Na John Gagarini, Kibaha
WATU wawili wamefariki dunia kufutaia mvua iliyonyesha juzi
mkoani Pwani ambapo miili yao imeweza kugundulika baada ya maji kupungua kwenye
mto Mpiji unaotenganisha mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.
Akithibitisha kuokotwa kwa miili hiyo kaimu kamanda wa polisi
mkoa wa Pwani Blasius Chatanda alisema kuwa miili hiyo ilikutwa kando kando ya
mto huo ambao ulikuwa umejaa kutokana na mvua kubwa zilizonyesha maeneo
mbalimbali ya nchi.
Chatanda alisema kuwa miili hiyo ilokotwa maeneo tofauti
ambapo mwili wa kwanza ulipatikana majira ya saa 2:30 eneo la Muheza kata ya
Pangani alitambuliwa kwa jina la Simon Ramadhan mwenye umri kati ya miaka (25)
na (30) uliokotwa eneo la mto Mpiji na marehemu alikufa alipokuwa akijaribu
kuvuka.
“Mwili wa pili wa Issa Ally (28) ambaye ni mgambo uliokotwa
eneo la Kiluvya na inadaiwa kuwa marehemu alisombwa na maji alipokuwa akijaribu
kumwokoa mtoto aliyetaka kusombwa na maji na kukutwa kilometa nne toka sehemu
aliyozama,” alisema Chatanda.
Alisema kuwa miili yote ya marehemu imehifadhiwa kwenye
hospitali ya Rufaa ya Tumbi kwa ajili ya kusubiri ndugu kwa ajili ya mazishi.
“Nawaomba wananchi kuwa makini wakati wa kuvuka kwenye mito
kuwa na subira ili maji yapungue waweze kuvuka na kuendelea na safari zao kwani
wasidaharu maji kama ni madogo ambapo yanaweza kuwaletea madhara,” alisema
Chatanda.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment