Saturday, October 7, 2017

MAMIA YA WANANCHI WALILIA AJIRA WAMOMBA RC AWASAIDIE






Na John Gagarini, Kibaha

MAMIA ya wananchi wa wilaya ya Kibaha na mkoa wa Pwani wamelilia mkuu wa mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo awasidie kupata ajira wazuia msafara wake kwa mabango kwenye kituo cha ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro kilichopo kwenye Kijiji cha Soga inayojengwa na kampuni ya Yapi Merkezi ya nchini Uturuki.

Wananchi hao walifikia hatua hiyo wakati mkuu wa mkoa wa Pwani akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ilipotembelea kujionea ujenzi huo ambao tayari umeanza na kusema kuwa watu wa mkoa huo wamekuwa wakibaguliwa na kuajiriwa watu kutoka Jijini Dar es Salaam zaidi wananchi hao.

Kwa upande wa Rukia Ally amesema kuwa wametumia gharama kubwa kujenga mabanda wanayofanyia biashara hiyo ya chakula na wamekopa mikopo kwenye taasisia za kifedha hali ambayo inawapa wasiwasi huenda wakauziwa mali zao.

Ally amesema kuwa wanahofu kuuziwa mali zao kwani watashindwa kurudisha fedha walizokopa kwa ajili ya kujenga mabanda na kunuanua bidhaa kwa ajili ya biashara hiyo hivyo kumwomba mkuu wa mkoa kuwasaidia ili kampuni hiyo iruhusu waendelee kupata huduma ya chakula nje na si ndani kwa mzabuni.

Kwa upande wake meneja mradi kutoka kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Mhandisi Maizo Mgedzi amesema kuwa wao wanaajiri kutokana na sifa za waombaji ambao wengi ni madereva na waendeshaji wa mitambo.
Kutokana na malalamiko hayo mkuu huyo wa mkoa wa Pwani ametoa siku saba kwa vyombo vya dola kufutailia suala la rushwa kama lipo na kutaka wahusika waliotajwa na wananchi hao kusimama kupisha uchunguzi.

Aidha ametaka kupelekewa majina ya watu waliajiriwa kama wanatoka mkoa wa Pwani au la kwani serikali imekuwa ikitaka wanufaika wa kwanza wawe wanaoishi kwenye eneo la mradi.

Pia ametaka utaratibu wa chakula nao uangaliwe ili akina baba na mama lishe walioko nje ya eneo hilo la mradi huo waruhusiwe kuendelea kufanyabishara badala ya kuwazuia wafanyakazi wasitoke nje baada ya kupewa mazabuni kwa ajili ya kuwapa chakula.

Naye mwakilishi wa mkandarasi wa kampuni hiyo Merz Oz alisema kuwa waliamua kuacha utaratibu wa wafanyakazi wao kula chakula nje kwa madai kuwa wanatumia muda mwingi na kufanya shughuli kushindwa kufanyika kwa wakati.

Oz alisema kuwa sababu nyingine ni kuhakikisha wafanyakazi wanapata chakula chenye ubora hasa ikizingatiwa kampuni yao ni ya kimataifa hivyo haiwezi kuwaacha wafanyakazi wao wanakula bila ya utaratibu na huwapatia bure chakula hicho jambo ambalo lilipingwa na wananchi.

Mwisho.



No comments:

Post a Comment