Na John Gagarini, Kibaha
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kibaha Mjini Mkoani Pwani Maulid
Bundala amefanikiwa kutetea kiti chake baada ya kushinda kwenye uchaguzi wa
chama hicho.
Bundala alifanikiwa kutetea nafasi yake hiyo kwa kipindi cha awamu
tatu sasa baada ya kushinda kwenye uchaguzi ambao ulifanyika kwenye shule ya
sekondari ya Filbert Bayi mjini Kibaha na kuwashinda wenzake wawili.
Wajumbe wa mkutano huo mkuu wa CCM Kibaha Mjini walimpa ushindi wa
kishindo Bundala kwa kumpigia kura 288 kati ya kura 489 za wajumbe wote huku
kukiwa hakuna kura iliyoharibika.
Aliyemfuatia mshindi alikuwa ni Batholomew Nyalusi ambaye alipata
jumla ya kura 164 akifutaiwa na Joseph Masenga ambaye alipata kura 37.
Kwa upande wa uwakilishi wa mkutano mkuu wa mkoa washindi wawili
walikuwa ni Rugemalila Rutatina kura 392 na Happines Mgalula kura 201 kwa
upande wa uwakilishi Halmashauri Kuu wilaya wajumbe wawili ni Kabunda Bekari
kura 238 na Philemon Mabuga kura 209.
Nafasi nne za uwakilishi toka Umoja wa Vijana (UVCCM) nafasi nne
ni Makwiro selaman kura 289, magreth Mbawala kura 283, Herman Kagaruki kura 269
na Jagala Salum kura 233.
Kwa upande wa uwakilishi Jumuiya ya Wanawake (UWT) nafasi nne
washindi walikuwa ni Zamda Komba kura 276, Dk Alice Karungi kura 255, Joyce
Mushi 230 na Joyce Shauri kura 185.
Washindi wa nafasi tatu za uwakilishi mkutano mkuu wa Taifa ni
Abdulaziz Jaad kura 355, Catherine Katere kura 336, Dk Alice Kaijage 332 ambapo
katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu alisema uchaguzi huo ulikwenda vizuri
na hakukuwa na malalamiko yoyote kutoka kwa wagombea.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment