Na John Gagarini, Kibaha
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amekubali maombi ya Kituo cha Afya cha Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani kuwa Hospitali ya wilaya.
Alitoa tamko
hilo kwenye uwanja wa Mtongani Mlandizi wilayani Kibahya wakati akipokea
Magari mawili ya kubeba wagonjwa na vitanda vitatu vya kuzalishia mama
wajawazito kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa na gari
moja kutoka kwa Rais Dk John Magufuli.
Alisema kuwa
ombi lililotolewa na Mbunge huyo kwa viongozi wa ngazi za juu na kwake
amelikubali hivyo mganga mkuu wa wilaya anapaswa kuandika barua na kuzipeleka
sehemu husika kisha zifikishwe wizarani kwa ajili ya utekelezaji.
“Mbunge wenu
amekuwa akipigania kituo hichi kwa muda mrefu kama alivyosema hivyo naona
hakuna kipingamizi ili mradi tu taratibu zifuatwe ili kufikia hatua hiyo lengo
kubwa ni kuboresha huduma kwa wananchi,” alisema Mwalimu.
Awali mbunge
wa Jimbo hilo Hamoud Jumaa lisema kuwa maombi hayo alishayatoa kwa viongozi
mbalimbali ikiwemo kwa Rais wa Awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete na Rais Dk John
Magufuli.
Jumaa alisema
kuwa kituo hicho kwa sasa kinahudumia watu wengi tofauti na ilivyokuwa zamani
ambapo kwa sasa wanakaribia watu 100,000 hivyo kuna haja kabisa ya kuwa
hospitali ya wilaya.
“Tuliambiwa
tufanye maboresho mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenga jengo la upasuaji,
chumba cha kuhifadhia maiti pamoja na kuweka uzio vitu vyote hivyo tayari
tumevifanya hivyo ombi letu hilo tunaomba ulifanyie kazi kwani tunaamini huduma
zitaboreka,” alisema Ummy.
Kwa upande
wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibaha Beda Mmbaga alisema kuwa
watahakikisha wanaboresha mahitaji yote yanayotakiwa ili kutoa huduma za ubora
kwa wananchi wanaokwenda kuhudumiwa hapo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment