Na John
Gagarini, Kibaha
DEREVA wa
gari la mizigo ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja amekufa baada
ya gari alilokuwa akiliendesha kugongwa na gari lingine kwenye ajali
iliyosababisha magari matatu kugongana.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa mjini Kibaha kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi
mkoani Pwani Jonathan Shana ilisema kuwa katika tukio hilo mtu mmoja
alijeruhiwa.
Kamanda Shana
alisema kuwa tukio hilo lilitokea Julai 20 majira ya saa 4:20 usiku barabara
kuu ya Dar es Salaam Morogoro eneo la Picha ya Ndege wilayani Kibaha.
Shana alisema
kuwa gari aina ya Scania lenye namba za usajili T 774 BBU likiendeshwa na
dereva asiyefahamika liligonga gari lililokuwa likiendeshwa na dereva
asiyefahamika lenye namba za usajili T 678 BRD lenye tela namba T 293 BVA na
Scania T 188 AVN likiendeshwa na Hashimu Mhina (36) wa Dar es Salaam.
“Chanzo cha
ajali hii ni dereva wa gari la kwanza kuyapita magari mengine bila ya kuchukua
tahadhari ambapo alikimbia mara baada ya ajali hiyo na tunamtafuta tumempa siku
tatu ajitokeze na asipojitokeza tutamtafuta ili afikishwe kwenye vyombo vya
sheria,” alisema Shana
Mwisho
Na John
Gagarini, Kibaha
JESHI la
Polisi mkoani Pwani linawashikilia wahamiaji 44 kutoka nchi ya Ethiopia kwa tuhuma
za kuingia nchini bila ya kibali.
Akizungumza
na waandishi wa habari mjini Kibaha kamanda wa Polisi mkoani Pwani Jonathan
Shana alisema kuwa wahamiaji hao haramu walikamatiwa wilayani Bagamoyo.
Kamanda Shana
alisema kuwa wahamiaji hao haramu walikamatwa eneo la Razaba kata ya Makurunge
Tarafa ya Mwambao wilayani humo wakiwa wametelekezwa kwenye ufukwe wa Bahari ya
Hindi.
Alisema kuwa kufuati tukio hilo jeshi lake linaendelea na
uchunguzi kujua watu waliohusika na tukio la kuwasafirisha wahamiaji hao haramu
kisha kuwatelekeza.
“Tunafuatilia
kujua vitu vingi ikiwa ni pamoja na wanaowafadhili wahamiaji hao haramu kwani
kumekuwa na baadhi ya watu wanaowasafirisha wahamiaji hao ili hatua za kisheria
ziweze kuchukuliwa dhidi yao,” alisema Shana.
Mwisho
No comments:
Post a Comment