Sunday, October 8, 2017

MKUU WA WILAYA KIBAHA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WATENDAJI




Na John Gagarini, Kibaha

MKUU wa wilaya ya Kibaha Asumter Mshama amesema kuwa serikali inawafanyia tathmini watendaji wa mitaa vijiji na vitongoji na wale ambao watashindwa kufikia vigezo wataondolewa ili kupisha wale wenye weledi wafanyekazi ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Ameyasema hayo mjini Kibaha wakati wa mkutano na viongozi hapo pamoja na wenyeviti kwenye Halmashauri za Mji na wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha na kusema baadhi ya watendaji wamekuwa hawawajibiki ipasavyo.

Nao baadhi ya wenyeviti walielezea changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili kwenye maeneo yao.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Marco Njau alikiri kuwepo kwa baadhi ya changamoto.

Naye kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Beda Mbaga amesema kuwa watakabili changamoto zilizo kwenye eneo lao ili kuleta maenedeleo kwa wananchi.

Naye Ernest Shalua ambaye ni mwakilishi wa Kamanda wa Polisi wilaya ya Kibaha amesema kuwa ili hatua ziweze kuchukuliwa kwa watuhumiwa lazima viongozi na wananchi watoe tushahidi kwenye matukio mbalimbali.

mwisho.  



No comments:

Post a Comment