Sunday, October 8, 2017

UJENZI WA BANDARI KAVU KWALA KIBAHA KUPUNGUMZA MSONGAMANO



Na John Gagarini, Kibaha

IMEELEZWA kuwa ukamilikaji wa Bandari Kavu ya Kwala wilayani Kibaha mkoani Pwani itasaidia kupunguza msongamao wa malori Jijini Dar es Salaam kwani makontena yote yanayoingia nchini hayatashushwa kwenye Bandari ya Dar es Salaam badala yake yatashushwa kwenye bandari mpya ya Kwala.

Kutokana na ujenzi huo wa Bandari Kavu ya Kwala mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kupanga mipango mji kwenye Kijiji hicho cha Kwala kwani sasa inaenda kuwa Mji.

Ndikilo aliyasema hayo alipotembelea mradi huo ambao ulianza mwezi Machi mwaka huu ukiwa na thamani ya shilingi bilioni 7.2 ukijengwa na kampuni ya kizalendo ya Suma JKT chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

“Halmashauri mnapaswa kuhakikisha mnaweka mipango miji kwenye eneo hilo ili kusiwe na ujenzi holela pia kuwe na huduma zote kuanzia mahoteli sehemu ya magari kusubiria siyo zije kujengwa na watu binafsi, polisi, mabenki na huduma nyingine muhimu,” alisema Ndikilo.

Alisema kuwa Hlmashauri isisubiri hadi mradi uishe ndiyo ianze kuweka mipangomiji kwani wanatakiwa kwenda sambamba na ujenzi wa mradi ili kuwe na mpangilio mzuri.

“Hichi kitakuwa kitovu cha biashara na kutakuwa na shughuli nyingi hivyo lazima kuwe na mpangilio mzuri wa ujenzi kwani hata barabara ya kuja huku ni mbaya lazima mamlaka zinazohusika zianze kuboresha mazingira na mara kazi zitakapoanza mwakani serikali ijipatie mapato,” alisema Ndikilo.

Naye Meneja mradi Mhandisi Raymond Kweka alisema kuwa wanatarajia kukamilisha Novemba 30 mwaka huu kwa awamu ya kwanza ujenzi huo ambao unaendelea vizuri ukiwa umefikia asilimia 85 kwenye eneo la mradi lenye ukubwa wa hekta zaidi ya 150.

Kweka alisema kuwa baadhi ya changamoto kubwa ni mvua baada ya barabara ya Vigwaza Kwala kukatika na maji kujaa kwenye eneo la mradi, maji yanatoka mbali ambapo mwanzo walitegemea bwawa jirani na mradi ambao limeendelea kukauka na kukosa maji.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Kibaha Beda Mbaga alisema kuwa wanatarajia kuanza kupitia maeneo yanayozunguka mradi huo ili kuweka mipangomiji kuanzia wiki hii kwa 


Mwisho.

No comments:

Post a Comment