Thursday, July 27, 2017

AUWAWA NA WANANCHI HASIRA KWA TUHUMA WIZI WA BODABODA

                                   
                                      Na John Gagarini,Kibaha

MTU mmoja anayedhaniwa kuwa ni jambazi mmoja ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa kisha kuchomwa moto kwa tuhuma za kupora pikipiki.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Jonathan Shana alisema kuwa kuwa tukio hilo lilitokea Julai 23 majira ya saa 1:45 usiku kitongoji cha Amani kata ya Kerege tarafa ya Yombo wilaya ya Bagamoyo.

Kamanda Shana alisema kuwa marehemu akiwa na wenzake watatu wakiwa na silaha inayodhaniwa kuwa ni bastola walimvamia mwendesha pikpiki aitwaye Mbaraka Joel (25) mkazi wa Amani walimpora pikipiki yake yenye namba za usajili T 852 BRA aina ya Sanlg.

“Watu hyao kabla ya kufanya uporaji walimsimamisha wakijifanya kuwa ni abiria lakini ghafla walimbadilikia kwa kufayatua risasi mbili hewani na kumtaka awape pikipiki ambayo aliiachia na kutoweka nayo kusikojulikana,” alisema Shana.

Alisema baada ya taarifa kulifikia jeshi la polisi wilaya ya Bagamoyo waliendesha msako mkali kwa kushirikiana na wananchi kupitia vikundi vyao vya ulinzi shirikishi kwenye maeneo mbalimbali likiwemo eneo la Mtambani.

“Wananchi hao waliweza kuwakurupusha watu hao wakiwa wanapanga mipango ya kwenda kufanya uhalifu sehemu nyingine na kutokana na idadi ya wananchi kuwa kubwa watu hao walikimbia na kutelekeza pikipiki mbili moja walioipora kwa Joel na nyingine yenye namba za usajili T MC 972 AJM aina ya Boxer,” alisema Shana.

Aidha alisema kuwa wananchi hao waliendelea kuwakimbiza na kufanikiwa kumkamata marehemu ambapo walimpiga kwa mawe na marungu kisha kumchoma moto na kupoteza maisha papo hapo.

“Wananchi hawapaswi kujichukulia sheria mikononi kwa kuwaua wahalifu wanapaswa kuwakabidhi polisi kwa ajili ya hatua za kisheria pia wataweza kubaini mtandao wa wizi kuliko kuwaua,” alisema Shana.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment