Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA cha soka Kibaha Vijijini wilayani Kibaha mkoani Pwani
(KIVIFA) kinatarajia kuchagua timu ya vijana wenye umri wa miaka 15 ya Copa
Coca Cola Agosti 16 mwaka huu.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa wa mashinadano wa (KIVIFA)
Mohamed Msamati amesema kuwa tayari wameshakaa na vilabu 11ili kuwaelekeza
namna ya kufanya mashindano hayo.
Msamati amesema mashindano hayo yatafanyika ili kutekeleza
agizo la Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA), kila wilaya kuhakikisha inapata
timu ya vijana kwa ajili ya mashindano ya mkoa.
Amesema kuwa kuwa kwa sasa wako kwenye maandalizi ya michuano
hiyo ambayo itashirikisha timu zote za Kibaha Vijijini na kuzitaka timu
kujiandaa na mashindano.
Aidha amesema kuwa Kila timu inapaswa kuandaa wachezaji wake
kwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kuhakikisha wilaya inapata wachezaji wazuri
watakaowakilisha kwenye mashindano ya mkoa.
Amebainisha kuwa watahakikisha mashindano hayo yanatumia
wachezaji ambao wana umri unaopaswa na kuepukana na kutumia wachezaji ambao
wana umri mkubwa maarufu kama vijeba.
Kwa upande wake mwenyekiti wa KIVIFA Meja Mstaafu Deus Makwaya
amesema wamejipanga vizuri katika kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa na
kupata timu bora.
Meja Makwaya amesema kuwa tayari wameteua viongozi kwa ajili
ya kusimamia mashindano hayo ya Copa Cola Cola ambao ni Dk Musa Sama ambaye ni
mwenyekiti, Juma Likali katibu na God Mwafulilwa meneja.
Amewataja wajumbe kuwa ni Hija Matitu, Juma Kisebengo, Said
Kidile huku walimu wakiwa ni Said Shaban na Mtoso ambao ni timu ya ushindi ya
kuandaa vijana hao.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment