Jumanne Kawambwa akishambuliwa kwa maneno makali na kudhalilishwa kwa kufokewa na
kutishiwa kufungwa pingu kama mhalifu na watuhumiwa hao hali ambayo iliyosababisha taharuki kubwa kwa jamii.

"Video hiyo ilionyesha Dk Shukuru Jumanne Kawambwa na mtu mwingine aitwaye Cathbert Enock Madondola walishambuliwa ambapo watuhumiwa hao baadae walipewa dhamana kwa mujibu wa sheria na watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapokamilika,"alisema Lutumo.

Alisema kuwa Wembe alifanya tukio hilo akiwa na askari mgambo aitwaye Abdala Mgeni ambapo chanzo cha tukio hilo ni magari ya mchanga ya mtuhumiwa kuharibu barabara na mashamba.

"Mtuhumiwa alifikia hatua hiyo baada ya magari yaliyokuwa yakienda kuchukua mchanga kwa mbali ya kuharibu barabara wakati yakipita kwenda kubeba mchanga eneo hilo hali iliyosababisha wananchi kufunga barabara kwa magogo ili kuzuia uharibifu huo wa barabara,"alisema Lutumo.

Kamanda Lutumo alisema kuwa Dk Kawambwa ni moja ya  wakazi wa eneo hilo ambapo walijaribu kuyazuia magari hayo ili kupunguza uharibifu.

Thursday, April 25, 2024

TFS YATOA MILIONI 20 KWA WANANCHI WA RUFIJI NA KIBITI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO

WAKALA wa Misitu Tanzania (TFS) imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 20 kwa ajili ya wananchi wa Wilaya za Rufiji na Kibiti Mkoani Pwàni ambazo zimekumbwa na mafuriko.

Akikabidhi mfano wa hundi Meneja Uhusiano wa (TFS) Johary Kachwamba kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa fedha hizo ni kusaidia mahitaji mbalimbali.

Kachwamba amesema kuwa wana misitu zaidi ya 10 yenye ukubwa wa hekari 32,000 hivyo wameona watoe pole kwa wananchi waliokumbwa na changamoto ya mafuriko.

Amesema kuwa wataendelea kushirikiana na serikali kusaidia sehemu mbalimbali zilizokumbwa na changamoto kama hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani ameishukuru TFS kwa kujitolea fedha hizo kwani zitaweza kusaidia wananchi hao kuweza kukabili baadhi ya mahitaji.

Kunenge amesema kuwa mbali ya kutoa fedha hizo pia wametoa eneo kwenye Kitongoji cha Chumbi B ambapo wananchi wa Muhoro watahamishiwa hapo.

Amesema wanaishukuru TFS katika jitihada za kulinda na kutoa elimu juu ya kuhifadhi mazingira na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala.

Aidha amesema wanashauri wananchi kuondoka kwenye eneo ambalo ni mkondo wa Bonde la Mto Rufiji na wananchi wakae maeneo ambayo si hatarishi kwa mafuriko.

Wednesday, April 24, 2024

PROFESA MKENDA ATAKA WATOTO WENYE CHANGAMOTO MAFURIKO WASAKWE WAENDE SHULE

WANAFUNZI ambao shule zao zimekumbwa na mafuriko nchini wataruhusiwa kusoma shule ambazo ziko jirani na wanakoishi ili wasikose masomo.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda alipotembelea kujionea hali halisi kwenye maeneo yenye taasisi za shule ambao zimekumbwa na mafuriko na kutoa misaada ya vifaa vya shule kwa baadhi ya Shule kwenye Wilaya ya Rufiji na Kibiti Mkoani Pwani.

Mkenda alisema kuwa wanafunzi ambao Shule zao zimekumbwa na mafuriko na hawataweza kusoma kutokana na mazingira hayo kuwa hatarishi na Shule kufungwa wanafunzi hao watasoma maeneo ambayo wazazi wao wamehamia ili wasikose elimu.

“Mfano tumejionea Shule ya Msingi Muhoro ili wanafunzi waende Shule inabidi wapande Mitumbwi kama sisi tulivyoapanda kiusalama siyo sawa kwani ni hatari kwa maisha yao na hata nyumba za walimu tumeona zimezingirwa na maji kwa hali hiyo ni vigumu Shule hiyo kuendelea kutumika hivyo wanafunzi hao wasome popote pale walipo ambapo ni jirani na wanapoishi kwani serikali haitaki mtoto akose elimu,”alisema Mkenda.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Caroline Nombo alisema kuwa wanaendelea kufuatilia maeneo yote nchini ambayo yanachangamoto za mafuriko ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma pia kutoa vifaa kwa wanafunzi na walimu ili kwa wale ambao vifaa vyao vimeharika na mafuriko wanapatiwa vingine ili masomo yaendelee.

Naye mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alisema kuwa wamechukua jitihada mbalimbali za kukabili changamoto hiyo ya mafuriko ambapo kwenye Shule ya Msingi Muhoro wameifunga Shule hiyo na nyingine na kuruhusu wanafunzi  kusoma kwenye Shule ambazo wako jirani nazo na hazina changamoto ya mafuriko.

Naye Ofisa Elimu Mkoa wa Pwani Sara Mlaki alisema kuwa Shule zilizoathirika na mafuriko Wilaya ya Rufiji ni 11 zenye wanafunzi 7,264 wasichana wakiwa ni 3,657 na wavulana 3,607 walimu 58 ambao nyumba zao zimeathirika.

Monday, April 22, 2024

SERIKALI IMEENDELEA KUTENGA FEDHA MIRADI YA NISHATI

 

Wellu Mtaki, Dodoma 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutenga fedha za kutekeleza miradi ya nishati ambapo katika kipindi cha miaka mitatu zaidi ya shilingi trilioni 8.18 zilitolewa.

“Maono na maelekezo yake kuhusu usimamizi wa sekta hii yamekuwa na mchango mkubwa katika ufanisi wa shughuli za sekta, katika hili, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuweka kipaumbele kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati.”

Aidha amesema kuwa Katika kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa umeme nchini, tayari nchi yetu imeanza kutumia umeme wa bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project (JNHPP). Huu ni ushindi na kielelezo tosha kwamba Mama yupo kazini.

Ametoa pongezi hizo jioni (Ijumaa, Aprili 19, 2024) wakati akifunga Maonesho ya Wiki ya Nishati yaliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amelipongeza Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kuweza kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji yaliyopo sasa. 

“Leo tarehe 19 Aprili, 2024 uzalishaji wa umeme ni mkubwa. Shirika letu la TAMESCO limemudu kuzalisha umeme zaidi ya mahitaji tuliyonayo na bwawa la Julius Nyerere Hydropower Project limeanza kazi na tayari megawati 235 ziko kwenye mfumo.”

Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha maonesho hayo yanakuwa endelevu ili Waheshimiwa Wabunge waweze kupata fursa ya kuwasilisha hoja zao mahsusi na kutatua kero za wananchi wanaowawakilisha.

Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya washiriki wa maonesho hayo ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita, Waziri Mkuu ameitaka Wizara hiyo ione uwezekano wa kuandaa maonesho kama hayo katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri. “Wakurugenzi wa Kanda na Mameneja wa Mikoa na Wilaya mko hapa. Nendeni mkae na muangalie jinsi ya kutekeleza jambo hilo,” amesisitiza.

Ameitaka Wizara hiyo iweke mkakati wa kuhakikisha wananchi wote wanapata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu fursa zinazopatikana kutokana na miradi inayotekelezwa na sekta ya nishati. “Pamoja na kuyaleta maonesho hapa Bungeni, kuna haja ya kupeleka maonesha kama haya kwenye maeneo ya katiati ya mji ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi na kujibu hoja zao,” amesema.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wadau mbalimbali walioshiriki  maonesho hayo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme.

Naye, Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema sekta ya nishati ni kati ya sekta mtambuka kwa sababu inalisha sekta nyingine nyingi na ikitikisika, inatikisa na maeneo mengine pia.

Amesema pamoja na utoshelevu wa umeme kwenye gridi ya Taifa, ili kuwe na maendeleo bado nchi inahitaji umeme wa kutosha na hasa kwenye viwanda na siyo kuwasha taa za majumbani.

Ameitaka Serikali itafute njia ya kutumia vizuri maji yanayotoka kwenye bwa la JNHPP ili yaweze kuwanufaisha wananchi wanaoishi maeneo ya jirani na bwawa hilo. “Bwawa limejaa kwa hiyo Serikali ihakikishe maeneo ya jirani yanapata maji ya kutumia. Tuanzishe gridi ya maji kama ilivyo kwenye gridi ya umeme. Kule chini tutengeneze njia ya kutunza maji kwa ajili ya matumizi ya umwagiliaji na mifugo,” amesema.

Naye, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema ushiriki wa mwaka huu umevunja rekodi kwani watu zaidi ya 480 walitembelea maonesho hayo ambapo 267 walikuwa ni Waheshimiwa Wabunge.

Ameyataja maeneo ambayo washiriki walikuwa wakiulizia zaidi ni umeme, nishati ya jua, nishati jadidifu, nishati safi ya kupikia, mafuta na gesi.

Amesema ili kujenga uelewa mpana kwa wananchi, wanapanga kuandaa kongamano maalum juu ya gesi asilia ambalo linatarjiwa kufanyika Mei, mwaka huu.

Sunday, April 21, 2024

GOODWILL NA SAPPHIRE GLASS ZATOA MISAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO RUFIJI



KAMPUNI ya utengenezaji Marumaru ya GoodWill na ya Vioo ya Sapphire Glass za Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani zimetoa misaada mbalimbali kwa wahanga wa mafuriko Wilayani Rufiji.

Akikabidhi misaada hiyo ofisa rasilimali watu wa GoodWill Jerry Marandu kwa mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Katibu Tawala wa Mkoa huo Rashid Mchatta amesema wameungana ili kusaidia wahanga hao wa mafuriko.

Marandu ambaye pia aliwakilisha kampuni ya Sapphire Glass amesema kuwa misaada hiyo ni unga wa sembe mifuko 70, mchele mifuko 10 na sabuni mifuko 20 ambavyo wameona vitasaidia sehemu ya mahitaji kwa walengwa hao wa mafuriko.

Naye Katibu Tawala Rashid Mchatta amezishukuru kampuni hizo kwa kujitolea kusaidia jamii kwani ni moja ya jukumu lao hivyo kuiunga mkono serikali kusaidia wananchi wake.

Mchatta amewaomba wadau wengine nao kuunga mkono kwa kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ili kuwapunguzia changamoto wananchi waliokumbwa na mafuriko kwenye Wilaya za Rufiji na Kibiti.





Saturday, April 20, 2024

SHIRIKA LA (THPS) LATOA MSAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO RUFIJI NA KIBITI

  







SHIRIKA la Tanzania Health Promotion Support (THPS) limetoa msaada wa vifaa vya shule na vyakula kwa wahanga wa mafuriko katika Wilaya za Rufiji na Kibiti Mkoani Pwani.
Misaada hiyo ilikabidhiwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Bodi Profesa Mohamed Janabi ambaye amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa (THPS) Dk. Redempta Mbatia, viongozi kutoka Serikali za Mkoa wa Pwani na Wilaya za Rufiji na Kibiti, wahudumu wa afya, maofisa wa THPS na wananchi wenye mapenzi mema.

Prof Janabi amesema msaada huo wenye thamani ya Shilingi milioni 18.8  ni pamoja na vifaa vya shule  zikiweno sare za shule, mabegi, madaftari na kalamu vyenye thamani ya shilingi milioni 7.8 huku kwa upande wa vyakula ni pamoja na unga wa mahindi kilo 1,500, maharage kilo 750 na mafuta ya kupikia dazeni 29.5 vyote vikiwa na thamani ya Shilingi milioni 10.9.

Amesema kuwa mahitaji hayo yanatarajiwa kutoa ahueni kwa waathirika wa mafuriko wakati wakijpanga kurejea kwenye shughuli zao mbalimbali za kiuchumi.

"THPS na wao kama moja wapo ya wadau wakubwa wa afya wanaofanya kazi mkoani Pwani tumeungana na Serikali katika jitihada za kusaidia watu waliokumbwa na mafuriko,"amesema Prof Janabi.

Aidha amesema kuwa wanatumai msaada huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza adha wanayoipata wakazi wa Wilaya za Rufiji na Kibiti waliokumbwa na mafuriko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe.  Abubakar Kunenge alitoa shukrani zake kwa THPS kwa msaada huo na kusema kuwa anatarajia kuendelea kushirikiana na Shirika hilo.

Kunenge amesema kuwa msaada huo utasaidia kuleta matumaini kwa watu waliopoteza mali na makazi kutokana na mafuriko hayo.

THPS ni Shirika lisilo la kiserikali lililoanzishwa mwaka 2011 na kupitia uimarishaji wa mifumo ya afya na jami linalenga katika kushughulikia changamoto mbalimbali za afya ya umma, ikiwa ni pamoja na VVU na UKIMWI, kifua kikuu, ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto, huduma za afya ya uzazi, watoto wachanga, watoto nã vijana, maabara na mifumo ya taarifa za usimamizi wa afva, UVIKO- 19 na tathmini za afya ya umma.








Friday, April 19, 2024

KUNDI LA KIBAHA HURU FIKRA HURU LATOA MADAWATI 30

KUNDI la Whatsapp la Kibaha Huru Fikra Huru limetoa msaada wa madawati 30yenye thamani ya shilingi milioni tatu ili kusaidia wanafunzi ambao wanakabilia na upungufu wa madawati kwenye Shule za Msingi za Halmashauri ya Mji Kibaha.

Mwenyekiti wa Kundi hilo la Kijamii Mchungaji Paschal Mnemwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha mara baada ya kukabidhi madawati hayo amesema wameguswa na changamoto ya wanafunzi hao kukaa chini.

Mch Mnemwa amesema kuwa wameamua kuchangia madawati hayo ili kuisaidia serikali ili kukabiliana na changamoto hiyo ili wanafunzi wasome katika mazingira mazuri.

"Nawashukuru wana kikundi na watu mbalimbali kwa kutoa fedha na huu siyo mwisho kwani huo ni mwanzo wa kusaidia kumfuta vumbi mtoto wa Kibaha ili kumfanya mtoto awe na moyo wa kusoma na wadau mbalimbali wajitoe kusaidia tujenge tabia kusaidia maendeleo,"amesema Mnemwa. 

Amesema jamii isitegemee misaada toka nje bali ianze kuchanga yenyewe ili kusaidiana wenyewe kwa wenyewe badala ya kusubiri kusaidia kutoka nje ya nchi wafadhili wa kwanza iwe jamii yenyewe ili kuleta maendeleo.

"Mifumo ya mitandao ya kijamii ilitengenezwa ili kuiweka jamii pamoja kusaidiana na wasiitumie vibaya kwani endapo itatumika vibaya itaharibu maadili ya jamii ikitumika vizuri inaweza kuleta maendeleo,"amesema Mnemwa.

Akipokea madawati hayo mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amesema kuwa anawashukuru na kuwapongeza kundi hilo kwa kuunga mkono jitihada za serikali kwa kujitolea madawati hayo.

Ndomba amesema kuwa madawati hayo yatasaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati kwenye shule mbalimbali za Mji wa Kibaha na kuwataka wadau wengine kuchangia kama walivyofanya kundi hilo.

Kwa upande wake Ofisa Elimu Msingi Taaluma wa Halmashauri ya Mji Kibaha Adinani Livamba amesema kuwa wana upungufu wa madawati zaidi ya 3,000 ambapo madawati ni hitaji kubwa kwani wanafunzi wanafunzi wanaongezeka pia yanaharibika hivyo changamoto hiyo haiwezi kwisha kabisa.

Livamba amesema kuwa wanachukua hatua mbalimbali kukabili changamoto hiyo ikiwa ni pamoja na kufanya ukarabati wa madawati 1,321 na wanafanya na matengenezo na madawati hayo yatasaidia wanafunzi 90 wa darasa la kwanza, la pili na la tatu ambao ndiyo watanufaika.

Naye msemaji wa kundi hilo Hamis Mponji amesema kuwa fedha zimechangwa na watu wa Kibaha na nje ya Kibaha ambapo kulikuwa hakuna kiwango maalum cha kuchanga ni kile ambacho mtu kaguswa kukitoa.

Moja ya viongozi wa kundi hilo Hamad Kibwelele amesema kuwa wakati wanaanzisha kundi wakaona lisiwe na maongezi tu bali wafanye kitu cha maendeleo kwenye jamii na kukubaliana kuchangia madawati huku wakiangalia nini cha kufanya kwa baadaye ili kuleta maendeleo Kibaha.

Tuesday, April 16, 2024

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAONGEZA MELI ZA UVUVI BAHARI KUU

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu  (Deep Sea Fishing Authority-DSFA) imefanya maboresho katika kanuni za Sheria Uvuvi wa Bahari Kuu  na kupandisha utoaji wa vibali vya uvuvi katika Bahari Kuu kutoka  meli tisa mwaka 1988 hadi meli 61 mwaka 2023/24 kwa ajili ya kufanya uvuvi katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari (EEZ) upande wa Tanzania.

Hayo yamesemwa Leo Tarehe 16 Aprili 2024 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Muungano kuelekea maadhimisho ya miaka 60.

Ameeleza kuwa DSFA imeingia mkataba na Kampuni ya Albacora ya nchini Hispania kwa ajili ya ujenzi wa  kiwanda cha kuchakata samaki katika Mkoa wa Tanga na kitakuwa na uwezo wa kuchakata tani 20 za samaki kwa siku, kuhifadhi tani 2,400 za samaki na kuajiri wafanyakazi zaidi ya 100.

Pia amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepanga kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kukitumia Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji cha Machui – Tanga kupata vifaranga vya samaki na viumbe maji wengine wakiwemo jongoo bahari kwa ajili ya kuendeleza uchumi wa buluu.

Aidha, zaidi ya wananchi milioni 4.5 wanakadiriwa kupata kipato chao cha kila siku kutokana na shughuli za Uvuvi, zikiwemo kuunda na kutengeneza boti, kushona nyavu, biashara ya samaki na mazao yake pamoja na Baba na Mama lishe. 

Ikumbukwe kuwa sekta ya uvuvi ni miongoni mwa sekta tatu za Kilimo ambazo zinaajiri wananchi wengi na imeweza kutoa ajira za moja kwa moja kwa wavuvi 198,475 na wakuzaji viumbe maji wapatao 35,986.

SERIKALI YATOA BILIONI 696.7 KUPUNGUZA UMASKINI

SERIKALI imetoa shilingi bilioni 696.7 kwa ajili ya kupunguza na kuondoa umaskini kwa kaya milioni 1.3 kwenye vijiji  na mitaa.

Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya wizara hiyo yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 60 ya Muungano.

Simbachawene amesema kuwa lengo la Serikali ya awamu ya sita na awamu zilizopita zinazoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni kupunguza na kuondoa umaskini wa kipato.

Amesema Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ulianzishwa na serikali  mwaka 2000 kama mojawapo ya mikakati ya kupambana na umaskini kwa kutumia dhana ya ushirikishaji jamii.

"Jumla ya miradi 1,704 ya huduma za jamii yenye thamani ya shilingi bilioni 72 ilitekelezwa kupitia mpango huu wa TASAF awamu ya I awamu hii ilitekelezwa kwa mafanikio makubwa katika kuwapatia wananchi huduma muhimu za kijamii katika sekta mbalimbali zikiwemo za maji, elimu, miundombinu na afya,”amesema Simbachawene.

Simbachawene amesema awamu ya Pili ya TASAF ilianza utekelezaji mwaka 2005 hadi 2013 katika Halmashauri zote za Tanzania Bara na wilaya zote za Tanzania Zanzibar.

Amefafanua kuwa  jumla ya miradi 12,347 ya huduma za jamii yenye thamani ya shilingi bilioni 430 ilitekelezwa wakati wa Awamu hii ya Pili ya TASAF (TASAF II).

Amesema katika miaka 60 ya Muungano, serikali inayoongozwa na Rais,  Dk. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza jitihada za kuzuia na kupambana na rushwa ili wananchi waweze kupata huduma bora.

Aidha amesema kuwa TAKUKURU kwa kutambua kuwa Skauti ni suala la Muungano kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) ziumeunda timu ya uratibu ya kitaifa yenye Wajumbe kutoka Chama cha Skauti Tanzania (CST), ZAECA na TAKUKURU ili kuimarisha ushirikiano katika jitihada za kupambana na rushwa.

Pia amesema Ushirikiano huu ni muhimu sana kwa ustawi wa Taifa kwa kuwa Skauti wapo katika kundi la vijana na ni “Jeshi kubwa” ambalo tumeshuhudia likitoa mchango chanya katika matukio mbalimbali ya kijamii na kitaifa.

WANAOTUKANA VIONGOZI KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA


WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Masauni amesema kuwa  wanaotumia mitandao kuwatukana viongozi wa nchi  watakumbana na mkono wa sheria popote walipo.

Masauni ametoa kauli hiyo Aprili 15/2024  katika kumbi wa habari Maelezo Jijini  Dodoma alipokuwa akijibu swali la mmoja wa waandishi wa habari aliyeuliza Serikali ina mpango gani wa kuwachukulia hatua watu wanaomtukana Rais Samia katika mitandao.

Amesema kuwa hawatakuwa na msamaha  kwa mtu yoyote atakayevunja sheria ya kutukana viongozi na atatafutwa popote mpaka apatikane.

‘’Mimi niseme tu Serikali haina msalie mtume kwa mtu yeyote anayevunja sheria kwa kutukana viongozi katika mitandao na ina mkono mrefu wanaofanya hivyo watatafutwa popote walipo mkono wa sheria utawakamata,’’amesema Masauni.

Aidha Masauni ambaye alikuwa akielezea mafanikio ya miaka 60 ya Muungano amesema tangu enzi za waasisi wa Muungano Mwalimu Nyerere na Amani Karume walijenga Taifa lenye maadili hivyo ni budi kuendeleza yale waliyoacha waasisi wetu.

Sambamba na hayo ametoa wito kwa wananchi kuwa Serikali haitamfumbia macho mtu au kikundi cha watu wanaotukana viongozi kupitia mitandao  kwa kuwachukulia hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine.

‘’Msifikirie haya mambo yanayoenendelea mitandaoni na kutukana watu hawachukuliwi hatua utajikuta na wewe unafuata mkumbo usiige kwani hakuna atakayeachwa salama,"amesema Masauni.

Waziri huyo amesema kuwa hatua kali zitachukuliwa kwani Serikali ya Rais Samia haipendi kusumbua watu inataka watu waishi kwa amani na kila mmoja atii sheria bila shuruti.

‘’Dhamira ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapendi kuona watoto wake wanapata shida hivyo vyombo vya usalama vipo kazini’’, amesema Masauni.

Pia amesema katika kipindi cha miaka 60 ya Muungano sekta ya usalama wa nchi  iko vizuri na mafanikio ni mengi ikiwemo kuwa na majeshi ya polisi imara.

Sunday, April 14, 2024

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI YATOA SHUKRANI KWA CHUO CHA VETA MKOA WA PWANI KUWAPATIA USAFIRI KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA 102 KUZALIWA KWA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA DODOMA




Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdul Punzi kwa niaba ya uongozi ameshukuru chuo cha Veta Pwani kupitia Mkuu wa chuo hicho Madam Crala Kibodya kuwezesha safari hiyo kwa kutoa usafiri wa Coaster.

Ndugu Omary Punzi amesema huo ni uzalendo mkubwa kawa wadau nchini wasisite kusaidia katika shughuli nyingine.

Maadhimisho hayo yaliyofana yaliyohudhiliwa na Wananchi wengi wanafunzi na makundi mengine Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWAKILISHI WA BALOZI WA UGANDA YAPONGEZA UBUNIFU WA TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI







Mwakilishi wa Balozi wa Uganda Bregedia Ronald Bigirwa apongeza ubunifu wa Uongozi Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani kwa Tshirt yenye maneno mazuri.

Akipokeaa Tshirt hizo  yeye na mke wake katika maadhimisho hayo ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere lililofanyika katika Ukumbi wa Mji wa  Mtumba Mkoani Dodoma tarehe 13.4.2024

MEJA JENERALI BALOZI ANSELM BAHATI SHIGONGO ATUMA SALAMU ZA MKOA WA PWANI KONGAMANO LA MIAKA 102 YA KUZALIWA KWA MWALIMU NYERERE DODOMA

 



MWENYEKITI wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani Mh Meja Jenerali Balozi Anselm Bahati Shigongo amesema kuwa Mkoa wa Pwani ni mkoa bora katika uwekezaji wa viwanda.

Mh Meja Jenerali Balozi Bahati ameyasema hayo katika maadhimisho ya kitaifa ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mtumba Mjini Dodoma tarehe 13.4.2024 maadhimisho hayo yalihudhuliwa na Mh Daktari Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Amewaomba wadau wa maendeleo nchini waende Mkoani Pwani kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

KIMITI AIPONGEZA SERIKALI YA AWAMU YA SITA YA MH DKT SAMIA SULUHU HASSAN RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA






MWENYEKITI wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taifa Mh Paul Kimiti ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani namna anavyoenzi fikra na falsa za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa kuweza kutenga eneo la kujenga Makumbusho ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Dodoma.

Kimiti ameyasema hayo katika Maadhimisho ya kitaifa ya kumbukumbu ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Ukumbi wa Mtumba tarehe 13.4.2024 mkoani Dodoma ambapo mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wananchi wengi waliojitokeza kushuhudia Maadhimisho ya kumbukumbu hiyo.

Kimiti amesema kuwa jambo hilo litasaidia kutunza Kumbukumbu za Mwasisi huyo wa Taifa kwa kufanya vijana na makundi mengine kwenda kujifunza pia itaongeza pato la Taifa akiamini watu wa mataifa mengi watakuja kujifunza mambo mbalimbali yaliyofanywa na Nyerere.


Saturday, April 13, 2024

JAMII YAASWA ISILE MALI ZA YATIMA


SHEIKH Mkuu wa Mkoa wa Pwani Hamis Mtupa amewataka watu wanaodhulumu mali za yatima waache kwani ni sawa na kula moto ambao utawachoma matumbo yao.

Mtupa aliyasema hayo Wilayani Bagamoyo wakati wa dhifa kwa ajili ya watoto yatima, wajane na wazee iliyoandaliwa na Taasisi ya (SHAKIBA) Islamic Foundation ya Bagamoyo.

Alisema baadhi ya watu wamekuwa wakiwanyanyasa na kuwadhulumu mali za wazazi wao na kuzitumia huku watoto hao wakiwa hawaruhusiwi kuzitumia.

"Watu wanaokula au kujinufaisha na za yatima ni sawa na kula moto sawa na kaa la moto kulitia tumboni hivyo moto huo utawachoma na kila watakalolifanya halitafanikiwa,"alisema Mtupa.

Aidha alisema kuwa mtu anayekula mali ya yatima anamkanusha Mungu siku ya malipo atalipia dhuluma aliyoifanya kwa yatima hao ambao wanahitaji kusaidiwa.

"Tunapaswa kuwafadhi watoto yatima badala ya kuwatesa ili tupate thawabu wawekeni kwenye sehemu yao kwani ukimtunza kumpa faraja na kumlea utajiwekea mahala pema peponi,"alisema Mtupa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa SHAKIBA Alhaj Abdul Sharifu alisema kuwa taasisi hiyo ina lengo la kusaidia watu mbalimbali wenye mahitaji wakiwemo wajane, yatima na wazee.

Sharifu alisema kuwa tayari wameanzisha kituo cha kulea yatima ambapo 124 anawalea huku 24 akiwa anawsomesha wakiwa madarasa mbalimbali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Firdaus Centre Kituo cha Kulea Yatima cha Kongowe Kipala Mpakani Dk Sheikh Sharifu Firdaus alisema kuwa hakuna jambo baya kama kufiwa na wazazi.

Dk Sheikh Firdaus alisema kuwa watoto yatima wanapata tabu sana na wanachangamoto nyingi sana wanazokutana nazo hivyo wanahitaji misaada mbalimbali.

Kwa upande wake mwenyekiti idara ya wanawake Jamila Suleiman alisema kuwa wanawake wanahitaji kusaidiwa na waume zao na siyo kuwapa mizigo wanawake.

Suleiman alisema kuwa wao wanapigania haki za wanawake ambapo dini haitaki wanawake wanyimwe haki zao ambapo vipigo huondoa upendo na kusababisha visasi na majadiliano ni suluhu ya ugomvi.

Mratibu wa SHAKIBA Taifa Dk Fakhad Mtonga alisema kuwa lengo la kuanzishwa ni kusaidia jamii kwenye masuala mbalimbali yakiwemo ya afya, elimu, kilimo, uvuvi na elimu ya dini.

Dk Mtonga alisema kuwa pia wamekuwa wakitoa elimu ya kukabili vitendo vya ukatili na ukatili wa jinsia, kujitambua na kukabili vitendo viovu na wanatarajia kuanzisha kituo cha afya ambapo wasiojiweza waratibiwa bure na watu wengine watalipia gharama za matibabu kwa bei nafuu kilianzishwa 2020.

Thursday, April 11, 2024

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MFUMO MPYA WA KIELETRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA NeST

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi wa Mfumo mpya wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma unaojulikana kama National e-Procurement System of Tanzania (NeST) kabla ya uwekezaji huu.

Ununuzi wa umma ulikuwa ukifanyika kwa kutumia mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma uliojulikana kama Tanzania National e-Procurement System (TANePS) ambao ulijengwa na kampuni ya kigeni kutoka Ugiriki lakini Serikali ilibaini changamoto nyingi  kwenye ununuzi uliokuwa ukifanyika kupitia mfumo wa TANePS ikiwemo taarifa zote za Ununuzi wa umma kuwa chini ya usimamizi wa kampuni ya kigeni nje ya nchi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa kujenga uwezo wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Amin Mcharo wakati akizungumza na vyombo vya habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dodoma, kuhusu mafanikio makubwa waliyopata katika miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa changamoto hii na nyinginezo zilipelekea uamuzi wa kuanzisha mfumo mbadala ambao utakuwa bora zaidi, wenye kuleta tija, unaojengwa na wataalam wa ndani na kusimamiwa na Serikali. 

Aidha  amewaasa wananchi kujisajili katika mfumoNeST na kuomba zabuni mbalimbali zinazotangazwa na Serikali ili kuweza kujipatia kazi na kuhakikisha anayeomba amekidhi vigezo vinavyotakiwa katika kuomba zabuni husika na pindi wanapopata zabuni wazifanye kwa uadilifu na ufanisi ili waendelee kuaminiwa katika miradi mingine kutokana zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya Serikali inatumika kwenye ununuzi wa umma.



Ikumbukwe kuwa PPRA imekuwa ikitekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwahudumia wananchi ili kutimiza lengo la Serikali iliyopo madarakani  ya kupeleka huduma kwa wananchi na kuchochea matumizi ya utafiti, sayansi na teknolojia na ubunifu kama nyenzo ya maendeleo, kama inavyoonyesha katika Sura ya kwanza,Kipengele cha 8(e) ya Ilani hiyo wakati sura hiyohiyo kipengele cha 8 (f) ikielezea kujikita katika  kutengeneza ajira zisizopungua milioni 8 katika sekta rasmi na zisizo rasmi kwa ajili ya vijana.

Tuesday, April 9, 2024

*WMAs ZATAKIWA KUWA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA*

 

Serikali imewataka viongozi wa Jumuiya za Hifadhi Wanyamapori (WMAs) kuzingatia matumizi sahihi ya fedha  ili kuwanufaisha wananchi wa vijiji wanachama   pia kuzingatia mikataba inayoingiwa na WMAs hizo  kwa maslahi ya Taifa.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) ametoa kauli hiyo  leo Aprili 8,2024 Jijini Dodoma wakati wakati wa kikao cha viongozi wa Jumuiya hizo pamoja  na baadhi ya maofisa wanyamapori wa wilaya kuhusu changamoto za usimamizi wa maeneo ya WMAs nchini.

Amesema rasilimali fedha ni lazima  zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuendeleza miradi ya maendeleo ya vijiji kwa kuwashirikisha wananchi wa vijiji hivyo. 

 “Ni lazima muweke mkazo katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na uwazi na matumizi sahihi ya fedha pamoja na  utoaji wa taarifa kwa wanufaika kwenye vijiji husika, msipofanya hivyo uongozi utageuka shubiri mtakapofanyiwa ukaguzi” Mhe. Kairuki alisisitiza.

Amesema kuwa katika kipindi cha Mwaka wa fedha  2022/2023 Serikali imetoa mgao wa takribani bilioni 9.6 ambazo Serikali  inaamini zimetumika kwa mujibu wa Kanuni za WMAs ambazo zinaelekeza kuwa sehemu ya fedha hizo zitumike kutekeleza miradi ya maendeleo ya vijiji. 

Amesema kupitia kanuni hizo za uanzishaji na uendelezaji wa maeneo ya hifadhi kwa sasa kuna jumla ya WMAs 22 zilizodhinishwa na kupata haki ya matumizi ya rasilimali za wanyamapori lakini kuna nyingine 16 ambazo ziko kwenye mchakato wa kuanzishwa.

Aidha, ametumia fursa hiyo kuzishukuru WMAs kwa mchango wao katika kusaidia  kukuza uchumi kwa mtu mmoja mmoja na katika jamii  pamoja na kusaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika jamii na vijiji wanachama.

“Hii imejidhirishisha katika Sekta ya uwindaji wa Kitalii na utalii wa picha ambapo tumeshuhudia umekuwa chachu ya uchumi  kwa vijiji wanachama ambao wanaunda jumuiya zetu” Mhe. Kairuki amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Kairuki alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wadau wa uhifadhi imeendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha Jumuiya zinaendelea kuimarika ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo viongozi wa WMAs kwa lengo la kuimarisha utawala na usimamizi wa maeneo hayo na kuwezesha mafunzo kwa Askari wa Wanyamapori wa Vijiji (VGS) ambapo takribani VGS 540 wamepata mafunzo katika Chuo cha Wanyamapori Likuyuseka – Maganga.

Pia amesema Serikali imewezesha upatikanaji wa vitendea kazi ikiwemo magari ya doria kwa baadhi ya Jumuiya kama Mbarangandu na Nalika, Vilevile, Jumuiya zimewezeshwa vifaa vya uwandani kama vile mahema, GPS, kamera, sare za Askari Wanyamapori wa Vijiji (VGS) na vifaa vya ofisini kama kompyuta katika Jumuiya za MBOMIPA, WAGA na UMEMARUWA.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Kamishna CP Benedict Wakulyamba, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Fortunata Msoffe ,Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA,wawakilishi wa Makamishna Uhifadhi wa TANAPA, NCAA na TFS, Wakuu wa Idara na Taasisi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Maafisa Wanyamapori wa Wilaya, Wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii na  Viongozi wa Jumuiya za Wanyamapori.

Sunday, April 7, 2024

WASICHANA WATAKIWA KUWA MABALOZI KUPINGA VITENDO VYA UKATILI


Kamati ya Kupinga Ukatili wa kijinsia iliyo chini ya Wanawake na Samia imewataka wasichana ( Mabinti ) kuhakikisha wanakuwa viongozi wa kujiongoza wenyewe ili kuhakikisha wanapingana na suala zima la ukatili wa kijinsia na kuhakikisha wanakuwa mabalozi wazuri Ili kukomboa jamii inayokumbana na suala la unyanyasaji wa Mabinti na wanawake.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya ukatili wa kijinsia mkoa wa Dodoma  Grace Ringo wakati wa mafunzo ya utoaji  wa elimu katika chuo Mipango  chini ya uongozi wa Binti Makini kuhusu kupinga unyanyasaji kwa wanawake.

Amesema yapo mambo ambayo mwanamke wanakutana nayo kama Ulawiti, kupigwa , pamoja na kukosa haki ambazo zinamfanya mwanamke akashidwa kujiamini katika nafasi yake na kupelekea anguko  la uchumi katika jamii hata familia hivyo niwaombe Mabinti ambao mmepata elimu leo muhakikishe mnasaidia jamii

Kwa upande wake Mjumbe wa kamati ya ukatili wa kijinsia Mkoa wa Dodoma Irene Sanga amewasihi Mabinti kutumia mitandao kwa ajiri ya kuwaingizia kipato na sio kutumia mitandao kwa kufanya mambo maovu huku akiwasisitiza wawe na nidhamu Katika jamii ya leo

"Wapo Mabinti ambao wanatumia mitandao kwa kuangalia vitu visivyofaha na kupelekea Vijana kualibika kwa kuiga mambo ambayo kwa nafasi na umri bado na kulazimisha kufanya vitu kama rushwa za ngono," amesema Sanga.

Naye Mjumbe wa kamati ya kupinga ukatili chini ya ofisi ya Mkoa wa Dodoma  Rhoda Denis amewataka wasichana kuzingatia kujithamini na kujitambua  Ili kujikomboa katika maisha ya jamii ya leo.

"Wapo wanawake wanapigwa na waume zao sababu kukosa kujitambua ila kama utajua thamani yako utaweza kufika sehem ambayo utaweza kupata msaada," amesema Rhoda

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Binti Makini Chuo Cha Mipango Dodoma Swaumu Rajabu amewahimiza wanawake kujitokeza kugombania nafasi mbalimbali za uongozi kwani wanawake tunanafasi kubwa sana katika jamii leo hivyo tuwe mstari wa mbele kuwasihi na wengine unaowaona wanaweza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi yetu .

 Aidha amesema kuwa chuo Cha mipango kinaenda kufanyika uchaguzi wa viongozi wa serikali ya wanafunzi ikiwemo nafasi mbalimbali kama Rais wa chuo Cha mipango, wabunge pamoja nafasi nyingine hivyo amewaomba Binti Makini wote wenye sifa wajitokeze wakagombee nafasi hizo.

Ikumbukwe kuwa kamati ya Kupinga Ukatili wa kijinsia iliyochini ya wanawake na Samia inaendelea kufanya mafunzo ya utoaji wa elimu kwa wanawake na wanaume ili kuhakikisha elimu hii inawafikia wengi ili kutengeneza Taifa lenye nguvu kazi na lenye Maadili ikiwa na kauli mbiu IPELEKE DODOMA DUNIANI NA DUNIA  ILETE  DODOMA

Saturday, April 6, 2024

MTAA WA KWAMFIPA WAANZA UJENZI WA SEKONDARI

MTAA wa Kwamfipa Kata ya Kibaha Mkoani Pwani umeishukuru serikali kwa kuwapatia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 60 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ambayo utawapunguzia changamoto wanafunzi wa Mtaa huo wanaotembea umbali wa Kilometa nane kwenda Shule ya Sekondari ya Simbani.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kibaha Mohamed Muanda alipotembelea kuangalia maendeleo ya ujenzi huo kwani ni ukombozi kwa wanafunzi wanaotoka kwenye Mtaa huo.

Muanda amesema kuwa hicho kilikuwa kilio cha wananchi wa Mtaa huo pamoja na Mtaa wa Mwendapole ambapo Mitaa hiyo miwili ina jumla ya shule tatu za Msingi ambapo wanafunzi wote husoma Shule hiyo ya Simbani ambayo ni ya Kata.

Kwa upande wake Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Jumanne Mwinshehe amesema kuwa wananchi walijitolea kwa kufanya usafi kabla ya ujenzi kuanza huo ukiwa ni mchango wa wananchi na wataangalia fedha za Halmashauri zitaishia wapi ili wananchi wachangie ambapo ujenzi huo uko hatua ya msingi.

Naye Christina Sabai wanafunzi wanakwenda Sekondari mbali na kwa watoto wa kike ambao hukumbana na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kurubuniwa na waendesha pikipiki na kuhatarisha masomo yao kwa kupata ujauzito.

Aidha fundi wa ujenzi wa mradi huo wa Shule hiyo Juma Mabula amesema watatumia siku 75 kukamilisha ujenzi huo kwani vifaa vyote viko hivyo wanaamini watakamilisha kwa muda uliopangwa ili wanafunzi waanze kusoma.

Friday, April 5, 2024

TAASISI YA KUMUOMBEA RAIS NA WASAIDIZI WAKE YAFANYA MAOMBI KUIOMBEA SERIKALI

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Taasisi ya kumuombea Rais  na wasaidizi wake imefanya maombi ya kuombea viongozi wa serikali akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Spika wa Wabunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Akson pamoja na Mawaziri na Wabunge. 

Katibu Mkuu wa taasisi hiyo Angelina Malembeka akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya maombi hayo amesema lengo ni kuwaombea ili waongoze kwa hekima.

Malembeka amesema kuwa anaamini taasisi hiyo itaweza kusaidia mambo mengi yasiyofaa yasipate nafasi na malengo ya taasisi ni kumuombea Rais  na wasaidizi wake pamoja na wataalamu mbalimbali wanaofanya shughuli za jamiii ndani ya nchi.

"Katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mambo yanaenda vinzuri ila wao wanafanya kazi ya kuombea Ili kuhakikisha utekelezaji unaenda vizuri zaidi,"amesema Malembeka.

Alisema wanaona mambo yanaenda vizuri katika miradi mbalimbali na utekelezaji wa ilani ya CCM na kazi yao ni kuombea viongozi wawe na ujasiri, nguvu na kuwapa matumaini na ikumbukwe kuwa suala hili la kuombea Rais na wasaidizi wake ni suala la muendelezo na kazi yake ni kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu.

Aidha amesema kuwa idadi ya wanachama ni zaidi ya wanachama 600 lakini walioshiriki maombi hayo walikuwa ni 208 ambapo wengine hawakuhudhuria kutokana na sababu mbalimbali.


 

Thursday, April 4, 2024

MKUU WA MKOA DODOMA ROSEMARY SENYAMULE AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, imeendelea Wilayani Kondoa April 3/ 2024 ambapo amefanya ukaguzi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa wilayani humo ikiwemo Ujenzi wa Wodi ya wazazi, jengo la Mochwari na jengo la upasuaji katika hospitali ya wilaya ya kondoa.

Aidha amekagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari  ya wasichana Kondoa pamoja ukaguzi wa nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya kondoa mji ambapo ujenzi unaendelea na unatarajia kukamilika muda wowote kwani umefika hatua za umaliziaji ( Finishing).

Hatahivyo Mhe. Senyamule ameendelea kuwahimiza watumishi wa sekta ya afya kuendelea kutunza mazingira yanayozunguka katika vituo vyao ili kuendelea kuweka mazingira safi na ya kuvutia siku zote ikiwemo kupanda miti kwa mpangilio unaofaa.

SIDO YAWATAMBUA WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUZALISHA BIDHAA BORA KUKUZA UCHUMI

KATIBU Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta amewataka wajasiriamali  watakiwa kuzingatia uzalishaji wa bidhaa zao kitaalam ili kukuza uchumi wa mkoa huo.

Mchatta ameyasema hayo wakati akikabidhi vyeti vya kwa wajasiriamali wenye viwanda vidogo na vidogo kabisa wa mkoa huo ambao wametambuliwa na Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) Mkoa wa Pwani.

Amesema kuwa wajasiamali hao wanapaswa kuzingatia ubora na viwango pia kushirikiana na taasisi zinazothibitisha viwango vya bidhaa ili ipate soko ndani na nje ya nchi.

Aidha ameipongeza SIDO kwa jitihada za kuwawezesha wajasiriamali ambapo Mkoa huo una jumla ya viwanda 1,533 vikubwa 122 vya kati 120 vidogo 274 na vidogo sana 1,117.

Naye Meneja wa SIDO Mkoa wa Pwani Beata Minga amesema kuwa unatambua jitihada za wajasiriamali ambao wameanzisha viwanda ambavyo vitaongeza ajira na kuongeza pato la mwananchi mkoa na Taifa.

Minga amesema kuwa vyeti hivyo vya kuwatambua vitawasaidia pale wanapohitaji kutambuliwa na taasisi nyingine ambazo ni za uwezeshaji na zoezi hilo litakuwa endelevu ambapo jumla ya wajasiriamali 65 wametambuliwa 

Wednesday, April 3, 2024

*MTOTO* *ATOLEWA* *SARAFU KOONI*

Wataalamu katika Idara ya ENT ya Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wamefanikiwa kuitoa sarafu iliyokuwa imekwama kwenye koo la mtoto mdogo kwa siku sita.

Daktari Bingwa wa Masikio, Pua na Koo wa BMH, Emmerenceana Mahulu, amesema BMH imempokea  mtoto huyo wa miaka miwili siku ya Alhamisi ya tarehe 26, Machi.

"Tumefanikiwa kuitoa sarafu iliyokuwa imekwama kwenye koo la mtoto kwa siku sita kwa kutumia kifaa tiba kinachoitwa _esophagoscopy_," amesema Daktari huyo Bingwa ambaye pia Kaimu Mkuu wa Idara ya ENT ya BMH.

Dkt Mahulu amefafanua kuwa sehemu ya koo ilipokuwa imekwama sarafu  ilisabisha uvimbe, akiongeza kuwa ilikuwa imeacha uwazi kidogo ambayo ilikuwa ikiruhusu vimiminika kama uji, maji juisi kupita.

"Mtoto anaendelea vizuri baada ya matibabu na anaweza kula vizuri kwa sasa. Tumeishamruhusu na tutamuona tena baada ya wiki moja ili kuona maendeleo yake," amesema. 

Kwa mujibu wa mama wa mtoto, Juliana Yuda, mkazi wa kijiji cha Mkoka, Kongwa, Dodoma, mtoto wake, ambaye alitoka kucheza na wenzake siku ya Jumamosi ya  tarehe 20, Machi, alirudi nyumbani muda wa mchana akiwa analia.

"Mtoto alikuwa hawezi kula kwa muda wa siku sita, alikuwa anashindia uji, juisi na maji tu. Hali yake ilizidi kuwa mbaya Siku ya Alhamisi," anasema.

Anaongeza kuwa Alhamisi ya tarehe 26, Machi alimpeleka mtoto Hospitali ya Wilaya ya Kongwa ambapo alipewa rufaa kuja BMH baada ya kupigwa picha ya x-ray na kubaini sarafu imekwama kwenye koo.

Tuesday, April 2, 2024

WAFANYAKAZI OFISI YA RAIS FEDHA MIPANGO ZANZIBAR NA WAFANYAKAZI WIZARA YA FEDHA WASAIDIA WATU MAHITAJI MAALUM




Na Wellu Mtaki, Dodoma

Wafanyakazi Ofisi ya Rais fedha na Mipango Visiwani Zanzibar wakishirikiana na wafanyakazi wa wizara ya fedha wametembelea vituo vinne vya watu wenye mahitaji Maalum.

Vituo hivyo ni kituo cha Safina Street Network, Asmaa Bint Shams, kituo Cha  wasioona watu wazima Buigiri na Shule ya Msingi ya watoto wenye mahitaji maalum Buigiri ikiwa ni muendelezo wa ziara yao kila mwaka kutembelea vituo vya watu wenye maitaji Maalum na kutoa misaada ya chakula na fedha.

Hayo yamesemwa na ofisa Uendeshaji Ofisi ya Rais fedha na mipango Zanzibar Rajab Uweje wakati akizungumza na vyombo vya habari Jijini Dodoma mara baada ya ziara wameweza kutambua  mahitaji mengine ya vituo hivyo na ametoa ahadi awamu zijazo watajitaidi kuhakikisha wanatatua changamoto zao.

"Tumetoa ahadi katika vituo hivi tumechukua changamoto zao tuone awamu ijayo tuje kutatua changamoto tunaondoka hapa tukiwa tunaenda kuongea na viongozi wetu kuwaeleza hali iliyopo huku ili awamu ingine tuje tusaidie kutatua changamoto,"amesema  Uweje.

Pia ametoa wito kwa walezi wa vituo hivyo kuendelea kuwatunza watoto hao  na kuwasimamia  vizuri ili kujenga Taifa  lenye raia wema.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Hazina Sports Club Mugusi Musita amesema kuwa upo muhuhimu wa jamii kutambua kusaidia watu wenye maitaji maalum kutokana ha changamoto zilizopo kwenye jamii zao hivyo anaiomba jamii kiujumla kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kusaidia watoto kwani watoto ndiyo Taifa la kesho.

"Vituo vinamahitaji mengi na makubwa sana   kama viongozi  watambue watoto hawa wanamaitaji sana tumekuja kuwapa chochote ila naona kama havitoshi pia tutachuka nafasi hii kupeleka taarifa za cha changamoto hizi katika Halmashauri ya Chamwino nao waone namna ya kusaidia," amesema Musita.

Naye Mratibu wa  Shirika la Safina Street Network Dodoma Ebeneza Ayo ameiomba jamii kuacha kutoa hela kwa watoto wa mitaani ndiyo inasababisha watoto hao kuendelea  kukaa mitaani kuombaomba bali jamii iendelee kuwapa msaada kwa kuwasidi kuwapekeka katika vituo vya kulelewa ili waweze kupata msaada pamoja na elimu Ili kusaidia kutengeneza Taifa lenye nguvu kazi.

"Tuwapende hao watoto wanaotoka katika manzingira hatarishi tuwe  tayari kuwasaidia kwa mambo  mbalimbali tunavyokutana nao mitaani tujaribu kuwasaidia  waweze kwenda kwenye vituo au ofisi ustawi wa jamii na sio kuwapa hela kwani ukiwapa hela ndiyo wanazidi kukaa mitaani , lakini pia hata sisi wenye mashirika ya kuwasaidia watoto tunachangamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji katika kituo chetu hivyo tunaomba jamii iweze kutusaidia,"amesema Ayo.

Mwenyekiti wa Makazi ya watu wasioona Buigiri  Yaledi Daudi ameiomba serikali kuwasaidia kujenga maeneo yao ya Makazi kutokana na nyumba zao kuwa chakavu ili waweze kuishi maisha bora.

"Kwa upande wa serikali tunamshukuru  sana Rais Samia kwa kazi nzuri anayofanya na natoa wito kwa serikali kuwa nyumba zetu tunazoishi zimekuwa chakavu tunaomba serikali itujengee nyumba ili kuwa na maisha bora,"amesema Daudi

Ikumbukwe kuwa ziara hizi hufanyika kila mwaka ikiwa na lengo la kuwasaidia watu waishio manzingira magumu pamoja na watu wenye uhitaji mbalimbali, ziara hizi ufanyika katika maeneo ya visiwani Zanzibar na Bara kwa awamu tofauti tofauti.