Na John
Gagarini, Kibaha
MKUU wa
wilaya ya Kibaha Asumter Mshama amesema kuwa serikali inawafanyia tathmini
watendaji wa mitaa vijiji na vitongoji na wale ambao watashindwa kufikia vigezo
wataondolewa ili kupisha wale wenye weledi wafanyekazi ili kuwaletea maendeleo
wananchi.
Ameyasema
hayo mjini Kibaha wakati wa mkutano na viongozi hapo pamoja na wenyeviti kwenye
Halmashauri za Mji na wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha na kusema baadhi ya
watendaji wamekuwa hawawajibiki ipasavyo.
Nao baadhi ya
wenyeviti walielezea changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili kwenye maeneo
yao.
Kwa upande
wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Marco Njau alikiri kuwepo
kwa baadhi ya changamoto.
Naye kaimu
mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Beda Mbaga amesema kuwa
watakabili changamoto zilizo kwenye eneo lao ili kuleta maenedeleo kwa wananchi.
Naye Ernest
Shalua ambaye ni mwakilishi wa Kamanda wa Polisi wilaya ya Kibaha amesema kuwa
ili hatua ziweze kuchukuliwa kwa watuhumiwa lazima viongozi na wananchi watoe
tushahidi kwenye matukio mbalimbali.
mwisho.
No comments:
Post a Comment