Na John Gagarini, Pwani
WATU wasiofahamika wameendelea kufanya mauaji wilayani Kibiti ambapo wamewaua viongozi wawili wa Kijiji cha Mangwi kata ya Mchukwi kwa kuwapiga.
Viongozi waliouwawa ni pamoja na Michael Nicholaus Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mangwi na mtendaji wa Kijiji hicho Shamte Makawa.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 27 majira ya usiku kwenye Kijiji hicho na watu hao baada ya kufanya tukio hilo walichoma nyumba moto kisha kutoweka.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Pwani Onesmo Lyanga alipoulizwa juu ya tukio hilo alikiri kutokea na kusema kuwa bado wanaendelea kufuatilia ili kuwabaini wahusika wa matukio hayo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment