Saturday, October 7, 2017

WAFANYABIASHARA MKOA WA PWANI WAFANYA UTALII WA NDANI MIKUMI















Na John Gagarini, Morogoro

WAFANYABIASHARA nchini wametakiwa kuungana na Serikali katika kutangaza vivutio vya Utalii ili kuongeza idadi ya watu wanaotembelea vivutio hivyo na kuongeza pato la Taifa kupitia utalii.

Hayo yalisemwa Mikumi na Abdala Ndauka mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania (JWT) mkoa wa Pwani wakati waliotembelea Mbuga ya wanyama ya Mikumi iliyopo mkoani Morogoro.

Ndauka alisema kuwa wafanyabiashara wananafasi kubwa ya kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo nchini ambavyo havipatikani sehemu yoyote duniani kupitia bidhaa zao wanazozalisha.

“Sisi jumuiya ya wafanyabishara mkoa wa Pwani tumeamua kufungua ukurasa kwa wafanyabiashara kutembelea vivutio vya utalii ambavyo vinavutia watalii wengi nchini na duniani,” alisema Ndauka.

Alisema kuwa ili vivutio vya utalii vitambulike wafanyabishara wana nafasi kubwa ya kuvitangaza na kuongeza watalii wa ndani na nje ya nchi.

“Kwa kuja kwetu huku kuangalia vivutioo hivi tumeweza kujifunza na kuona mengi ambayo tulikuwa tukiyasikia na kuona kupitia vyombo vya habari lakini tumeona wenyewe kwa macho yetu wanyama kama vile Simba,Tembo Swala, Twiga, Nyati, Pundamilia,Viboko na Mamba,” alisema Ndauka.

Aidha alisema kuwa watalii wa ndani wanapaswa kutapembelea vivutio mbalimbali vilivyopo nchini kwani gharama za kuingia kwa sasa zimepungua japo zinapaswa kupungua zaidi ili watu wengi waweze kutembelea.

Kwa upande wake Salugroli Masaga alisema kuwa kwa kutembelea Mbuga hiyo ya Mikumi ameweza kujifunza mambo mengi ikiwiwa ni pamoja na fursa zilizopo kwa wafanyabiashara.

Masaga alisema moja ya fursa ambazo aliziona ni wafanyabiashara kufanyabiashara mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuanzisha migahawa, uuzaji bidhaa za kitalii kama mikufu hereni na mavazi yanayotengenezwa hapa nchini.

“Mbali ya kuona wanyama tumepata fursa ya kujua tabia zao na maisha yao ambayo ni kivutio kikubwa kwani baadhi ya wanyama wanaonekana kama wana tabia tofauti ambazo ni faida kwa wengine,”  alisema Masaga.


Aliwataka wafanyabiashara, vikundi na watu mmojammoja kutembelea pia kutangaza biashara zao kwa kutangaza vivutio hivyo vya kitalii adimu duniani.

Mbuga hiyo ilianzishwa mwaka 1964 ikiwa na ukubwa wa kilometa za mraba 1,070 na iliongezwa ukubwa na kufikia kilometa za mraba 3,200 mwaka 1975 ikiwa ni ya tano kwa ukubwa kwa Mbuga za Taifa.

Mbuga inayoongoza ni Ruaha yenye ukubwa wa Kilometa za mraba 20,226, Serengeti yenya ukubwa wa Kilometa za mraba 14,763 na Mkomazi yenye ukubwa wa Kilometa za mraba 3,245 ikiwa na wanyama wakubwa aina nne kati ya tano ambao ni Simba,Tembo, Nyati na Chui

Mwisho.  

No comments:

Post a Comment