Na John
Gagarini, Kibaha
WAANDISHI wa
Habari mkoani Pwani na hapa nchini wametakiwa kutotumia vibaya kalamu zao ili
kulinda amani ya nchi kwani maneno yao endapo yatatumika vibaya ni hatari zaidi
ya bunduki.
Hayo
yalisemwa mjini Kibaha na mkuu wa wilaya ya Kibaha Asumter Mshama wakati
akifungua kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Pwani mafunzo juu ya Haki za Binaadamu
Utawala Bora na Amani nchini kwa Viongozi na watumishi wa serikali za mitaa
mkoa wa Pwani yaliyoandaliwa na Alpha And Omega Reconciliation And Peace
Building (AREPEB).
Mshama
alisema kuwa waandishi wana nafasi kubwa ya kudumisha amani iliyopo kwa kutumia
vyema kalamu zao katika kuleta mshikamano na kuepusha utengano.
“Nyie ndiyo
mnanafasi kubwa ya kuifanya nchi iendelee kuwa na amani au mnaweza kuifanya
nchi ikaingia kwenye machafuko hivyo mnatakiwa kutumia vizuri kalamu zenu kwa
kutotumia vibaya kalamu zenu,” alisema Mshama.
Alisema kuwa
mafunzo hayo yatawasaidia viongozi hao kuwahamasisha wananchi kulinda amani ya
nchi na kutokubali kuingia kwenye migogoro ambayo itasababisha amani kuvunjika.
“Tanzania
bado tuna amani kubwa na ya kutosha hatuna sababu ya kuleta vurugu kwani nchi
inatawaliwa kwa utawala wa sheria lakini kuna baadhi ya watu wanataka
kutuingiza kwenye matatizo,” alisema Mshama.
Naye
mkurugenzi wa (AREPEB) Francis Luziga
alisema kuwa lengo lao kubwa ni kujenga amani hapa nchini kwa kubadilishana
uzoefu na viongozi na watendaji wa serikali za mitaa na wasimamizi wa
watekelezaji wa sheria katika masuala ya haki za binadamu na utawala bora.
Luziga
alisema kuwa pia mafunzo hayo yameambatana na uzinduzi wa mfumo wa kieletroniki
wa kupokea maoni na malalamiko dhidi ya masuala mazima ya haki za binadamu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment