Na John
Gagarini, Kibaha
MTAA wa Maili
Moja umesema utawafuatialia na kuwachukulia hatua mgambo ambao waliwadhalilisha
akina mama wafanyabiashara ndogo ndogo kwa kuwadai rushwa ya ngono kwa
madai kufanyabiashara kwenye eneo ambalo haliruhusiwi.
Akizungumza
kwenye mkutano wa mtaa mwenyekiti wa Mtaa wa maili Moja Athuma Mkongota alisema
kuwa baadhi ya akinamama walilalamika ofisini kwake kuwa walitakiwa watoe penzi
ili wasitozwe faini kwa kudaiwa kufanya biashara kwenye maeneo yaliyokatazwa.
Mkongota
alisema kuwa jambo la kushangaza akinamama hao waliokuwa wakifanyabiashara nje
ya eneo la Hifadhi ya Barabara ambapo waliondolewa kufuatia kubomolewa soko la
zamani la Maili Moja.
“Hawa mgambo
walifanya makosa kuwanyanyasa akinamama hawa hata kama walikuwa na makosa
taratibu za wanaokiuka sheria sizipo kwanini wadai mapenzi pia walikuwa
hawafanyibiashara kwenye eneo lililokatazwa hivyo tutawatafuta na kuwapeleka
kwenye vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua,” alisema Mkongota.
Mkongota
alisema kuwa baada ya wakinamama hao kuondolewa eneo lililokatazwa la hifadhi
ya barabara ambalo liko jirani na stendi walienda kwenye barabara za mitaa na
kuendelea kufanyabiashara lakini mgambo hao waliwafuata na kuwakamata huku
wakimwaga vyakula na matunda waliyokuwa wakiyauza.
“Baadhi ya
akinamama walifika ofisini na kudai kuwa baadhia ya mgambo walikuwa wakiwataka
kimapenzi ili wasiwapige faini wakidai kuwa wanachafua mazingira jambo hili
halikubaliki kwani tutawatafuta na wakibainika watepelekwa sehemu husika kwnai
kuna baadhi wanajifanya mabwana afya,” alisema Mkongota.
Kwa upande
wake Mwanahamisi Shomary ambaye ni muuzaji wa samaki alisema kuwa tangu
waondolewe kwenye eneo la stendi na kuhamia kwenye barabara za mitaa wamekuwa
wakisumbuliwa na mgambo hao.
Shomary
alisema kuwa mgambo hao wamekuwa kero kubwa kwani wanatunyanyasa sana huku
wakichukua bidhaa zetu na kuziharibu ambapo inabidi tujitafutie ili tuweze
kurejesha mikopo tuliyokopa.
Mwisho.