Thursday, July 27, 2017

WAASWA KUTUMIA VITUO VYA MAFUNZO

                                      Na John Gagarini, Kibaha

WALIMU wakuu wa shule za msingi, sekondari na vyuo nchini wameshauriwa kuwapeleka wanafunzi wao kwenye vituo vya mafunzo badala ya kuwapeleka kwenye sehemu za starehe.

Ushauri huo umetolewa na makamu mwenyekiti wa wataalamu wasaidizi wa mifugo nchini Tavepa Ephrahim Masawe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Masawe ambaye pia ni mkurugenzi wa shamba darasa Kibaha akizungumzia juu ya kilimo cha kisasa alisema kuwa ziara za safari ni vema zikawa za kujifunza kuliko kujifurahisha.

“Kwenye mafunzo hujifunza mambo mengi kuliko kwenda kwenye sehemu ambazao hazina faida kwani ujuzi unaweza kumsaidia mtu kuliko kufanya vitu visivyo na faida,” alisema Masawe.

Naye moja ya wanafunzi kwenye shamba darasa mkazi wa Mbweni Jijini Dar es Salaam Hilda Ngowi akiezea kilicho msukuma kwenda hapo kujifunza ni kutaka kupata ujuzi wa ufugaji wa kuku.

Ngowi alisema ushauri juu ya shule na vyuo kuwapeleka wanafunzi kwenye sehemu za mafunzo kama hayo alisema kuwa sehemu za mafunzo ni muhimu kwa vijana.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment