Wednesday, October 11, 2017

MAMA SALMA KIKWETE AITAKA JAMII KUMSAIDIA MTOTO WA KIKE KUPATA ELIMU











Na John Gagarin, Kibaha

MKE wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mama Salma Kikwete amesema kuwa kuna haja ya kuondoa mila na desturi zinazomkwamisha mtoto wa kike kukosa elimu.

Ambapo jamii nzima inapaswa kumlinda mtoto wa kike ili aweze kufikia malengo yake kwa ukimsomesha umeisomesha jamii nzima na nchi itapata maendeleo.

Aidha alisema kuwa mkoa wa Pwani uko ndani ya mikoa 10 yenye matatizo ya mimba za utotoni ikiwa na asilimia 30 huku mkoa wa Katavi ukiwa ni wa kwanza kwa kuwa na asilimia 45 jambo ambalo halikubaliki kwa jamii kupinga masuala haya.

Ameyasema  wakati wa sherehe za siku ya mtoto kike Duniani zilizoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Room To Read ambapo kimkoa zilifanyika Kibaha na kusema kuwa Pwani inapaswa kuongoza kwenye mambo ya maendeleo na si kuongoza kwa mambo mabaya.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Kibaha Asumter Mshama ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Pwani amesema kuwa licha ya sheria kali kuwekwa lakini baadhi ya changamoto zimekuwa zikimkwamisha mtoto wakike kupata elimu.

Naye mkurugenzi wa Room To Read amesema kuwa wameanzisha mradi wa mtoto wa kike wa stadi za maisha ili aweze kujitambua na kuwa na maamuzi sahihi na kujiepusha na vishawishi ambavyo ni vikwazo vya kushindwa kupata elimu.

Kwa upande wake Ofisa elimu Mkoa wa Pwani Germana Sondoka amesema kuwa changamoto zinazochangia mtoto wa kike kupata elimu ni nyingi lakini wamekuwa wakijatihidi kushirikiana na wadau kuzikabili.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment