Na John
Gagarini, Kibaha
WATU wenye
uwezo mkoani Pwani wametakiwa kumtukuza Mungu katika kipindi hichi cha mfungo
mtukufu wa Ramadhan kwa kuwasaidia watu wenye mahitaji ili wapate thawabu.
Hayo yalisemwa
jana mjini Kibaha na msaidizi wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mkoani Pwani,
Method Mselewa ambaye alimwakilisha mbunge
huyo Silvestry Koka wakati wa kutoa mkono wa Iddi kwa waumini wa dini ya
Kiislamu kutoka misikiti mbalimbali wilayani hapa.
Mselewa alisema
kuwa kutoa wakati wa kipindi hichi ni sadaka ambayo ina manufaa makubwa kwa
waislamu hivyo wawe na moyo wa kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao wajisikie
kama kuna watu wanawajali.
“Mbunge kila
mwaka kipindi kama hichi amekuwa akijitolea kwa makundi hayo ambayo ni pamoja
na wazee, yatima, wajane na wale wasiojiweza ambapo kila msikiti wanatoka watu
20 ili nao waweze kuandaa futari kwa familia zao,” alisema Mselewa.
Alisema kuwa
waumini hao wanatoka kwenye misikiti 64 iliyopo katika Jimbo la Kibaha ambapo
kila mmoja anapewa mkono wa Iddi ambao ni mchele kilogramu mbili, sukari
kilogramu moja na fedha kwa ajili ya kununulia mboga.
“Watu
wamekuwa wakifuturisha kwa kuwalisha watu chakula lakini Mbunge kaamua kubadili
staili kwa kuwapa vyakula hivyo ambapo wao watenda kuziandalia familia zao
tofauti na kuwapa chakula ambapo watakaokula ni wachache tofauti na
watakapopeleka nyumbani kuandaa wenyewe kwani yeye hawezi kuja na familia balia
atakuja mtu mmoja,” alisema Mselewa.
Aidha alisema
kuwa mbali ya kuwapatia vitu hivyo pia huwapatia ujumbe wa Iddi wa kudumisha
amani, upendo na ushirikiano kwa watu wote katika kipindi hichi na nyakati
zingine ambazo si za mfungo.
Alibainisha kuwa
mbali ya makundi hayo pia mkono wa Iddi unatolewa kwa viongozi wa chama
wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Baraza la Wanawake (UWT), Baraza
la Wazazi na Umoja wa Vijana (UVCCM) ambapo jumla ya watu 2,000 watafikiwa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment