Thursday, July 27, 2017

MWANAMKE AUWAWA KINYAMA

                                      
                                         Na John Gagarini, Kibaha

MWANAMKE mmoja ambaye ni mfanyabiashara Mariamu Omary (31) mkazi wa Mtaa wa Muharakani wilayani Kibaha mkoani Pwani ameuwawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari mjini Kibaha na Blasius Chatanda kwa niaba ya kamanda wa polisi mkoani Pwani alisema kuwa marehemu aliuwawa na watu wasiofahamika.

Kamanda Chatanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea eneo la Kwa Mathias majira ya saa 7 usiku umbali wa mita 40 toka kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.

“Marehemu alikutwa asubuhi huku akiwa amevuja damu nyingi sehemu za usoni na kichwani na alikutwa na jeraha kubwa kichwani upande wa kushoto,” alisema Chatanda.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Muharakani Hamis Mwarizo alisema kuwa marehemu alipigiwa simu usiku na mtu ambaye jina lake linaonekana kwenye simu ya marehemu.

Mwarizo alisema kuwa waliingia kwenye chumba cha marehemu na kuzikuta simu zake mbili na moja inaonyesha ilipigwa usiku huo na inaonekana baada ya kupigiwa ndipo alipotoka ndipo alipokutwa na umauti.

Naye mama mwenyenyumba Miriamu John alisema kuwa marehemu alikuwa ni mgeni kwenye nyumba yake akiwa na miezi akiwa na miezi miwili tu na siku ya tukio hawakuweza kusikia kitu chochote.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment