Na John
Gagarini,Kibaha
MADEREVA
wawili wamekufa baada ya gari walilopanda kugonga kingo za daraja la mto wa
wami na kuangukia mtoni
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Jonathan Shana amesema
kuwa gari lililopata ajali ni mali ya kampuni ya Usangu Logistics.
Shana amesema
kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa saba usiku na kulihusisha gari lenye
usajili namba T 857 ARP aina ya Scania likiendeshwa na Yahaya Karimu miaka kati
ya (30) na (35) akiwa na dereva mwenzake
ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja likitokea Dar es Salaam kwenda
Arusha.
Amesema kuwa
chanzo cha ajali hiyo ni breki za gari hilo kukatika na kugonga kingo za daraja
hilo kisha kuanguka mtoni
Na John
Gagarini, Kibaha
MTU mmoja
aliyetambulika kwa jina la Mwesigwa Mberwa (23) amekutwa amekufa kwenye nyumba
ya kulala wageni ya Msukuma iliyopo Mlandizi wilayani Kibaha.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Kibaha na kamanda wa Polisi
mkoani Pwani Jonathan Shana zimesema kuwa marehemu alikuwa amelala chumba namba
38.
Shana amesema
kuwa tukio hilo lilitokea Julai 22 majira ya saa 12 jioni eneo la kitongoji cha
Usalama wilaya ya Kipolisi Mlandizi ambapo marehemu alipanga kwenye nyumba hiyo
tangu Julai 19.
Amebainisha
kuwa muhudumu Kulekwa Kulwa ndiye aliyegundua kufa kwa marehemu baada ya kutia
mashaka kutokana na kutomwona kutoka nje mteja wake tangu alipoingia na kwenda
kutoa taarifa polisi.
Amesema kuwa
polisi walipofika kwenye chumba hicho iliwabidi kuvunja mlango na kuukuta mwili
wa marehemu ukiwa hauna jeraha lolote mwilini mwake na kupelekwa hospitali
Teule ya Rufaa ya mkoa ya Tumbi na ulifanyiwa uchunguzi na utakabidhiwa kwa
ndugu kwa ajili ya mazishi.
Mwisho.
Na John Gagarini,
Kibaha
ABIRIA
waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Tashirifu waliokuwa wakisafiri
kutokea Dar es Salaam kwenda mkoani Tanga wamenusurika kifo baada ya basi hilo
kuwaka moto.
Kwa mujibu wa
taarifa ya kamanda wa polisi mkoani Pwani kwa vyombo vya habari Jonathan Shana
imesema kuwa basi hilo liliteketea lote na moto huo haukuleta madhara yoyote
kwa binadamu na kusababisha hasara ikiwemo mizigo ya abiria.
Kamanda Shana
amesema kuwa ajali hiyo ilitokea Julai 22 majira ya usiku eneo la Kwa Zoka kata
ya Vigwaza wilaya ya Kipolisi Chalinze barabara kuu ya Dar es Salaam Morogoro.
Amesema kuwa
basi hilo lenye namaba za usajili T 681 DFX aina ya Yutong lilikuwa
likiendeshwa na dereva aitwaye Salum Issa (42) liliwaka moto hata hivyo chanzo
cha moto huo hakikuweza kufahamika mara moja na polisi wanaendelea na uchunguzi
kujua chanzo cha moto huo.
Mwisho.
Na John
Gagarini, Kibaha
JESHI la
Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu sita kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba
za watu watatu na kusababisha hasara ikiwa ni pamoja na pikipiki mbili zenye
thamani ya shilingi milioni 3.8
Kamanda wa
polisi mkoani humo Jonathan Shana amesema kuwa mbali ya kuchoma nyumba hizo pia
waliingia kwenye mazizi na kuchinja ngombe ambao idadi yao haijajulika kisha
kuondoka na nyama na kubakiza utumbo.
Shana amesema
kuwa tukio hilo lilitokea Kijiji cha Vikumburu kata ya Vikumburu Tarafa ya
Chole wilaya ya Kisarawe ambapo hata hivyo haikuweza kufahamika chanzo cha
uhabifu huo wa mali ambao thamani yake haijajulikana.
Amewataja watu
waliochomewa nyumba zao kuwa ni Joseph Simboyi (55), Rebeka Yona (23) na Selina
Simon (28).
Aidha
amewataja watuhumiwa wa tukio hilo kuwa ni Abdala Shomary (53), Omary Athuman
(42) Seifu Shomary (38), Uzalimata Selasela (36) Salum Shomary (40) na Jumanne
Omary (49) wote wakazi wa Vikumburu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment