Na John
Gagarini, Kibaha
IMEELEZWA
kuwa ukamilikaji wa Bandari Kavu ya Kwala wilayani Kibaha mkoani Pwani
itasaidia kupunguza msongamao wa malori Jijini Dar es Salaam kwani makontena
yote yanayoingia nchini hayatashushwa kwenye Bandari ya Dar es Salaam badala
yake yatashushwa kwenye bandari mpya ya Kwala.
Kutokana na
ujenzi huo wa Bandari Kavu ya Kwala mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist
Ndikilo ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kupanga mipango mji kwenye
Kijiji hicho cha Kwala kwani sasa inaenda kuwa Mji.
Ndikilo
aliyasema hayo alipotembelea mradi huo ambao ulianza mwezi Machi mwaka huu
ukiwa na thamani ya shilingi bilioni 7.2 ukijengwa na kampuni ya kizalendo ya
Suma JKT chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
“Halmashauri
mnapaswa kuhakikisha mnaweka mipango miji kwenye eneo hilo ili kusiwe na ujenzi
holela pia kuwe na huduma zote kuanzia mahoteli sehemu ya magari kusubiria siyo
zije kujengwa na watu binafsi, polisi, mabenki na huduma nyingine muhimu,”
alisema Ndikilo.
Alisema kuwa
Hlmashauri isisubiri hadi mradi uishe ndiyo ianze kuweka mipangomiji kwani wanatakiwa
kwenda sambamba na ujenzi wa mradi ili kuwe na mpangilio mzuri.
“Hichi
kitakuwa kitovu cha biashara na kutakuwa na shughuli nyingi hivyo lazima kuwe
na mpangilio mzuri wa ujenzi kwani hata barabara ya kuja huku ni mbaya lazima
mamlaka zinazohusika zianze kuboresha mazingira na mara kazi zitakapoanza
mwakani serikali ijipatie mapato,” alisema Ndikilo.
Naye Meneja
mradi Mhandisi Raymond Kweka alisema kuwa wanatarajia kukamilisha Novemba 30
mwaka huu kwa awamu ya kwanza ujenzi huo ambao unaendelea vizuri ukiwa umefikia
asilimia 85 kwenye eneo la mradi lenye ukubwa wa hekta zaidi ya 150.
Kweka alisema
kuwa baadhi ya changamoto kubwa ni mvua baada ya barabara ya Vigwaza Kwala
kukatika na maji kujaa kwenye eneo la mradi, maji yanatoka mbali ambapo mwanzo
walitegemea bwawa jirani na mradi ambao limeendelea kukauka na kukosa maji.
Kwa upande
wake kaimu mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Kibaha Beda Mbaga alisema kuwa
wanatarajia kuanza kupitia maeneo yanayozunguka mradi huo ili kuweka
mipangomiji kuanzia wiki hii kwa
Mwisho.
No comments:
Post a Comment