Friday, October 27, 2017

SABA WASOMBWA NA MAJI WANUSURIKA


Daraja linalounganisha mikoa ya Pwani na Dar es Salaam likiwa limejaa maji

 Baadhi ya wananchi wakifuatilia zoezi la uokoaji watu waliosombwa na maji ambao walipanda kwenye miti

 Moja ya kijana aliyenusurika Silas Moshi baada ya kusombwa na maji mara baada ya kuokolowa

 Dada ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kuokolewa akiwa amepoteza fahamu akipakiwa kwenye gari la polisi kwa ajili ya huduma ya kwanza.



 Kijana Mohamed Kitindi aliyenusurika baada ya kusombwa na maji 

 Furaha Mwaipopo moja ya watu walionusurika baada ya kusombwa na maji na kupanda kwenye mti


 Moja ya watu walionusurika akihojiwa na polisi baada ya kunusurika 

 Kened Meshaki ambaye alishika nguzo ya bango huku mwili wake ukiwa ndani ya maji kwa zaidi ya masaa matatu akiwa ameshikwa mkono na polisi kwa ajili ya kwenda kupatiwa huduma ya kwanza


Na John Gagarini,Kibaha

WATU saba wamenusurika kifo baada ya kusombwa na maji walipokuwa wakijaribu kuvuka huku wakiwa wameshikana mikono ambapo walijinusuru kwa kupanda kwenye miti kabla ya kuokolewa na kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani.

Aidha kati ya watu hao mmoja alikuwa akininginia kwa kujishika kwenye bomba la bango la matangazo huku mwili wake ukiwa ndani ya maji kwa masaa zaidi ya huku akiwa anaomba msaada wa kuokolewa bila mafanikio.

Watu walionusurika ni pamoja na Kened Meshaki, Mohamed Kitindi, Silas Moshi Henry Francis na mwanamke mmoj ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja ambao wote walikimbizwa hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Pwani.

Tukio hilo lilitokea jana eneo la Maili Moja wilayani Kibaha kwenye daraja linalotenganisha kati ya mkoa wa Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na kusababisha daraja kujaa maji na kusababisha magari na watu kushindwa kuvuka upande wa pili.

Daraja hilo ambalo linapita kwenye mto Mpiji lilikuwa halipitiki na kusababisha watu na abiria kushindwa kuvuka upande wa pili kutoka Maili Moja wilayani Kibaha na upande mwingine Kiluvya wilaya ya Ubungo.

Kutokana na daraja hilo kushindwa kupitika abiria wa mabasi wameshindwa kuendelea na safari zao za kwenda mikoani na maeneo mengine yanayopita kwenye barabara ya Morogoro.

Akizungumza na gazeti hili kwenye eneo la tukio hilo ofisa habari na uhusiano wa Jeshi la uokoaji Harison Mkonyi alisema kuwa zoezi la ukoaji limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wameweza kuwaokoa watu hao wakiwa salama.

Mkonyi alisema kuwa wamefanikiwa kuwaokoa watu hao kwa kushirikiana na wadau wengine ambao walijitosa kwenye maji hayo ambayo yalikuwa mengi na kulifunika kabisa daraja hilo na kusababisha kushindwa kupitika.

“Tunawashukuru wadau mbalimbali vikiwemo vikosi vya majeshi ya Polisi, Magereza, JWTZ na wananchi ambao walionyesha ushirikiano wa hali ya juu kuwanusuru watu hao akiwemo mwanamke mmoja,” alisema Mkonyi.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment