ABDUL Zahoro Sharifu
amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo
mkoani Pwani baada ya kumshinda aliyekuwa mwenyekiti Alimasi Masukuzi.
Uchaguzi huo
ambao ulifanyika Msata wilayani humo Sharifu alimshinda mpinzani wake kwa
kupata kura 711 dhidi ya kura 383 za Masukuzi huku Tariq Kafuku akipata kura
185 na nafasi ya Katibu Mwenezi ilikwenda kwa John Francis maarufu kama
Bolizozo aliyepata kura 112 akimshinda Hassan Sharifu aliyepata kura 4.
Kutokana na
ushindi huo Sharifu amesema kuwa chama ndiyo kilichoshinda na siyo yeye na
kuwataka wagombe na wanachama kuwa kitu kimoja ili kukijenga chama kwa ajili ya
kuendelea kushika dola.
“Kuanzia sasa
hakuna makundi makundi yamekwisha baada ya uchaguzi na kila mtu anahaki ya kuwa
na mgombea anayempenda lakini kwa kuwa mshindi kashapatikana hakuna sababu ya
kuwa na makundi,” alisema Sharifu.
Alisema kuwa
baada ya uchaguzi kwisha malengo yake ni kujenga chama kwa kuanzisha vitega
uchumi na kuachana na tabia ya kutegemea kuomba fedha kwa ajili ya kuendesha
shughuli za chama.
“Furaha yangu
ni kuona chama kinajitegemea chenyewe kwa kujiendesha kwani kina miradi mingi
na endapo itasimamiwa vizuri itakiletea manufaa chama,” alisema Sharifu.
Kwa upande
wake Bolizozo alisema kuwa kwa kutumia nafasi yake atahakikisha anashirikiana
na viongozi na wanachama kuleta maenedeleo ya chama ili kiweze kwenye chaguzi
kuanzia ya serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment