Na John
Gagarini, Kibaha
WALIMU wakuu
wa shule za msingi, sekondari na vyuo nchini wameshauriwa kuwapeleka wanafunzi
wao kwenye vituo vya mafunzo badala ya kuwapeleka kwenye sehemu za starehe.
Ushauri huo
umetolewa na makamu mwenyekiti wa wataalamu wasaidizi wa mifugo nchini Tavepa
Ephrahim Masawe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
Masawe ambaye
pia ni mkurugenzi wa shamba darasa Kibaha akizungumzia juu ya kilimo cha kisasa
alisema kuwa ziara za safari ni vema zikawa za kujifunza kuliko kujifurahisha.
“Kwenye
mafunzo hujifunza mambo mengi kuliko kwenda kwenye sehemu ambazao hazina faida
kwani ujuzi unaweza kumsaidia mtu kuliko kufanya vitu visivyo na faida,”
alisema Masawe.
Naye moja ya
wanafunzi kwenye shamba darasa mkazi wa Mbweni Jijini Dar es Salaam Hilda Ngowi
akiezea kilicho msukuma kwenda hapo kujifunza ni kutaka kupata ujuzi wa ufugaji
wa kuku.
Ngowi alisema
ushauri juu ya shule na vyuo kuwapeleka wanafunzi kwenye sehemu za mafunzo kama
hayo alisema kuwa sehemu za mafunzo ni muhimu kwa vijana.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment