Na John
Gagarini, Kibaha
WANANCHI wa
kata ya Picha ya Ndege wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kuacha kununua
nyama zinazouzwa mitaani kwa bei nafuu kwani ni hatari kwa maisha yao.
Hayo
yalisemwa na diwani wa kata hiyo Robert Machumbe alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari kufuatia kuenea kwa taarifa kuwa kuna watu wanauza nyama
mitaani zikiwa zimewekwa kwenye ndoo.
Machumbe
alisema kuwa watu hao wamekuwa wakichukua ngombe ambao wamekufa maeneo
mbalimbali kisha kuwauzia wanachi nyama hiyo kwa baei nafuu ya shilingi 2,000.
“Wananchi
nawaomba mjihadhari na nyama hizi zinazouzwa mitaani ni hatari kwa afya zenu
kwani hamjui nyama hizo zinatoka wapi kwani hazijapimwa na daktari hali ambayo
ni hatari,” alisema Machumbe.
Alisema kuwa
wananchi wasipende kununua nyama hizo bali wanunue sehemu maalumu ambako ni
kwenye mabucha ya kuuzia nyama ili wale nyama ambayo imepimwa na ni salama kwa
afya zao.
Kwa upande
wake ofisa mifugo wa kata ya Picha ya Ndege Mlaki alisema kuwa alipata taarifa wiki
iliyopita kuwa kuna ngombe walikufa kwa moja ya wafugaji wa Lulanzi na watu hao
waliichukua nyama hiyo na kuiuza mtaani.
Mlaki alisema
kuwa kuna athari ningi zinazotokana na watu kula nyama ambazo hazijapimwa kwani
wanaweza kuambukizwa magonjwa mbalimbali kama vile tb, tumbo, kuharisha na
magonjwa mengine.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment