Thursday, July 27, 2017

AKIMAMA WAFANYABIASHARA WALALAMIKA KUNYANYASWA


                                    Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Maili Moja umesema utawafuatialia na kuwachukulia hatua mgambo ambao waliwadhalilisha akina mama wafanyabiashara ndogo ndogo kwa kuwadai rushwa ya ngono kwa madai kufanyabiashara kwenye eneo ambalo haliruhusiwi.

Akizungumza kwenye mkutano wa mtaa mwenyekiti wa Mtaa wa maili Moja Athuma Mkongota alisema kuwa baadhi ya akinamama walilalamika ofisini kwake kuwa walitakiwa watoe penzi ili wasitozwe faini kwa kudaiwa kufanya biashara kwenye maeneo yaliyokatazwa.

Mkongota alisema kuwa jambo la kushangaza akinamama hao waliokuwa wakifanyabiashara nje ya eneo la Hifadhi ya Barabara ambapo waliondolewa kufuatia kubomolewa soko la zamani la Maili Moja.

“Hawa mgambo walifanya makosa kuwanyanyasa akinamama hawa hata kama walikuwa na makosa taratibu za wanaokiuka sheria sizipo kwanini wadai mapenzi pia walikuwa hawafanyibiashara kwenye eneo lililokatazwa hivyo tutawatafuta na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua,” alisema Mkongota.

Mkongota alisema kuwa baada ya wakinamama hao kuondolewa eneo lililokatazwa la hifadhi ya barabara ambalo liko jirani na stendi walienda kwenye barabara za mitaa na kuendelea kufanyabiashara lakini mgambo hao waliwafuata na kuwakamata huku wakimwaga vyakula na matunda waliyokuwa wakiyauza.

“Baadhi ya akinamama walifika ofisini na kudai kuwa baadhia ya mgambo walikuwa wakiwataka kimapenzi ili wasiwapige faini wakidai kuwa wanachafua mazingira jambo hili halikubaliki kwani tutawatafuta na wakibainika watepelekwa sehemu husika kwnai kuna baadhi wanajifanya mabwana afya,” alisema Mkongota.

Kwa upande wake Mwanahamisi Shomary ambaye ni muuzaji wa samaki alisema kuwa tangu waondolewe kwenye eneo la stendi na kuhamia kwenye barabara za mitaa wamekuwa wakisumbuliwa na mgambo hao.

Shomary alisema kuwa mgambo hao wamekuwa kero kubwa kwani wanatunyanyasa sana huku wakichukua bidhaa zetu na kuziharibu ambapo inabidi tujitafutie ili tuweze kurejesha mikopo tuliyokopa.


Mwisho.   

No comments:

Post a Comment