Thursday, October 19, 2017

MBUNGE KIBAHA MJINI AKABIDHI VYEREHANI KWA WATU WENYE ULEMAVU


Na John Gagarini, Kibaha

MBUNGE wa Jimbo la Kibaha mkoani Pwani Silvestry Koka ametoa vyerehani vinnne kwa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) wilaya ya Kibaha kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali.

Akikabidhi vyerehani hivyo kwa uongozi wa shirikisho hilo Katibbu wa Mbunge huyo Method Mselewa alisema kuwa mbunge huyo katoa vyerehani hivyo kufuatia ombi lao.

Mselewa alisema kuwa watu wenye ulemavu nao wanapaswa kusaidiwa kama wanavyosaidiwa watu wa makundi mengine yanavyosaidiwa ili kujiendeleza kiuchumi.

“Kuwa na ulemavu siyo mwisho wa maisha kwani nguvu mnazo na mnauwezo kama watu wasiokuwa na ulemavu na tutaendelea kuwasaidia ili nanyi mjikwamue kwa kujiongezea kipato chenu na cha familia zenu,” alisema Mselewa.

Alisema kuwa kutokana na kuungana kwao kutasaidia kuwafikia kwa urahisi kuliko kila mtu angekuwa anaomba peke yake ingekuwa ngumu lakini kwa kuwa pamoja imekuwa rahisi.

“Hizi mashine mnapaswa kuzitunza kwani mbali ya kuwapatia ujuzi kia zitawapatia kipato ambacho kitaweza kuwafanya muwe na mapato kuliko kuomba jambo ambalo halifurahishi,” alisema Mselewa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa SHIVYAWATA Ally Mlanga alisema kuwa wanshukuru msaada huo kwani kwao huo ni kama mtaji ambao watahakikisha wnaauendeleza.

Mlanga alisema kuwa wao hawataki fedha ila wanachotaka ni kupewa vitu ambavyo vitawasaidia kuliko fedha ambazo zinaweza kupotea kwa urahisi.

Naye ofisa Maendeleo wa Kata ya Kibaha Regina Lazaro alisema kuwa kupatiwa vyerehani hivyo vitawasaidia kujiongezea kipato kwani moja ya shughuli zake ni kuhamasisha ujasiriamali.

Lazaro alisema kuwa wamekuwa wakishirikiana na shirikisho hilo ikiwa ni njia mojawapo ya kuwasaidia kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na serikali au wadau toka sekta binafsi.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment